Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Haji Khatib Kai

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Micheweni

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. HAJI KHATIB KAI: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote nimshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunipa fikra za kuchangia kwa maandishi. Kwanza kabisa nimpongeze Mheshimiwa Waziri kwa kuteuliwa tena kuongoza Wizara hii muhimu ili aweze kutimiza azma yake kwenye sekta ya ardhi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mchango wangu napenda niuelekeze kwa Mheshimiwa Waziri na nitamtaka wakati wa kufanya majumuisho nipate majibu ya maswali yangu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la kwanza, Bunge la mwaka 2010 akiwa Waziri wa Wizara hii alisimamia Kamati ya Ardhi, Maliasili kwenda nchini Uganda kujifunza ni namna gani Uganda wamefanikiwa katika sekta ya ardhi. Pia Kamati ilijifunza ni namna gani na muda gani wananchi wa Uganda wanapoanza mchakato wa kumiliki ardhi na jinsi zoezi hilo linavyokwenda haraka yaani si zaidi ya wiki moja mwananchi wa Uganda anakuwa amemiliki ardhi. Kamati ya Ardhi iliyopita nikiwa mmoja wa Wajumbe tulishauri Serikali kupitia Wizara hii kufanya jambo hili. Je, kwa sisi Tanzania na ili jambo hili liweze kupunguza kero na msongamano kwenye ofisi za ardhi limefikia wapi?
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia Kamati iliyopita ilienda nchini Dubai kujifunza kwenye Shirika lao la Nyumba. Kamati ilishauri Shirika la Nyumba lipewe mamlaka yake, lijitegemee na lijiendeshe. Je, suala hili hadi sasa limefikia wapi ili Shirika la Nyumba lifanye shughuli zake kwa ufanisi zaidi? Ahsante sana.