Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Mbaraka Salim Bawazir

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilosa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. MBARAKA S. BAWAZIR: Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza Mheshimiwa Waziri kwa kusaidia sana katika kutatua migogoro baina ya wakulima na wafugaji katika Jimbo langu la Kilosa. Nashukuru sana kwa ushirikiano mliotupa japokuwa bado kuna matatizo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba mashamba ya Usagala A&B yaende kwa wakulima. Mashamba hayo yanamilikiwa na SINO Development Tanzania Limited (Usagara Sisal Estate). Wafugaji wapewe Mkata Ranch, Kandoro Ranch na Lukumai Ranch kwani maeneo haya yanafaa sana kwa wafugaji. Hali kwa sasa sio nzuri, watu wanalinda usiku na mchana mazao yao kuogopa wafugaji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba sana Serikali pamoja na mambo mazuri waliyoyafanya katika Jimbo la Kilosa wazingatie ushauri wangu kwa maslahi ya wananchi wa Kilosa. Naunga mkono hoja asilimia mia moja.