Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. ENG. EDWIN A. NGONYANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuunga mkono kwa asilima mia moja hoja ya Mheshimiwa Waziri ya Bajeti ya mwaka 2016/2017. Nimshukuru sana Mheshimiwa Waziri kwa namna unavyomsaidia Mheshimiwa Rais kuikuza nchi hii kupitia utatuzi wa migogoro ya ardhi kati ya wakulima, wafugaji, wawekezaji na maeneo ya hifadhi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimuombe Waziri anisaidie katika Jimbo langu la Namtumbo katika maeneo yafuatayo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, tumezindua mji mdogo wa Lusewa tarehe 4/4/2016 kwa kumteua TEO na Maafisa Ardhi wapime. Tunahitaji mji huo mdogo upimwe na kuainisha maeneo ya matumizi mbalimbali. Mchango wenu unahitajika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jedwali namba 138 la hotuba ya Mheshimiwa Waziri katika ukurasa 144 inayosema Shirika la Nyumba limenunua ekari zao katika Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo si sahihi, NHC ilitengewa viwanja 40 katika eneo linalopakana na TANESCO, viwanja vya low density, lakini NHC hawajatoa fedha za fidia na kwa sababu NHC hawatoi ushirikiano wowote kuhusu fidia na mpango wao wa kujenga nyumba hizo, Halmashauri inakusudia kugawa viwanja hivyo kwa wahitaji wengine watakaokuwa tayari kutoa fedha za fidia. Masharti ya kuitaka Halmashauri izinunue nyumba zitakazojengwa na NHC na kulipa fidia hayajakubalika na kwa kweli hayatekelezeki.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mipaka ya hifadhi ya Sebu inapanuliwa bila ya taarifa kwa vijiji husika vinavyoguswa na upanuzi. Vijiji vinavyohusika ni vya Kitanda, Mpuka, Luhangano, Mhangazi, Nangero, Nambecha, Likuyu mandela na kadhalika. Vijiji hivyo vitatenga sehemu ya ardhi yao kama Hifadhi ya Jamii (WMA) chini ya umoja wao wa Mbarang‟andu. Hivi sasa wanavijiji husika wanataka kurekebisha mpaka wa WMA waliojiwekea mwaka 1992 ili kupata eneo zaidi la kilimo kufuatia kuongezeka kwa wakazi wa upande mmoja na upanuaji wa mipaka ya hifadhi za kitaifa za Selous Game Reserve na Undendeule Forest Reserve; upanuzi huo unaochukua maeneo ya WMA kwa upande wa pili. Mazingira haya yanaleta mgogoro unaoanza kukiathiri CCM kwa kupoteza kata ya Mputa na vurugu za wakulima kuchomewa nyumba zao na kufyekwa mazao yao mashambani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tafadhali Mheshimiwa William Vangimembe Lukuvi, Mbunge wa Isimani na Waziri mahiri tusaidie kuituliza Namtumbo na Halmashauri yake kwa kurekebisha kasoro hizo hapo juu.
Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.