Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. JAPHET N. HASUNGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, mchango wangu upo katika maeneo yafuatayo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza ni ukosefu wa mfumo wa kimenejimenti ambao ni unganishi (Integrated Land Management System). Mfumo huu utashirikisha Wizara karibu zote ambazo majukumu yao yanategemea kuwepo kwa ardhi ya kutosha. Kwa mfano Wizara ya Kilimo na Uvuvi, Nishati na Madini, Uchukuzi na Ujenzi, Viwanda na Biashara, Mazingira, Maji, Elimu na Afya. Mpango jumuishi ni muhimu sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu gharama kubwa za upimaji wa ardhi wakati teknolojia imeimarika, kuna haja ya kupunguza gharama ili watu wengi wapime ardhi, kwa hili itasaidia kuifanya ardhi kuwa mtaji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu kukua kwa miji bila ya mpangilio mzuri, hii inaleta bomoa bomoa katika maeneo mengi. Pia kuna haja ya kuongeza kasi ya kupima miji yetu.