Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. James Kinyasi Millya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Simanjiro

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. JAMES K. MILLYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa ufupi naomba nichangie haya yafuatayo:-
(a) Mashamba pori na kutapeli ardhi ya watu ambao hawakuridhia; na
(b) Makazi, ujenzi wa NHC na tatizo la mishahara midogo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mashamba pori na ulaghai kupitia Wenyeviti. Kuna mashamba pori Simanjiro naomba utusaidie kwani wananchi wanateseka na mifugo yao na hivyo kusababisha migogoro kati ya wananchi na mbuga za wanyamapori (National Park). Shamba Namba 24 linasumbua wananchi wa kijiji cha Lobosoit „A‟. Mheshimiwa Waziri anafahamu tatizo hili na tayari maelekezo yale tumeshaanza kuyafanyia kazi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa zaidi ya miaka mingi shamba hili halitumiki na halilimwi na juzi kwenye Kikao Halmashauri ya Wilaya ya Simanjiro Bwana Brown Ole Suya alileta barua ya kubatilisha matumizi ya ardhi kutoka kwenye kilimo na mifugo kwenda mazingira.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ukweli ni kwamba siyo suala la mazingira na wananchi wa kijiji cha Lobosoit “A”, siyo tu hawakumpa mtu huyu hiyo ardhi ya kilimo na mifugo lakini hawapo tayari ardhi yao ihalalishwe ili mtu huyu aiuze ardhi hii kwa wageni (wazungu).
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wenyeviti wa Vijiji Simanjiro ambao sio waaninifu wameuza ardhi ya wanakijiji bila ridhaa yao na hili limepelekea mpaka wao kupata hati miliki. Waliomilikishwa kimakosa wamepewa mpaka hati miliki na Wizara ya Ardhi. Tutasaidikaje ili wale Wenyeviti wa Vijiji ambao sio waaminifu wachukuliwe hatua na wananchi warudishiwe ardhi yao?
Mheshimiwa Mwenyekiti, kijiji cha Laangai, mbali na tamko la mahakama la kuzuia ardhi ya wafugaji isiibiwe na isigeuzwe kuwa eneo la mapambano kama ilivyotokea Kiteto, naomba Wenyeviti na Serikali za Vijiji vya kitapeli zichukuliwe hatua. Iandaliwe orodha ya Wenyeviti wezi wa ardhi ili wachukuliwe hatua.
Mheshimiwa Mwenyekiti, bei ya ardhi inapandisha bei za nyumba; riba za kibenki ni tatizo kubwa la bei ghali za nyumba hizi. La pili, mwanafunzi aliyepata kazi/ajira mwaka huu atapataje nyumba iwapo mshahara wake ni mdogo sana?
Mheshimiwa Mwenyekiti, nchi ya Angola wana mpango mzuri wa kuiwezesha jamii yake kupata makazi bora. Naomba mkajifunze hayo ili wananchi wasaidiwe kupata nyumba bora na nzuri kwa mishahara yao midogo. Hawawezi kukodi nyumba za NHC kwa bei za sasa.