Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Mendard Lutengano Kigola

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. MENDRAD L. KIGOLA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Jimbo la Mufindi Kusini tuna mgogoro wa ardhi kati ya Wizara ya Maliasili na wananchi wa kijiji cha Kitasengwa, Ihomasa, Udumuka na Kilolo, Iyegeya na Mninga. Kufuatana na ongezeko la watu, wananchi wamekosa maeneo ya kujenga nyumba na shughuli za kilimo. Mawaziri waliopita walifika katika vijiji hivi ni Mheshimiwa Maige na Mheshimiwa Ole-Medeye; walifika katika vijiji vya Ihomasa na Kutasengwa. Pia waliahidi kuwa maeneo ambayo yanatumika na wananchi wataachiwa maeneo hayo, lakini mpaka leo hii maeneo haya bado hayajaachiwa wananchi hao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naamini sasa Waziri wangu wa Nyumba na Maendeleo ya Makazi atafika katika Jimbo la Mufindi Kusini na kuwaachia ardhi hiyo ili waweze kuendelea na shughuli za kilimo na kujenga nyumba zao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.