Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Lucy Fidelis Owenya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. LUCY F. OWENYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Kipekee naomba nimshukuru Mwenyezi Mungu kwa kuweza kusimama mbele ya Bunge lako Tukufu na nikiwa kama mdau wa utalii na Mjumbe wa Kamati ya Maliasili na Utalii niweze kuchangia yangu machache. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, utalii unachangia 17.5% kwenye pato la Taifa, lakini tunaweza tukafanya vizuri zaidi kama tutakuwa na mikakati ya kutosha kwanza kwa kuutangaza vya kutosha na pili kuhakikisha kwamba tunagundua utalii mpya. Nimefurahi Mheshimiwa Waziri amesema atatangaza sehemu za utalii Mwanza na kila mahali, lakini naomba nimshauri tu hata hapa Dodoma kuna utalii mzuri tu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama naweza nikashauri kuna mawe mpaka Singida. Dodoma tunaweza tukatangaza utalii wa Stone Mountain kama ilivyo Table Mountain South Africa, watu wanaenda kwenye Table Mountain wanatembelea mashamba ya zabibu. Kwa hiyo, wanaweza wakapita hapa kama destination ya a day tour, wakifika hapa watatembelea hiyo Stone Mountain, watatembelea zabibu, wanaweza wakatembelea Chuo Kikuu na attraction ya Bunge as well. Kwa hiyo, watu wa Dodoma nao wanaweza wakapata mapato kutokana na utalii. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia tunaweza tukawa na watalii throughout the year kuanzia Januari mpaka Disemba lakini ningemwomba Mheshimiwa Waziri wajaribu kuwa na rates za peak season na low season. Kwenye hoteli tayari tuna peak na low season na wakati huu mwezi Machi mpaka wa Julai pia airlines zina low season. Kwa hiyo, ningeshauri Wizara muangalie ni namna gani mnaweza mkapunguza ile park fee ili tuweze kuendana na utalii kama nchi nyingine zinavyofanya; kunakuwa na low season na high season. Kwa hiyo, ningeshauri wafanye hivyo ili tuweze kuongeza watalii zaidi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Tanzania Tourist Board imetengewa 4.1 billion. Kwenye hii 4.1 billion wametoa 1.4 kwa ajili ya mishahara, ina maana wanabaki na 2.6 billion. Mheshimiwa Waziri amesema wataenda kutangaza CNN, BBC na matangazo mengine wataweka kwenye majarida na kadhalika. Hata hivyo, kwenye Hotuba ya Upinzani wamesema mwaka 2013/2014, walifanya maonesho kule Sunderland - UK na wanadaiwa karibu shilingi bilioni tano. Sasa sielewi kama hii 2.6 billion inaenda kulipa deni au lile deni linalipwa na nani? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimepitia vifungu vyote vya randama ya Maliasili na Utalii sijaona hili deni wanalipaje. Mheshimiwa Waziri hebu alete bajeti ambayo ina uhalisia, watakuja kumtumbua hapa, watasema hafanyi kazi lakini pesa hapewi. Kwa hiyo, nafikiri ni vizuri aandikie bajeti yenye uhalisia, aseme madeni ni haya na anahitaji pesa kiasi hiki. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nizungumzie kidogo Mlima Kilimanjaro. National Parks zimeingiza shilingi bilioni 185, out of shilingi 185, Kilimanjaro National Park imeingiza shilingi bilioni 60, hizi ni fedha nyingi sana. Najua KINAPA wanajaribu kujenga madarasa na kadhalika lakini bado Halmashauri zinazouzunguka Mlima Kilimanjaro hazifaidiki na mapato yanayotokana na Mlima Kilimanjaro. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama ilivyo kwenye migodi wanapata 0.3% ya pesa zinazotokana na mgodi, kwa nini isifanyike hivyo kwa Kilimanjaro? Shilingi bilioni 60 ukitoa 0.3% ni hela nyingi sana ambazo zingepewa Halmashauri wakaweza kufanya maendeleo yao wenyewe, wakatengeneza zahanati na madarasa. Mheshimiwa Waziri hata Mwanga ipo katika hizi Halmashauri ambazo zinafaidika na mapato ya Mlima Kilimanjaro, kwa hiyo, nategemea atalichukulia hili on a serious note. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini Mlima Kilimanjaro ni lazima Wizara ishirikiane na Wizara ya Mazingira, Mlima Kilimanjaro unaharibika. Wamejaribu kukusanya takataka kutoka Mlima Kilimanjaro lakini bado hazijakwisha. Kwa sababu wataalam wako hapa kule Mti Mkubwa kupitia Lemosho na kule Barafu, vyoo viko vitatu na vya shimo ambapo ma-porter, ma-guide na wageni, zaidi ya watu 300 wanatumia vyoo hivyo. Tumekuwa tukiongea hapa ndani ya Bunge hili kuna vyoo ambavyo vilitoka Ujerumani kwa ajili ya majaribio sijui mpaka sasa hivi vyoo vile vimeishia wapi? Naomba Mheshimiwa Waziri wakati anakuja kujumuisha atueleze vile vyoo mpaka sasa hivi vimeishia wapi? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo hilo linaenda sambamba na maji. Barafu, Mweka na Millenium Towers, hakuna maji. Kwa nini sasa KINAPA wasichukue maji kutoka Karanga waka-pump yakaja pale juu ili watalii waweze kuyatumia badala ya sasa hivi wanaenda kuzoa maji mbali na kuyaleta pale. Sasa hivi kule crater watu wana camp crater lakini Mheshimiwa Waziri crater hamna choo, watu wanalala kule halafu ndiyo wanapanda juu.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuna watalii wanakuja zaidi ya mara 10 wanakuta mambo ni yaleyale business as usual. Kwa hiyo, naomba waangalie ni jinsi gani wataweza kutengeneza kule crater kuwe pasafi, ni pachafu sana.
Kwa hiyo, waangalie ni jinsi gani wataweza kutengeneza kule juu ili hawa tour leaders wanaorudi waweze kutuletea watalii kwa wingi zaidi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nizungumzie Southern Circuit. Southern Circuit tunashindwa kuiuza kwa sababu miundombinu si mizuri. Tumekuwa tukizungumza mara nyingi, sasa Wizara hii na Wizara ya Miundombinu iangalie ni jinsi gani inaweza kutengeneza miundombinu ya kwenda Southern Circuit. Wawekezaji wanakuja wanataka wakajenge hoteli lakini wageni watafikaje huko, hoteli ni ghali sana. Kuna ndege moja inayoenda huko inaitwa Coastal Air lakini price yake ni sawa na mtu anayetoka hapa kwenda Europe. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wazungu wengi wanaokuja Tanzania wana-save for years. Unakuta mtu ame-save almost five, six years ili aweze kuja Tanzania. Tukumbuke wageni wengi wanakuja kwa credit card, akifika hapa anajaribu kuangalia ni kwa jinsi gani anaweza ku-save aizungukie Tanzania yetu ilivyo nzuri lakini unakuta mara nyingi wanaishia kwenye Nothern Circuit kwa sababu ni cheaper, kuna hoteli nyingi lakini wanashindwa kwenda Southern Circuit kwa sababu ni too expensive.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, naomba Serikali muangalie ni kwa jinsi gani mnaweza kushirikiana na Wizara ya Miundombinu ili muweze kutengeneza hizo barabara ili wawekezaji waweze kuja kujenga hoteli kule na tuweze kuiuza kama tunavyoiuza Nothern Circuit. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nizungumzie kidogo huyu mjusi aliyeko huko Ujerumani. Kambi ya Upinzani imezungumza vizuri sana, ni fedha nyingi zinazopatikana kule Ujerumani. Euro 25 kwa watu 550 unaongelea karibu shilingi bilioni nne, sasa hivi sisi hatuhitaji hizo shilingi bilioni nne kweli?
Mheshimiwa mwenyekiti, ni kwa nini sasa msifanye arrangement aidha na sisi tupate percent yetu kama ikishindikana msafirisheni basi yule mjusi. Akiwekwa kwenye meli akawekwa pale Dar-es-Salaam ina maana watalii watakuja Dar-es-Salaam badala ya kwenda Ujerumani na sisi tutafaidika. Kuna vipesa vidogovidogo tunahangaikanavyo kwa ajili ya zahanati na kadhalika si vitapatikana pale! (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nategemea sasa Mheshimiwa Waziri anavyokuja kutujibu atatueleza ana mkakati gani wa kuhakikisha kwamba yule dinosaur wanamsafirisha aje hapa. Katika Bunge hili yule mama wa Lindi mpaka tukamuita mama mjusi humu ndani, alikuwa anamzungumzia kweli lakini hakuna kilichofanyika mpaka leo. Ni mategemeo yangu sasa kwa wakati huu Mheshimiwa Waziri atakuja na majibu atueleze ana mikakati gani ya kuhakikisha mjusi yule anarudi Tanzania.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kinachonisikitisha, mpaka sasa hivi hatuna Bodi ya TANAPA. Naomba Waziri anapokuja kujumuisha hapa hebu atueleze ni kitu gani au ni kwa nini wanashindwa kuunda Bodi ya TANAPA? Vitu vingi sana haviendi, tunalalamika hapa bila Bodi hawawezi kwenda kufanya chochote. Kwa hiyo, Mheshimiwa Waziri aje atueleze ni lini ataunda Bodi ya TANAPA…
(MWENYEKITI: Ahsante.