Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Mendard Lutengano Kigola

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. MENDRAD L. KIGOLA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa kupata nafasi hii ya kuchangia na mimi katika hoja hii muhimu sana. Mimi leo sehemu kubwa itakuwa ni ushauri kwa sababu Waziri anayeanza sasa hivi ni mara ya kwanza kushika nafasi hii ya Wizara ya Maliasili. Ila nataka niseme tu, Wizara ya Maliasili ni Wizara ngumu sana kwa sababu inagusa maeneo mengi sana ambayo yanahusu maslahi ya watu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nianza na masuala ya migogoro ya wananchi na Hifadhi. Kila kona Tanzania nzima kuna hifadhi ya misitu, na kule kwangu Mufindi kuna vijiji ambavyo viko ndani ya msitu lakini nataka niseme kwamba vile vijiji vilianza miaka mingi sana, miaka ya 1974, 1976, kwa hiyo misitu umekuta vijiji, kwa sababu ile misitu imepandwa mwaka wa 1977. Sasa namuomba Waziri, kuna vijiji vile ambavyo Mawaziri waliopita waliweza kutembelea vile vijiji na waliahidi kwamba wataachiwa na waliunda Tume, Tume ikafanya mchakato kule, na bahati nzuri sana wakasema kwa sababu siku hizi ni ushirikishwaji pamoja na wananchi, basi yale maeneo watawaachia wananchi waendelee kufuga na kulima.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nakuomba kuna kijiji cha Kitasengwa pale, Kitasengwa ni kijiji ambacho kinapakana na msitu pale na wananchi waliacha maeneo makubwa kuwaachia Wizara ya Misitu wakabakiwa na maeneo madogo na yale maeneo madogo Wizara ya Misitu inataka kuwanyang‟anya. Nakuomba Waziri yale maeneo madogo wawaachiwe wananchi wa Kitasengwa pale, na watu wa misitu wanaelewa na barua tulishaandika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili kuna kijiji cha Ihomasa, Mheshimiwa Waziri Ezekiel Maige alienda, hata kipindi cha Mheshimiwa Balozi Kagasheki alienda pale, na waliahidi kabisa kwamba yale maeneo wanayaachia wananchi. Lakini mpaka leo hawajayaachia wananchi wale, nakuomba Waziri, mimi Waziri Maghembe nakuamini sana. Kwa sababu na tume imeishaundwa noamba wananchi wa Ihomasa, wapewe lile eneo dogo waendelee kuishi; kwa sababu wanashindwa kulima na tunasababisha njaa. Kuna kijiji kingine kiko pale Kilolo ambacho kinaunganika na Udumuka, na wenyewe wana tatizo linalolingana na Kijiji cha Kitasengwa. Ni maneo ambayo wananchi wanapata chakula pale.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba na wenyewe waweze kuachiwa maeneo hayo. Kuna hifadhi nyingine iko kwenye Kijiji cha Iyegeya, Iyegeya ni kijiji kiko Luhunga pale. Kile kijiji kuna hifadhi kubwa sana imebaki tu, hakuna wanyama wala nini, wanaita hifadhi, sasa mimi huwa nashindwa kuelewa hifadhi inahifadhi nini kwa sababu pale hakuna msitu. Ni eneo pori tu wanasema hifadhi, wananchi hawana sehemu ya kulima wala kufanya nini, naomba wawaachie wananchi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, bahati nzuri Mawaziri wote waliopita walishafika kule na wakaahidi kwamba wataachiwa, naomba na wewe basi umalizie ufanye mkutano na wale watu. Kwanza mikutano tulishafanya sana, ni kutoa amri tu, siku moja waendelee unakaa ofisini unaagiza Wizara yako, basi wananchi wanaweza kuachiwa maeneo yale.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la mwisho ambalo ningependa sana kuchangia ni kuhusu Jimbo la Mufindi Kusini ambapo wananchi walio wengi walihama kuachia maeneo Wizara ya Misitu. Na walifanya vizuri siwezi kusema walifananya vibaya, kwa sababu ule msitu sasa hivi ni Pato kubwa sana la Taifa. Na hatuwezi kusema Serikali inafanya biashara hapana, Serikali inatoa misaada, inatoa service kwa wananchi, na wananchi wale lazima wanufaike na misitu. Sasa cha ajabu inakuwa kinyume chake kwa nini? Tunashindwa kuelewa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nitoe mfano mdogo tu, kijiji cha Nyololo ni kijiji kikubwa sana, kijiji cha Igowole ni kijiji kikubwa sana, ukienda Igowole mpaka kule Sawala, mpaka kule Kibawa, mpaka Mninga vijjiji vyote hivi vilikuwa ndani msitu. Na waliachia Wizara kwamba wapande misitu, ili Taifa letu liweze kupata faida. Lakini cha ajabu sasa hivi vile vijiji vinavyozunguka ndani ya msitu havipati faida, kuna vitu vingine ni vidogo vidogo tu mimi nashangaa sana Wizara haifanyi kazi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hivi tunategemea kwa mfano Mji ule Nyololo pale ukiangalia ng‟ambo ya huku juu ni msitu mkubwa karibu kilometa 40, tumeachia Wizara, kijiji cha Nyololo hakina hata maji. Maji ambayo hata shilingi milioni 20 haiwezi ku-cost, kwa nini Wizara inashindwa kusaidia huduma za kijamii? Tunasema wawekezaji wasaidie huduma za kijamii kwenye vijiji vinavyohusika, lakini kijiji cha Nyololo hakina maji hakina barabara. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, hata barabara tu Wizara ya Misitu mna magreda pale, magreda tukienda pale mpaka uandike barua uomboleze ufanye nini, na wale watu ndio wanaolinda msitu. Watu watapataje moyo wa kulinda msitu wakati hawana hata barabara, hata maji tu mnashindwa. Mimi Mheshimiwa Waziri Maghembe namuamini sana, naomba vijiji vinavyozunguka misitu lazima vipate huduma za kijamii. Na tunaposema huduma za kijamii ni zipi, nataka nikuambie Mheshimiwa Mwenyekiti, ukifanya huduma ya maji, ukisaidia kujenga zahanati, ukasaidia kujenga kituo cha afya, wewe utakuwa umesaidia huduma za kijamii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa Wizara utasikia tunatoa mafunzo jinsi ya utunzaji wa misitu na kulinda moto. Hivi wewe unalinda moto wakati una afya mbaya na kituo cha afya hakijajengwa na kiko ndani ya msitu? Mheshimiwa Waziri mimi nakuomba sana, kwa mfano ukienda pale Mninga tuna kituo cha afya pale, kituo kile kimejengwa miaka mitano, mpaka sasa hivi hakijaisha. Unaenda pale utasikia Wizara ya Misitu eti wametoa labda mbao 100, mbao 200, kwa nini usitoe msitu tu useme umemaliza kituo cha afya tumemaliza kila kitu?
Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi Mbunge nilienda pale nikatoa bati 200, mifuko ya simenti 100, Wizara inatoa mbao 20 au 10 hiyo haiwezi kukubalika kabisa hiyo. Mheshimiwa Waziri nataka nikuambie kitu kimoja, mwaka huu lazima tuone Wizara ya Misitu inatoa vitu vya kijamii vinaonekana. Kwa mfano, hapa nilikuwa nasoma hapa, mmesema mnategemea kukusanya shilingi bilioni sita, mwaka wa jana walikusanya shilingi bilioni nne, shilingi bilioni nne sisi wana Mufindi hatujafaidi. Sisi suala la madawati lilitakiwa liwe historia tu, hapa tunaanza kuongelea madawati sisi watu wa Mufindi! (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkuu wa Mkoa juzi alisema anatuita Wabunge tuanze kuchangisha madawati, hatuchangii. Misitu ipo pale tuanze kuchangia kwa nini, lazima misitu ile ifanye kazi pale, hatuwezi kuwa tunasimamia kulinda misitu; halafu mnatubanabana sisi Wabunge na fedha ndogo ndogo hizi, wakati kuna shilingi bilioni sita iko hapa hiyo haiwezi kukubalika kabisa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunataka madawati pale yakamilike. Mwaka jana mimi niliomba nikasema katika shilingi bilioni nne, mtupatie hata shilingi bilioni moja tu Wilaya ya Mufindi tutakuwa tumemaliza madawati, matokeo yake wanaenda kutoa madawati 100. Hatuwezi kudanganywa kama watoto wadogo, tutalindaje misitu? Haya umesema hapa kuna masuala ya mradi wa nyuki. Nilisikia siku moja kuna kikundi fulani kimechonga mizinga, badala ya kuwagawia wananchi wanaoishi kwenye misitu kule, wakaanza kufanya biashara wakasema kila mzinga shilingi 60,000 sasa tena ni biashara imetoka wapi? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nikajua mnawahamasisha ili wafuge nyuki, sasa utapeli tapeli huu unatoka wapi huu, hii inakuwa ni tatizo hatuwezi kuwa tuna matatizo tunayaona hivi na mwaka huu sisi tuko smart. Nadhani Wabunge wanaotoka Wilaya ya Mufindi watakuwa wakali sana kwa hili, hatuwezi tukawa tunahaibika na vitu vidogo vidogo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, haya tunakuja kwenye ugawaji wa vibali. Ugawaji wa vibali unaenda kitapeli tapeli, mtu anafanya kama biashara ya kwake. Ile ni mali ya Serikali, ya wananchi wote, utakuta mtu mmoja anagawagawa vibali anagawa kwa wananchi anafanya biashara, kwa nini asishikwe apelekwe polisi ahukumiwe, mnamuangalia tu. Matokeo yake sisi Wabunge tunapata makashfa makubwa, sisi hatulali kule, mtu mwingine anakaa Dar es Salaam kule, amekusanya vibali analala usingizi, sisi kule tunalala tunalinda moto kule, mwenyewe anakuja kutapeli kule, hii haiwezi kukubalika hata siku moja. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri bajeti yake itapita, na kwa sababu ya mara ya kwanza tunamsamehe kwa leo, lakini ninayoyaongea haya, next time nikiona yametokea sitakubaliana kabisa. Watu wanaleta ujanja ujanja wa vibali, tumesema vibali mpeleke kwenye vijiji, vijiji vile ukisaidia Kijiji kimoja kibali kimoja tu wakajenga zahanati, kijiji kimoja utakuwa umesaidia watu zaidi ya 70, au zaidi hata 1000. Kijiji cha Mninga kiko ndani ya msitu hata zahanati miaka mitano hatujamaliza, kwa nini usiwape kibali pale?
Mheshimiwa Mwenyekiti, jamani vitu vingine ni vitu rahisi rahisi tu, Serikali tutaanza kuilaumu kwa vitu vidogo sana. Hatuwezi kulaumu kwa vitu vidogo vya utekelezaji. Kwa kweli hii inaleta uchungu sana, kuna vitu vingine ni vitu vidogo vidogo lakini kwa ajili ya watu wachache wanatuletea gharama kubwa ya kuweza kuhutubia kila siku. Mwaka jana nakumbuka Waziri Mkuu alitutuma mimi na Waziri Nyalandu tukaenda Mufindi kule, Waziri Nyalandu alienda pale akafanya mkutano mzuri kwa wananchi, wananchi wakampigia makofi, kwenye utendaji ikawa zero kwa nini? Haiwezekani kabisa hii ndugu yangu, haiwezekani.