Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Riziki Saidi Lulida

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. RIZIKI S. LULIDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nikushukuru na mimi kupata nafasi hii ya kuchangia katika Wizara ya Maliasili na Utalii. Mimi ni-declare interest kwamba ni mdau wa maliasili. Kwanza nimezaliwa Selous, lakini ya pili ni Mwenyekiti wa Kupambana na Ujangili, say no to poaching. Bahati nzuri Kamati yangu tulizunguka Tanzania nzima, tukaona mazingira ambayo tumeyaona lakini nataka na mimi nitoe kama ushauri kama utaweza kusikilizwa, lakini tuangalie suala la uhifadhi na environment ya Tanzania.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nilipata bahati kuhudhuria mikutano mbalimbali ya climate change. Tanzania sasa hivi tunakwenda kwenye gold, tumetoka katika green tunakwenda kwenye gold, maana yake Tanzania inakwenda kwenye jangwa. Sasa tujiulize tunaangalia maslahi ya nchi au tunaangalia maslahi binafsi ya kwamba mimi niwe Mbunge, ili fujo ya nchi kuingia katika disaster ya kuwa katika gold na hali ya nchi kuwa katika ukame. Wabunge sisi tujiulize na tujipe nafasi ninachokizungumza nchi yangu inakwenda wapi? Tunakwenda katika jangwa! Tulikuwa na Profesa mmoja akatuambia mnaiona Tanzania? Tanzania inakwenda katika jangwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, leo nchi za Uarabuni wanapanda miti na kuhakikisha wanautoa udongo India, kuhakikisha Arabuni kama Dubai inakuwa katika green na mvua wanapata sasa hivi. Lakini Tanzania mito mingi mikubwa sasa hivi inakauka na inapotea kabisa. Nataka nimshukuru na niwapongeze watu wa Ngorongoro, niwapongeze watu wa TANAPA na Wamasai waliopo ndani ya Ngorongoro, wale ni wahifadhi wazuri na wanasimamia ndiyo maana mpaka leo Ngorongoro Conservation inaonekana kama Ngorongoro Conservation. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, inaonekana TANAPA na uhifadhi wake, na kutoa tozo kubwa kwa ajili ya Serikali mwaka huu wametoa shilingi bilioni 10. Niko katika kamati ya uwekezaji, mashirika ambayo yameweza kujitegemea ni Ngorongoro, TANAPA, National Housing na TRA basi, mashirika mengine yote yako katika hali ya kufa. Sasa tujiulize tunataka uhifadhi au tunataka tuhakikishe uhifadhi hamna, mvua hamna tutaishije Tanzania hii? Hata mito haitakuwepo. Leo wewe ni mfugaji unaingia ndani ya Pori la Serengeti kuna simba, kuna tembo mgongoni una bunduki, nipe tafsiri yake ni nini hapo? Sielewi kabisa hiyo picha inayoniambia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, halafu pili tuhakikishe haya mapori ni michoro ambayo ilikuwepo tangu enzi ya mkoloni, walijua tuwaweke maeneo ya uhifadhi hawa Waafrika watamaliza misitu yote watahakikisha hifadhi hakuna hata mvua itakuwa haipatikani. Na ndiyo maana kuna demarcation kuna, kuna ma-beacon ambayo yameweka mle ndani kuhakikisha hizi alama zinaendelea kudumu lakini kwa uhifadhi waliamua kuhakikisha wamewagawia, mwisho tunajiuliza je, tugawe hifadhi zote watu wachukue wamalize wafugaji halafu hii nchi ikae katika ukame? (Makofi)
Nataka nitoe tafsiri ya hili, wafugaji walipelekwa Mkoa wa Lindi walitoka Ihefu, Ihefu ilikauka kabisa TANESCO hata mvua ilikuwa hamna, maji hamna nchi ikaingia katika giza. Lile giza limepelekwa Lindi, shamba la bibi Lindi nenda leo Selous hakuna simba, nenda leo Selous hakuna ndovu wamehakikisha wafugaji wameingia mpaka ndani ya Selous.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa tujiulize tunaangalia maslahi ya nchi au tunaangalia mimi nichaguliwe kuwa Mbunge halafu baadaye niendelee kuwa Mbunge nchi iingie katika disaster haikubaliki. Ninakuomba Waziri mwenye dhamana toa semina Wabunge wajitambua kama uhifadhi ni kitu kizuri ndani ya nchi hii. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi mwaka 2008 nilikuwa Mjumbe wa Kamati ya Maliasili Mwenyekiti wangu alikuwa Job Ndugai. Ni wewe ndiwe uliyeanzisha CNN, ndipo Tanzania ikaanza kukua katika utalii. Ni wewe ndiye ulileta fixed rate watu wakaambiwa ni lazima watu wenye mahoteli walipe baada ya kuona wewe unataka kuupaisha uchumi na wao kazi yao ni kuuhujumu uchumi walikuondoa kwa kuhakikisha uchumi ulio ndani ya maliasili unaporomoka. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakuombea kwa Mwenyezi Mungu akulinde, akupe afya njema uiongoze nchi kama anavyoiongoza Waziri wa Ardhi na wewe nataka nikupe fimbo hiyo ufanye kazi hiyo, kazi kwa kwenda mbele. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nimezaliwa Selous, nimezaliwa Selous mimi ni Mngindo kwa asili ninatoka ndani ya Liwale. Selous ndiyo mbuga kubwa ya kwanza katika Afrika na ninaweza kusema ni duniani haijatangazwa, kuna corridor kubwa ya tembo ambao wanatoka Mozambique wanakuja Tanzania wakiingia Tanzania wanaingia Namtumbo, wanaingia Masasi, wanaingia Nachingwea, wanaingia Liwale, wanaingia Kilwa wanakwenda mpaka Mahenge wanavuka wanakwenda mpaka Tarangire. (Makofi)
Sasa ushoroba huu wanafaidika nini na watu wa Kusini? Ninaomba madawati yaliyopangwa ya TANAPA yawapeleke watu wa Lindi, Mtwara na Ruvuma wafaidike nayo. Huyu sungura asigawiwe kwa upande mmoja, hii siyo haki. Tulidai haki ya gesi mkasema gesi ni ya Watanzania kwa nini madawati mnagawa kwa mafungu? Nataka nihakikishiwe, Mheshimiwa Waziri pamoja na kukupenda sana kama haujapeleka allocation Lindi sitakubaliana, kama hujapeleka allocation Ruvuma sijakubaliana na wewe na kama hujapeleka allocation Mtwara kwa kweli sikubaliani nawe na ninaomba sheria hii irudishwe hapa tuifute ili angalau Tanzania nzima wafaidike. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkoa wa Lindi unaongoza kuwa na rasilimali kubwa, tumepiga kelele ya mjusi ambaye yuko Ujerumani kila mwaka wanapata dola bilioni tatu Tanzania hata senti tano hatuipati. Hapa wanatufanyia dhihaka mjusi, mjusi, lakini ni haki ya mjusi. Maeneo yale tupate shule, tupate barabara lakini mpaka leo watu wa Ujerumani wanafaidika na yule mjusi, sisi tunapata nini? Nataka Mheshimiwa Waziri wa dhamana aniambie tozo linalopatikana kutokana na yule mjusi linakwenda Mipingo Tendeguru, sisi tusibakie kama boga linasuka mikeka wenye tunalala chini, hatukubali kwa hilo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Kilwa iko katika urithi wa dunia na katika urithi wa dunia Kilwa ni namba 21 duniani hata hizo Ngorongoro, TANAPA ziko nyuma lakini kwa vile iko Kusini mpaka leo imeachwa katika urithi wa dunia. Hautuzwi, hakuna mapato, hakuna kinachoangaliwa kule Kilwa zaidi ya tumepaacha hakuna ndege zinazokwenda kule, watu wanakwenda kinyemela nyemela hakuna mapato yanayopatikana. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nizungumzie suala la utalii. Mtalii akija Tanzania anakuja na package, anaingia TANAPA, anaingia Ngorongoro, anakwenda Zanzibar. Masikitiko yangu makubwa Zanzibar hakieleweki hela zinakwenda wapi? Imefikia mahali kuwa tozo zinazopatikana Zanzibar ni hela za watu wajanja, inafikia kujiuliza Zanzibar kuna nini? Utalii wa Sychelles umewafanya mkawa matajiri, Zanzibar watu wanaendela kuwa maskini kwa vile hawasimamii rasilimali yao. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama Zanzibar wameshindwa kusimamia utalii tupo tayari kusimamia utalii wa Zanzibar na utaruka. Kama huku TANAPA wanaweza kukusanya shilingi bilioni 100, Ngorongoro shilingi bilioni mia moja na Zanzibar iko wapi hela ya utalii aibu kubwa sana. Ifike mahali ujiulize kuna fanyika nini mpaka Zanzibar ikaonekana hata utalii wa maana, pesa inayongia kama concession fee Zanzibar hakuna? Kule kuna ujanja na ulaji ambao hauna mwenyewe na kazi yao kutoa vitenge, wakiwapa vitenge wamemalizika tuuangalie utalii wa Zanzibar kwa jicho la huruma watu hawa waweze kusaidiwa.
Na wampe Maalim Self afanye kazi