Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Selemani Moshi Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninashukuru sana kwa kunipa nafasi hii nianze mchango wangu kwa kuchangia juu ya Hifadhi ya Taifa ya Katavi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hifadhi hii ipo Mkoa wa Katavi, ni hifadhi kubwa sana, lakini bahati mbaya sana Wizara husika haijaitangaza. Ili tuweze kutangaza utalii ni vema tukaelekeza mawazo kwa maeneo yote ya nchi yetu. Ukanda wa Kusini utalii haujatangazwa ndiyo maana Mbuga ya Ruaha, Mbuga ya Katavi, Mahale hazifanyikazi vizuri kwa sababu Serikali yenyewe imeweka mipaka; utalii unaotangazwa katika nchi yetu zaidi unatangazwa kwa Mikoa ya Kanda ya Kaskazini. Ninaiomba Serikali ielekeze nguvu kutangaza na maeneo mengine ili zile fursa wapate kuzitembelea, tuna imani watalii watakuwa wengi pindi watakapokuwa wamebadilisha na maeneo mengine wakaenda kuangalia fursa zilizopo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninazungumzia suala la Hifadhi ya Katavi kwa sababu Mbuga ya Katavi inayo uwezo wa kuunganisha watalii wa kutoka Katavi na wakaenda Mbunga ya Mahale ambayo iko Mkoa wa Kigoma ambao ni jirani, wanaweza wakitoka Mkoa wa Iringa katika Hifadhi ya Ruaha wakaja Mbuga ya Katavi na baadaye watalii hao wakaenda Mahale, wanaweza wakapata maeneo mengi ya kuangalia utalii wa nchi yetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye Mbuga ile ya Katavi tunaiomba Serikali iangalie uhifadhi wa hifadhi hiyo ya Katavi kwa sababu upo uwezekano hifadhi hii ikatoweka kwa sababu hakuna miundombinu mizuri. Ninaishauri Serikali tunao Mto wa Katuma ambao unaifanya Hifadhi ya Katavi iwepo, itunze na ihakikishe inaandaa mazingira mazuri ya kuhifadhi ili kuwe na utaratibu wa kuvuna maji, kuna maeneo wakati fulani inapofika kipindi cha mwezi wa Oktoba hifadhi hii huwa inakauka, hakuna maji na wanyama kama boko na mamba huwa wanakufa kwa wingi sana. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na hilo kwenye hifadhi ya wanyama ya Katavi, bado wafanyakazi wanaofanyakazi kwenye hifadhi hii wanashida kubwa sana ikiwa ni pamoja na vitendea kazi hawana, ninaiomba Serikali kupitia Wizara husika iwapelekee vitendea kazi ili waweze kupambana na majangili wanaoenda kwenye mbuga hii sambamba na hifadhi ya Msitu wa Luwavi ambao ni jirani na kwa Mheshimiwa Keissy. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumzie suala la migogoro kati ya vijiji ambavyo vinazungukwa na WMA. Kumekuwa na tatizo kubwa sana kati ya vijiji vya Kabage, Kungwi, Sibwesa, Kasekese, Kaseganyama na Kapalamsenga. Vijiji hivi kila mara wananchi wanasumbuliwa wanachomewa nyumba na Serikali kwa sababu wao wana migogoro na WMA.
Mheshimiwa Mwenyekiti, WMA ni ardhi ambayo wanavijiji walikubaliana, lakini bado wananchi hakuna walichonufaika na mpango mzima wa WMA. Ninaiomba Serikali, Mheshimiwa Waziri, fanya ziara Mkoa wa Katavi utembelee kwenye vijiji hivyo, uje utatue tatizo la WMA ambayo inawalazimisha wananchi hawana faida nayo, ukitatua huu mgogoro utakuwa umesaidia sana wananchi kwenye maeneo hayo. Ni vizuri tukaangalia pande zote mbili, mimi naamini uhifadhi tunauhitaji sana kwa sababu unalinda mazingira na unawafanya wananchi waneemeke na fursa zilizoko. Yale maeneo ambayo yamekuwa na migogoro ni vizuri Serikali mkawa karibu ili mkawatendea haki wale wananchi, tutoe dhana ile ambayo ipo ya kila siku kusikiliza hii migogoro.
Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo lingine ambalo ninapenda kuzungumzia ni hifadhi ya misitu. Mkoa wangu wa Katavi una hifadhi mkubwa sana ya misitu na tuna eneo la Hifadhi la Msitu wa Tongwe, ambapo kumekuwa na uvunaji holela wa magogo yanayochukuliwa na wasimamizi wakubwa sana ni TFS ambao wanasimamia misitu kwenye nchi yetu kwa ujumla. Ninaiomba Serikali tunahitaji sasa maeneo ambayo kunavunwa hiyo misitu, kuwe na kitu ambacho kinawanufaisha wananchi kwenye maeneo husika, vipo vijiji ambavyo vimepakana na hiyo misitu, wanatunza lakini hawanufaiki, unafika mahala hata watoto wanaosoma kwenye shule, hawapati madawati kwenye maeneo hayo. Ni vema Serikali ikaja na mpango wa kuangalia maeneo ambayo yanawanufaisha wananchi na wanatunza ile misitu kuwe na mrejesho ambao utawafanya wawe na nguvu ya kuhifadhi hiyo misitu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwa nazungumzia sana eneo lingine wakati ule wa Operesheni Tokomeza. Wananchi hasa wakulima walinyang‟anywa silaha ambazo zinawasaidia kufukuza wanyama waharibifu. Serikali ije na majibu kwa sababu wananchi hawa wanaolima, wanyama waharibifu wanakwenda kuharibu mazao yao na silaha zote walishazibeba. Tunaomba Serikali iwarudishie wananchi hawa....
MWENYEKITI: Ahsante.