Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali katika Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Wilfred Muganyizi Lwakatare

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Bukoba Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali katika Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. WIFRED M. LWAKATARE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Unapozungumzia suala la reli ya kati, reli ya kati kwa Kagera haiishii Mwanza. Reli ya kati inaishia katika bandari ya Kemondo ambapo siku za nyuma wakati bado reli inafanya kazi vizuri reli ya kati, tulikuwa na meli ambayo ilikuwa inapakia mabehewa na kuna njia ya reli ambayo inaishia bandari ya Kemondo. Tunapozungumzia reli wananchi wa Kagera, Mheshimiwa Lugola amezungumzia kwa upande wake namna gani ambavyo bidhaa zinavyosafirishwa kwa njia ya barabara zinavyokuwa na bei kubwa zinapofika katika eneo lake. Sasa nazungumza kwake ni tisa, kumi ni Kagera, sisi ndiyo tuliopo pembezoni mwa nchi hii. Cement ni shilingi elfu ishirini na mbili kufikishwa pale Bukoba Mjini na bei hii naamini ni kwa sababu bidhaa ya cement na bidhaa nyinginezo zinasafirishwa kwa njia ya barabara.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo kwetu sisi kukosekana kwa reli ya kati kwa wananchi wa Kagera na hususani Bukoba mjini, ni kwamba mipango hii inayopangwa bila kuzingatia kuweka reli, wananchi wa Kagera mnataka waendelee kuwa maskini. Na mimi niseme hivi, umaskini huu unakwenda mpaka kusababisha bei ya kahawa kushuka, kipindi cha nyuma kahawa ilikuwa inasafirishwa kwa reli, yale mabehewa yalikuwa yanayokwenda mpaka Bukoba kupeleka bidhaa pale Kemondo, yanarejesha bidhaa ya kahawa mpaka kwenye bandari zetu tayari kusafirishwa kwenda nchi za nje, kwenye masoko.Usafiri wa barabara wa kusafirisha kahawa umechangia pamoja na sababu nyingine umechangia kushusha bei ya kahawa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo niombe, tunapopanga mipango hii Waheshimiwa, tujitahidi kuangalia kina na kiini cha ni namna gani watu mipango mnayoipanga inashindwa kuwaondoa ndani ya umaskini. Niseme kwa wananchi wa Kagera na Bukoba in particular, tukumbushane hata ahadi zinazofanyika mziweke katika mipango na zitekelezeke.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Mkapa katuahidi meli baada ya Mv. Bukoba kuzama; Mheshimiwa Kikwete katuahidi meli, Mheshimiwa Magufuli naye wakati akiomba kura ameahidi meli. Sasa huko mbele tunapokwenda leteni mipango kanyaboya, leteni mipango ambayo haioneshi ahadi zilizopita.
MHE. SULEIMAN M. NCHAMBI: Taarifa!..
MHE. WIFRED M. LWAKATARE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, ili roho yake ipone pamoja na kwamba na yeye amemwita Magufuli basi Rais Magufuli, furahi basi. (Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni hivi, nilikuwa nazungumzia suala la ahadi, tuliahidiwa meli, meli haijaja. Sasa katika uchunguzi wangu tatizo linalotupata katika mipango inayopangwa na Serikali, suala la kutoleta sheria inayopaswa kwenda sambamba na mipango inayoletwa. Matokeo yake hakuna nidhamu ya utekelezaji wa mipango hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia hata ndani ya Bunge hili, kulikuwa na utaratibu wa kuunda Kamati ya Governance Assurance Commitee, Kamati ya Ahadi za Serikali, hii Kamati naamini ingeweza kusaidia katika suala la kuishinikiza na kuisimamia Serikali kwa ahadi zinazotolewa Ndani ya Bunge hili. Matokeo yake hakuna Kamati hizi. Kwa hiyo, mipango inayopangwa na naamini hata hii mipango inayopangwa, kwa kuwa hatuna sheria, hatuna Kamati inayosimamia hii mipango, huenda hizi ahadi na mipango ikawa hewa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa sheria hizi hazipo na mimi hapa ndiyo maana namuunga mkono Mheshimiwa Warioba katika Katiba ya Warioba ambayo ilikuwa inahitaji Mawaziri wasiwe Wabunge. Kwa sababu tatizo la nchi hii kutokana na kwamba hatusimamiwi na sheria, kila mmoja anayepata nafasi ya kuwa Rais, kuwa Waziri Mkuu, kuwa Waziri, wote wanaanza kukimbilia kuangalia kwao kunahitajika nini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, siyo ajabu tukaanza kusikia hata mipango mingine zaidi ya Bagamoyo, zaidi ya viwanja vya ndege, zaidi ya kupeleka mabomba ni kwa sababu watu hawasimamiwi, watu mipango inapangwa kufuatana na nani yuko wapi na ana-influence gani na Hazina. That is the problem! Kwa hiyo, niombe sambamba na mipango hii sheria itungwe lakini ile Governance Assurance Committee ifanye kazi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati nipo Chuo Kikuu Walimu wangu akiwemo Profesa Baregu, Profesa Mutahaba, Marehemu Profesa Liviga waliwahi kuniambia na kunifundisha kwamba mahala ambapo hakuna good governance hakuna true democracy. Mipango yoyote haiwezi kuenda. Mheshimiwa Mpango naamini na wewe ni msomi unaamini kabisa, najua unaamini kwamba mipango yote unayoipanga kama itakuwa na sokomoko la kutuingiza tena katika mgogoro wa miaka yote mitano kuingia sakata lililokuwepo mwaka 2000 mpaka 2005 kule Zanzibar hakuna mipango itakayofanyika. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, niseme ndugu zangu sikio lililokufa halisikii dawa. Hawa CCM, kwanza niwashukuru wananchi wa Bukoba Manispaa, waliuthibitishia ulimwengu na Taifa hili na wakathibitishia wengine waliosema wana ushahidi ndani ya dunia hii na mbinguni kwamba Lwakatare ni gaidi. Malipo ya wananchi wa Bukoba waliyoyatoa ni kuhakikisha Lwakatare anashinda kwa kishindo na anakabidhiwa Halmashauri kuja Bungeni hapa. (Makofi)
Sasa niwaambie Makamanda hizi nyimbo, miongozo, taarifa mnaopigwa iwape nguvu ya kukanyaga mafuta ndani ya Bunge. Nilipokuwa likizo nje ya Bunge nilikuwa naona mlikuwa mnaanzia hapo mpaka hapa. Leo tumewasukuma, tumekwenda mpaka pale nawahakikishia Bunge linalokuja mtasogea hivi na wengine watapita njia hii. (Makofi)
Makamanda nilikuwa likizo nje ya Bunge, wananchi huko nje ya Bunge wanatuelewa. Wananchi nje ya Bunge sisi uwanja wetu wa kucheza na watu wanaotushangilia wako nje, hapa wacha washangiliane wenyewe kwa wenyewe. Nawahakikishia Makamanda msirudi nyuma. Mapigo mliyopiga akina Msigwa ndiyo yamezaa leo Halmashauri za kutosha, imezaa Wabunge wa kutosha na 2020 Wallahi na Mtume nawaambia tunachukua Serikali. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa suala la Zanzibar CCM mumshukuru Maalim Seif. Maalim Seif uzuri wenyewe anapenda Ikulu lakina ni mtu mfaidhina, ni mtu anaswali swala tano ndiyo bahati yenu, angekuwa kama akina a.k.a Nkurunzinza wallahi pangechimbika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.