Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2015, Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2015, Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. HUSSEIN M. BASHE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa fursa ya kuchangia. Kwanza nitumie fursa hii kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutupa fursa sote kuamka siku ya leo na kuja kutimiza wajibu wetu wa kisheria.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Kanuni ya 106 imesema wazi hatuna mamlaka ya kubadilisha chochote katika bajeti ya Serikali, kwa hiyo niseme, tunachofanya hapa ni kushauri ili mengine yachukuliwe yaweze kufanyiwa kazi kwenye mwaka wa fedha 2017/2018; lakini mengine itakapokuja Finance Bill ili tuweze kuitumia kuitaka Serikali kufanya mabadiliko katika baadhi ya maeneo, hilo ni jambo la kwanza. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la pili, nishukuru Wizara ya Fedha. Nimeangalia document ya mpango ambayo ilizinduliwa juzi, nimeangalia hotuba ya hali ya uchumi, yapo yale ambayo tumekuwa tukiyasema katika Bunge la mwezi uliopita wakati tunajadili mpango na yapo ambayo tumeyasema katika kipindi hiki wameanza kuya-accommodate. Jambo ninaloshukuru kutoka Wizara ya Fedha, ni kauli ya Waziri kwenye Hotuba yake ya ku-acknowledge kwamba mpango wetu wa mabadiliko kwenda kwenye sekta ya viwanda, wata-accommodate viwanda vinavyotokana na mazao ya kilimo, hili ni jambo la kheri kabisa. Kwenye maisha kutambua na kutekeleza ni vitu viwili. Hatua ya kwanza ni kutambua na ya pili ni kutekeleza. (MakofiI)
Mheshimiwa Naibu Spika, nina baadhi ya mambo ambayo nataka nishauri na tutumie Finance Bill kuweza kufanya hayo mabadiliko.
Mheshimiwa Naibu Spika, hoja ya Serikali kwenye msamaha wa mazao yasiyosindikwa; ningeomba, athari ya jambo hili ni kwa wananchi. Lengo ni kuongeza uzalishaji wa mazao, wametolea mfano, soya, mbogamboga, lakini mazao haya yakisindikwa tu yanakutana na kodi. Hapa ina-work against vision ya Mheshimiwa Rais, kwa sababu mkulima kalima mboga mboga hawekewi kodi, lakini akienda kuisindika anakutana na kodi, hili ni tatizo.
Mheshimiwa Naibu Spika, nitolee mfano wa alizeti. Tukipeleka alizeti kiwandani ikawa processed inakutana na VAT, maana yake mafuta haya ya alizeti hayamsaidi mkulima wetu kwenye value addition, tuna mu-encourage mkulima auze raw, hili ni tatizo. Ningeomba hili tusilipitishe Waheshimiwa Wabunge. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, ingekuwa inaonesha value addition kwa maana ya kwamba tunafuta kodi zote kwenye mazao yatakayosindikwa maana yake tunashauri na kushawishi wananchi wetu kuwekeza kwenye viwanda vidogo vidogo ili mazao wanayolima yaingie kwenye viwanda, wauze finished goods; hili ni eneo moja.
Mheshimiwa Naibu Spika, tozo kwenye huduma za utalii. Competitors wetu wote dunia au kwenye masoko ya jirani kwa maana ya Kenya, Msumbiji, South Africa bado Tanzania itaendelea kuwa the most expensive destination. Kwa hiyo, ningeshauri Waheshimiwa Wabunge, tusipitishe hii VAT ambayo inachajiwa kwenye utalii kwa sababu haitosaidia kabisa sekta ya utalii, bado destination yetu itaendelea kuwa ghali.
Mheshimiwa Naibu Spika, kutokana na ripoti aliyoisoma Mheshimiwa Waziri, mkitazama Sekta zilizochangia kukua kwa uchumi wa nchi yetu mojawapo ni tourism; ya pili ni usafiri; na ya tatu ni financial services. Sekta zote hizi tumeziwekea kodi, tunatarajia kweli huu uchumi uta-grow kwa 7.2? Nina mashaka, sioni kukua kwa 7.2 kama tutaweka hizi kodi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, leo hii Beira, Mombasa, wamefuta kodi za ongezeko la thamani, kwenye goods on transit; sisi tumeweka, nini tunatarajia? Maana tume- tighten taratibu zetu za kukusanya kodi bandarini, ni jambo jema sana, lakini tunaweka kodi, kuna uwezekano wenzetu waliofuta, watu wakakimbilia kule. Kwa hiyo, ningeshauri Serikali ikaachana na kodi hii.
Mheshimiwa Naibu Spika, kaka yangu Mheshimiwa Zungu kaongelea kodi ya mitumba, niwaombe hatuna viwanda vya nguo vya ku-meet mahitaji ya nchi yetu, lakini tukiweka kodi kwenye mitumba, tuna discourage importation ya mitumba, tutaua small business, tutaua soko la pale Dar es Salaam, Wamachinga wanaojitafutia riziki barabarani, matokeo yake tutaongeza vibaka barabarani. Tujenge kwanza uwezo wa kuzalisha nguo ndani ya nchi ndipo tu-impose kodi kwenye hili.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini Serikali itasema; na mimi hili kidogo nina mashaka Mheshimiwa Waziri. Serikali itasema inatoa wapi fedha? Kwa sababu hizi kodi zina budgetary implication. Ushauri, yapo maeneo ambayo hamna sababu ya Dkt. Mpango kuchukua fedha kutoka kwenye Mfuko wa Hazina kuyahudumia:-
Moja, tumetengea hundred and sixty one billion Shilling, kwa ajili ya kununua vichwa vya treni na mabehewa, ningeshauri kuna sheria zinakuja kwa mwendokasi huku, tutaletewa hapa. Leteni moja ya sheria ya RAHCO, tuifute RAHCO iwe chini ya TRL. TRL ikakope fedha hizi; kwa nini tukulazimishe Mpango uwape cheki ya one sixty one billion TRL wakati wana uwezo wa kujiendesha?
Mheshimiwa Naibu Spika, mwondoeni huyu mzimu unaoitwa RAHACO hili ni chaka la wizi. Mwekeeni hizi mali zote TRL, ataenda kukopa kwenye financial institution. Nimwambie Mheshimiwa Waziri, ana one of the best CEO kwenye TRL Masanja, ametoka Private Sector anajua hela, anajua biashara, amwezeshe kwa kumletea hiyo sheria. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kuna kodi ya kiinua mgongo cha Wabunge, nataka niishauri Serikali na nataka niwaambie Waheshimiwa Wabunge, Serikali hapa imetuletea kamtego kutaka kutochonganisha na wananchi, kwamba tunajipendelea. Sheria ya The Political Service Retirement Benefit Act ya mwaka 1999, section 24(2) imeelezea exemption; subsection (4) imewa-define those leaders waliopewa exemption, nataka aniambie Waziri wa Fedha kama kweli tunataka kuwa fair kwa nini kamwacha Mheshimiwa Rais, Waziri Mkuu, Mawaziri, Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya? Mimi nasema Wabunge tulipe kodi, lakini wawekeni wote.
Mheshimiwa Naibu Spika, it is unfair kutuchonganisha na wananchi, Majaji why not? Wawekeni wote walipe. It will be fair mbele ya macho ya sheria, itakuwa fair mbele ya kila mtu kwamba tunalipa kodi wote kama tumeondoa exemption, achene kufanya division; msitu-divide, wawekeni wote walipe. Eee na Naibu Spika na Spika wote tulipe. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nimpongeze Mheshimiwa Waziri wa Fedha determination na dhamira yao ya kupeleka asilimia 40 ya fedha ya maendeleo kwa wananchi, ni jambo jema sana, lakini nataka niwaulize swali, hivi unapelekaje fedha Halmashauri ya Nzega, halafu CAG umemkata miguu.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimesikia kengele, aaa, ya kwanza.
Mheshimiwa Naibu Spika, dada yangu Neema kanipa dakika zake.
Eee nashukuru. Mheshimiwa Naibu Spika, tumepeleka 40 percent ya fedha za umma…
Mheshimiwa Naibu Spika, Neema Mgaya, dakika tano.
Mheshimiwa Naibu Spika Ahsante. Waziri Mpango, Hazina, TRA; wanakimbizana barabarani kukusanya fedha wanapeleka 40 percent ya fedha za maendeleo kwa wananchi; jambo jema lakini mnapelekaje fedha bila kumwezesha watchdog? Watch dog wa Serikali na Bunge hili ni CAG, lakini tunampunguzia fedha. Halafu tumempunguzia fedha wanahitaji taarifa za CAG ili wakazitekeleze mfano TAKUKURU tumewapa 72 billion, how? inakuwa vice-versa hii. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, ningeshauri Serikali na Waheshimiwa Wabunge; Waziri Mpango aliulizwa swali hapa akasema kwamba CAG akiishiwa atakuja kugonga mlango; jamani! Yaani wanataka aende kugonga mlango kwake, Mzee nimeishiwa hela ya mafuta na yeye atampa kutoka wapi Mheshimiwa Waziri?
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo ningeshauri CAG aongezewe fedha; zinatoka wapi? Zile bilioni 161 tulizokuwa tukanunue mabehewa na vichwa vya treni tuchukue fedha kule kwa sababu hakuna sababu, RAHCO ivunjwe, TRL wakakope twende huko. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la pili, nashtuka kidogo. Kwenye bajeti ya mwaka 2015/2016 inflow expectation kutoka kwa donors ilikuwa 2.14 trillion Shillings, lakini tuliyopokea ni 65 percent only. Mwaka huu kwenye bajeti tumeongeza kwenda 3.7 trillion. Najiuliza kama zile za mwaka jana wale wale development partner hawajatuletea, tuliyotaka kukopa kwao hawajatupa, mwaka huu kuna muujiza gani watupe three trillion Shillings? Nini madhara yake? Target mliyojiwekea mnaweza msiifikie. Ningeshauri m-review hii, simameni kwenye 1.4 ambayo mliipata mwaka jana. Mkipata ziada ni kheri, lakini ni afadhali kupanga yale ambayo tunaweza kuyafanya.
Mheshimiwa Naibu Spika, tumeweka kodi kwenye crude oil, tunataka tumsaidie huyu mwananchi wa chini, lakini kwenye mafuta ya alizeti yanayosindikwa pale Singida na Shinyanga tumeweka 18 percent, yanayokuwa imported tumeweka kodi, huyu mwananchi wa Nzega ananunua haya mafuta kwa bei ghali. Hatuna sababu ya kuweka kodi kwenye crude oil, wala hatuna sababu ya kuweka kodi kwenye mazao ya kusindika; hasa ya chakula na mafuta.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini Mheshimiwa Waziri, kwenye bajeti ametenga, ingawa nimeona kwenye kitabu cha maendeleo ni one trillion ya standard gauge; lakini kwenye hotuba amesema 2.4 trillion, kidogo nashindwa kuelewa. Hata hivyo, nauliza hivi, hivi ni lazima kweli 15 percent ya commitment ya nchi tuweze kutumia fedha zetu za ndani kuweka?
Mheshimiwa Naibu Spika, ningeshauri Serikali iangalie uwezekano, pamoja na kuwa tunajenga reli ya kati, ambayo mimi naiunga mkono, reli ya kati ya mtazamo wa Kitanzania hatuna sababu ya kutumia fedha zetu za mfukoni kufanya hili jambo; hebu tuangalie option ya PPP kama itawezekana, lakini jamani kuna uwezekano wa concession, why should we go for our pocket every now and then? Ningeshauri Serikali kuwaza kufanya kila kitu kutoka mfukoni kwake.
Mheshimiwa Naibu Spika, ameongea Mheshimiwa Profesa Norman na Mheshimiwa Zungu kuhusu suala la ku-impose kodi kwenye transfer ya share. Wenzetu wamefuta halafu bahati mbaya tumeweka kwa foreigners 20 percent, kwa wa ndani 10 percent na ukiangalia listed companies pale ni chache, matokeo yake hawa watu watakimbilia Nairobi Stock Exchange, watakwenda kule kwa sababu kuna incentive. Ningeiomba Serikali, dhamira ya kukusanya ni njema, lakini nakuomba Mheshimiwa Waziri kodi isiwe ni ya kukusanya tu itumike kama stimulus kwa ajili ya maendeleo ya uchumi wa nchi hii. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja. Ahsante sana.