Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2015, Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Dr. Dalaly Peter Kafumu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igunga

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2015, Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. DKT. DALALY P. KAFUMU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Naomba nimshukuru Mungu tena kwa kunipa nafasi hii mara ya nne kuchangia katika Bunge lako.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niipongeze Serikali kwa mambo makubwa mawili. La kwanza, Serikali kutenga fedha nyingi kwenda kwenye maendeleo kwa sababu fedha hizi zitawafikia wananchi.
La pili, azma ya Serikali ya kujenga viwanda (nchi ya viwanda), hili ni jambo zuri na tunalipongeza. Tutakuwa na changamoto nyingi ambazo Waheshimiwa Wabunge wanazisema lakini nadhani tukitekeleza haya mambo mawili nchi yetu itafika mahali pazuri. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nichangie mambo kadhaa. La kwanza ni hili jambo la gratuity ya Wabunge, naomba nianze na hilo. Sheria ya mwaka 1999 ya Political Service Retirement Benefit iliwekwa makusudi kwamba viongozi hawa wa kisiasa spectrum yote mpaka DC, wamefanya kazi kubwa sana ya kuhangaika na wananchi, wanapewa retirement ya namna ile kwa kuwapongeza na kuwapa zawadi na hii ilikuwa ni hekima tangu mwaka 1981 sheria ilipotungwa na kurekebishwa. Sasa leo kama hekima ya Serikali ni kuiondoa, nadhani watafakari vizuri zaidi kama alivyosema Mheshimiwa Ngeleja ili kama ni lazima basi spectrum nzima ya viongozi iweze kulipa kodi kwenye mafao yao. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la pili amelisema tena Mheshimiwa Waziri wangu mstaafu ni kuhusu sekta ya uchimbaji wa madini ambapo kwenye nchi zingine ni injini ya uchumi wa nchi zile. Serikali ilianza vizuri sana miaka ya 1990 mpaka miaka mitano iliyopita kuhamasisha uchimbaji mkubwa pamoja na uchimbaji mdogo, lakini mwaka huu uchimbaji mkubwa sijausikia kabisa. Tutafanya makosa makubwa sana kwa sababu sekta hii ni sekta inayoleta FDI ya kutosha, ni sekta inayoleta ajira na mifano ya Afrika ipo. Botswana, South Africa, Mali, Ghana, Burkina Faso hata DRC Congo ni nchi ambazo uchumi wao unategemea sana madini, sasa sisi tunaacha kuwaalika wawekezaji wakubwa waje kuwekeza katika nchi yetu kufanya kazi hii, tunafanya makosa. Naomba Serikali tutafakari tena kuna kitu gani kimetokea, sheria nzuri tunayo, nilisema wakati nachangia kwenye madini na narudia tena jamani Serikali tuhamasishe uwekezaji katika spectrum yote. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo lingine ambalo nataka kuzungumzia ni misamaha ambayo walikuwa wanapewa mashirika ya kidini wanapoingiza vitu kwa ajili ya shughuli zao. Serikali inasema watalipa halafu watarudishiwa, mimi nina mifano katika sekta ya madini, unapo-export unasamehewa VAT na unalipa hiyo VAT kurudishiwa ni ngoma. Makampuni yanaidai Serikali hii shilingi bilioni zaidi ya 100, wameshindwa kabisa kurudisha. Tusifikirie kurekebisha jambo kwa kuongeza kodi, turekebishe mfumo. Sisi kila kitu kikiharibika kwenye kodi tunaenda kwenye kodi badala ya kurekebisha mfumo ambao umefanya hii kodi isikusanywe. Kwa hiyo, naomba sana mashirika ya dini yanapoleta vitu kwa ajili ya kuhudumia wananchi wetu yasamehewe kama kawaida, turekebishe utaratibu wa kukusanya hizo kodi.
Mheshimiwa Naibu Spika, leo nazungumza kidogo kidogo ili niweze kuchangia mambo mengi, jambo lingine ambalo napenda kuchangia ni kuhusu watumishi wa umma. Mheshimiwa Rais alipoingia katika Serikali yake amefanya kazi moja nzuri sana ya kuhakikisha discipline inarudi katika utumishi wa umma. Amefanya ziara za kushtukiza na amefanya mambo makubwa na sisi tunamuunga mkono. Hata hivyo, kuna changamoto imejitokeza kwa wale wasaidizi wa Mheshimiwa Rais wameshindwa kurudi kwa wafanyakazi na kuwapa motisha (morali) ya kufanya kazi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, mtaalam mmoja wa mambo ya psychology ya institutional structures alisema hivi:-
“Leaders must know how to develop their EQ and put into practice to attain emotional intelligence, they need for insparing others to achieve. These emotionally excellent leaders are able to create a heart of an emotionally intelligent organization. An emotionally intelligent organization is one where its leaders and their followers exhibit a high level of emotionally excellence which allows them to connect one another and deliver in the organization.”
Mheshimiwa Naibu Spika, sisi nchi yetu ni organization ambayo viongozi wanaosimamia wafanyakazi na wafanyakazi wenyewe lazima wawe na uhusiano ambao siyo wa paka na panya, uhusiano wa kuogopana, hatutapata mafanikio mazuri katika kufanya kazi.
Kwa hiyo, naomba wasaidizi wa Rais (Mawaziri na wasaidizi wao) hebu warudi kwenye Wizara zao. Mimi nimekaa kwenye Wizara, mtumishi usipompa hamasa ya kufanya kazi atagoma kimya kimya, huwezi ukapata matunda ya kazi yake. Leo hii ukienda kwenye Mawizara watu wameinama wanasema naogopa kutumbuliwa. Viongozi mnaosimamia watumishi, wahamasisheni watumishi wapende kazi yao, wasiogope, wajisikie kufanya kazi kuipenda nchi yao vinginevyo productivity itaharibika, tutaendelea kutumbua lakini hatutapata mafanikio mazuri. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, la mwisho nataka niseme habari za Mkoa wa Tabora. Mkoa wa Tabora ni mkubwa kuliko mikoa yote Tanzania na ndiyo maana tumeomba tuugawe. Mkoa wa Tabora una matatizo ya maji kuliko mikoa yote Tanzania. Mkoa huu unahitaji kutazamwa kwa jicho tofauti. Tunaomba ule mradi wa kuleta maji Mkoa wa Tabora kutoka kule Malagarasi utekelezwe ili Tabora tupate maji.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwenye elimu Tabora tunaonekana wa mwisho, lakini ni kwa sababu ni mkubwa, usimamizi unakuwa ni mgumu sana kwa viongozi wetu. Leo ninavyoongea Mkuu wa Mkoa wa Tabora hana gari, hawezi kutembea kabisa kuzungukia maeneo yake unategemea elimu itakuwaje? RAS naye pia hana gari na ma-DC wetu nao hawana magari.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba Serikali iuangalie Mkoa wa Tabora na itusaidie tuweze kufanya kazi kuwahudumia wananchi wetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo, naunga mkono hoja na ahsante sana kwa kunipa nafasi.