Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Joshua Samwel Nassari

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Arumeru-Mashariki

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. JOSHUA S. NASSARI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru. Kwa kuanza, sincerely kabisa nimpongeze sana Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Hifadhi la Taifa pamoja na timu yake kwa kazi nzuri ambayo wamekuwa wakiifanya. Pamoja na changamoto ndogo ndogo ambazo bado zipo, lakini nyingi tunajua zinasababishwa na financial constraints na tukizingatia kwamba makusanyo yote yanayokusanywa na TANAPA yanakwenda kwanza kwenye Mfuko Mkuu wa Serikali. Kwa hiyo, kwa kweli nimpongeze na ni matumaini yangu kwamba, yale madogo madogo ambayo bado hayajafanyiwa kazi na yenyewe yatafanyiwa kazi kadiri muda unavyokwenda.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kwa kuwazungumzia ma-guides ambao ndiyo wanafanya kazi za kuwa na watalii tangu wanapoingia nchini mpaka wanapoondoka. Makampuni ya utalii yanatengeneza fedha kupitia biashara ya utalii, lakini ukiangalia mtu ambaye ana-deal na utalii tangu mtalii anapotua airport mpaka siku ya mwisho anaporuka ni guide, lakini ukiangalia maisha yao, ukiangalia namna gani ambavyo wanakuwa mistreated, kwa kweli inasikitisha sana. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nitumie fursa hii kumwomba ndugu yangu Profesa Jumanne Maghembe pamoja na Mhandisi Ramo Makani kwamba sasa waielekeze Wizara au hao Maafisa ambao wapo kwenye Wizara yao waangalie ni namna gani ya kukaa chini na vyama vya hawa waongoza utalii kwa maana ya guides ili wazungumze nao na waangalie changamoto ambazo wamekuwa nazo na waangalie ni kwa namna gani wanakuwa mistreated na kampuni na ni namna gani ambavyo kampuni zinaamua tu ku-hire and fire leo ama kesho. Vile vile guides wengi wamekuwa hawapati ajira za kudumu kwenye kampuni zao, bado wanafanya kazi kama vibarua.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini ukiachilia mbali hawa guides vile vile wapo watu ambao wanaitwa porters ambao wanabeba mizigo na kusindikiza wageni kupanda mlimani. Siku za nyuma Serikali iliagiza kwamba kila porter ambaye anakwenda na mgeni milimani kwa siku moja alipwe fedha ambazo siyo chini ya dola 10 za Kimarekani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mpaka tunavyozungumza leo hii bado wapandisha wageni mlimani wapo ambao mpaka leo hii wanalipwa sh. 6,000/= mpaka sh. 5,000/= kwa siku; na kazi wanayoifanya ni kubwa kupindukia kwa sababu wakati mwingine watalii wanaugua wakiwa njiani na wengine wanazidiwa wakiwa wanapanda mlima. Pia hawa watu kazi yao si tu kubeba mizigo peke yake kuna wakati mwingine unakuta mpaka kuwabeba watalii wakati wakizidiwa wanapougua huko njiani na wanaofanya ile kazi ni porters.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nilishawahi kuona porters wakisafirisha watalii ambao wamejiharishia kwa sababu ya hali mbaya ya hewa, kuzidiwa wakiwa mlimani, lakini ukiangalia pesa wanayolipwa mtu analipwa sh. 6,000/- kwa siku na anapanda mlima kwenye high altitude. Kwa kweli inasikitisha. Kwa hiyo naomba Mheshimiwa Waziri atakapokuja hapa atoe maelekezo upya kwamba wanaopandisha wageni mlimani wanapaswa kulipwa shilingi ngapi na kampuni ambazo haziwapi ile dola 10 ambayo Wizara ilielekeza tujue wanachukuliwa hatua gani. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya hilo, niongelee suala moja ambalo limezungumzwa pia kwenye hotuba ya Msemaji wa Kambi ya Upinzani kuhusu kampuni inayoitwa Green Mile Safari Limited. Kampuni hii na naamini kwamba ofisi ya umma (The Public office) is an institution. Anapoamua Waziri mmoja kumnyanganya mtu leseni kwa sababu amekosa sifa za uwindaji na ushahidi upo wa nyaraka, picha za video na picha za mnato, halafu mwaka mmoja au miwili baadaye anakuja Waziri anamrudishia tena mtu yule yule leseni ya kurudi kuendelea kuwinda kwenye kitalu. Halafu unamnyang‟anya kampuni nyingine kama wanavyonyang‟anywa hao Winget Window safaris.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaomba tufahamu, hivi ni kwamba maamuzi yaliyofanyika miaka miwili iliyopita hayakuwa maamuzi sahihi? Hizi zile picha za video na picha za mnato ambazo zilionyesha namna gani hawa watu walikuwa wanawinda jike wadogo ambao hawaruhusiwi kuwindwa kwa mujibu wa taratibu leo hii wamekuwa watakatifu tena?. Ndiyo maana inasemwa mtaani kwamba kampuni hii ilikuwa ina backup kutoka State House.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa sina uhakika lakini mtanifanya niamini hivyo kwa sababu kama imenyanganywa leseni kwa kutokufuata taratibu halafu leo hii mnairudishia bila kufuata taratibu tena, tunapata mashaka kidogo. Mheshimiwa Maghembe tusije tukapata wasiwasi na yeye na utendaji wake wa ofisi, naomba alizungumze wakati anahitimisha, vinginevyo tutafanya vile ambavyo huwa tunafanya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini lingine niongelee kuhusu TFS. Sisi kule Meru kwa mfano lipo shamba la miti na wanaotunza mashamba yale ni wananchi wa vijiji vinavyozunguka, kama Vijiji vya Kilinga, Mulala, Songolo, Sakila na vijiji vingine.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka wa juzi baada ya kuvuna miti; wakati TFS wanapanda miti mingine wananchi huwa wanapewa zile plot wanalima huku wanatunza miti. Lakini badala yake tumeona kwa miaka ya hapo nyuma na hususan mwaka 2014; kwamba badala ya kuwapa wananchi ambao wanazunguka yale mashamba, wanapewa watu wengine kutoka nje, wanapewa watu kutoka Jeshi la Polisi, anapewa OCD wa Wilaya ili waki-backfire awasaidie kuzuia wananchi. Sasa tunaomba tu kujua hivi nini maana ya dhana ya ujirani mwema? Hivi hawa wananchi siku moja akaamka tu mwananchi kichaa akachukua dawa akaenda akapiga ile miti si itakufa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, tunaomba hawa watu wa TFS wahakikishe wanaboresha mahusiano na vijiji vinavyozunguka na mojawapo ya namna ya kuboresha mahusiano ni ikiwepo kuhakikisha wanaopata zile plots za kulima ni wa vijiji vinavyozunguka.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ni habari ya hoteli za kitalii na masuala ya service levy kwenye Halmashauri zetu. Kwa mfano tu kwa Halmashauri yangu ya Meru peke yake, kwa takwimu za mwaka mmoja wa fedha peke yake, nitasoma baadhi ya hoteli tu hapa. Hoteli ya Dik Dik peke yake tumeshindwa kupata mapato kwa mwaka mmoja shilingi milioni tisa na laki tisa. Hoteli ya Kigongoni shilingi milioni mbili laki nane; hoteli ya Arumeru River Lodge shilingi milioni tatu na laki nne; hoteli ya Hatari Lodge shilingi milioni kumi na laki moja; hoteli ya Mountain Village shilingi milioni thelathini na laki tisa; kampuni ya Macho Porini Tours zaidi ya shilingi milioni mbili na laki tatu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ukijumlisha kwa mwaka mmoja wa fedha kwa haya makampuni sita niliyoyataja hapa peke yake Halmashauri tume-loose zaidi ya shilingi milioni 59. Sasa milioni 59 kwa hoteli sita peke yake kwa Halmashauri moja maana yake it’s a lot of money kwa miaka mitano ambazo zingeweza kusaidia wananchi wetu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa tungeomba kujua ni kwa namna gani hawa watu wanakwepa? Wengine wanajisajili kwenye EPZ ili waweze kupata grace ya kodi? Kwa hiyo, ningeomba Mheshimiwa Waziri hili nalo akija alizungumzie ili tusije tuka-suffocate Halmashauri zetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, la mwisho na muhimu sana, ni Operation Tokomeza. Nilikuwepo kwenye Bunge lililopita na tulizungumza kuhusu habari ya Operation Tokomeza na Bunge hili lilielekeza Serikali kwamba ifanye nini na maazimio tuliyapitisha hapa ndani ya Bunge lako Tukufu. Badala yake leo hii ni miaka miwili ama mitatu baadaye bado maazimio ya Bunge hayajatekelezwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jamani tusisahau kwenye Operation Tokomeza tunao wananchi ambao wamepoteza maisha, ambao walilazimishwa mpaka kufanya mapenzi na miti, tunao watu ambao walilazimishwa kufanya mapenzi mbele ya watoto wao wakiwa wanaona, tunao watu ambao walinyanganywa ya mbao mpaka leo wameingizwa kwenye umaskini, tunataka kujua fidia zao ni lini? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, yale maazimio ambayo yaliazimiwa ndani ya Bunge hili Tukufu ni lini yanakwenda kutekelezwa. Kwa sababu tunajua kuna baadhi ya watu wamesafishwa lakini mimi ninao wananchi mpaka leo wanaripoti polisi, ninao wananchi mpaka leo wamenyang‟anywa silaha zao halali ambazo wamemilikishwa kihalali zipo polisi mpaka leo hawajarudishiwa. Tunao watu ambao wameingizwa kwenye umaskini baada ya Operation Tokomeza na kwa kweli hatujui ni kwa namna gani wanakwenda kufidiwa, hatujui ni kwa namna gani tunaenda kugusa ile trauma ambayo waliipata kupitia Operation Tokomeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho kabisa ni hii ha bari ya ufugaji, uhifadhi pamoja na ukulima. Ndugu zangu katika hili niseme wazi kwamba, viongozi lazima tuangalie tusije tukaligawa Taifa vipande vipande. La pili, vile vile niulize hivi ni lini ng‟ombe wamewahi kula miti, hivi ni lini ng‟ombe wamewahi kuchoma mkaa, kwa sababu leo hii tunasema kwamba wafugaji tuwaondoe kabisa kama vile hawapo kwenye ramani ya hili Taifa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ukweli ni kwamba baadhi yetu tumekuwa Wabunge, tumekuwa Mawaziri, tumesoma kwa sababu ya ng‟ombe. Naomba nioneshwe leo hii nani Waziri hapa ambaye amewahi kusoma kwa sababu ya utalii peke yake? Ni mwananchi gani Mtanzania ambaye anaguswa moja kwa moja na impact ya utalii kwenye nchi ukilinganisha na impact ya ufugaji kwenye Taifa letu? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa tunakosea viongozi na baada ya hapo tunakwenda kuwatesa wananchi. Mheshimiwa Profesa Jumanne Maghembe, nilimsikia kauli yake aliyoisema, anapaswa kuwaomba radhi Watanzania na hususani wafugaji wa Taifa hili. Narudia akitaka abaki salama kwenye kiti chake na nilifikiri pengine angekuwa Waziri wa kwanza kuja kutumbuliwa kwa ile kauli, kwa bahati mbaya Kitwanga ametangulia, nimwombe anapaswa kuwaomba radhi Watanzania baada ya hapo akaw chini na Waziri wa Ardhi na Waziri wa Mifugo wazungumze waangalie ni kwa namna gani tunaweza ku-strike a balance. Tunahitaji mifugo, tunahitaji conservation at the same time tunawahitaji wakulima. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo hawezi tu kuwafanya wafugaji ni kama vile ni jamii ambayo imekuwa neglected, ni watu ambao wamekuwa vulnerable kwa miaka mingi, at the same time na yeye Minister anasimama anaanza kusema kama vile kwanza hatufugi, hatuhitaji ng‟ombe kwenye nchi, hatuhitaji nyama wakati nimemwona leo akila nyama canteen. Sasa nashindwa kuelewa, hawa ng‟ombe anaowakataa mbona leo alikuwa anawala kwa nini asingekula msitu pale canteen leo, kwa nini asingekula nyama ya simba pale canteen! (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naomba sana tunapokuwa viongozi tuangalie namna ya kuliunganisha Taifa na siyo kuligawa Taifa, tunawahitaji wafugaji, tunahitaji uhifadhi, tunawahitaji wakulima ili Taifa liweze kusonga mbele...
MWENYEKITI: Ahsante.