Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Daniel Edward Mtuka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Mashariki

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. DANIEL E. MTUKA: Mheshimwa Mwenyekii, nikushukuru kwa nafasi hii, na mimi niweze kutoa mchango kwenye Wizara hii ya maliasili na utalii. Niende moja kwa moja kwenye eneo la migogoro kati ya hifadhi na wananchi, lakini migogoro kati ya wakulima na wafugaji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nini chanzo cha migogoro hii? Iko mingi lakini mimi nimeona viko vyanzo vinne. Sababu ya kwanza ni ongezeko ya watu na mifugo wakati ardhi haiongezeki. Ni kweli wakati wa uhuru tulikuwa watu milioni tisa sasa hivi tunakwenda kwenye 50. Mifugo ilikuwa michache lakini sasa hivi mifugo ni mingi, lakini ardhi iko palepale. Pale kwangu Manyoni sasa hivi tumeongezeka sana lakini pia watu wanaohamia. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sababu ya pili ya migogoro hii, ni uharibifu wa mazingira, tunakata miti sana. Kwa mfano, kwangu pale Manyoni upande wa Mikoa ya Magharibi wamekata miti sana, mazingira yameharibika, sasa wanakuja wanasogea Mkoa wa Singida-Tabora wanavamia huko kuja mpaka Chunya na Mbeya. Watu wanakata miti watu wanachoma mikaa. Kaskazini huku, kuna shida pia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hicho ni chanzo cha mgogoro cha nne kwamba, baada ya mwaka 2009 sheria ilibadilishwa mipaka ya hizi hifadhi ikafinywa ikala maeneo makubwa sana, Umasaini huku, Ugogoni huku, imekula sana Usukumani huku. Watu wanahama kutoka Umasaini, watu wanahama kutoka Usukumani magharibi wanakuja kuvamia Morogoro, Rukwa na maeneo mengine; huu ni mgogoro wa moja kwa moja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nilisikia mchangiaji mmoja jana anachangia kwa nguvu sana kwamba sisi hatukuwahi kuona ng‟ombe wengi wa namna hiyo. Sasa hivi tunaona malaki ya ng‟ombe ni vitu vigeni kwetu lazima huo ni mgogoro.
Mheshimiwa Mwenyekiti, chanzo cha mwisho nilichokiona mimi ni uvamizi wa mifugo kutoka majirani zetu, Rwanda, Kenya, wanaingia kwenye misitu, wanawasukuma wenyeji huku tunaanza kugombana nao, hicho ni chanzo pia cha migogoro.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nini sasa kifanyike? naiomba Serikali yangu ambayo ni sikivu ya Chama cha Mapinduzi irejeshe mipaka ya zamani kwenye hifadhi. Zamani ile mipaka Mungu ameiweka ni ya asili, Wanyama wanakaa kule Binadamu anakaa huku tusilazimishe kuongeza mbuga zile, tusilazimishe kuongeza misitu wakati sisi tunaongezeka, mifugo inaongezeka. Naomba sheria hii ibadilishwe, mipaka hii irejeshwe ile ya zamani, eneo hili litatupa ardhi kubwa sana migogoro hii itapungua.
Mheshimiwa Mwenyekiti, njia nyingine ya kupunguza migogoro ni wakati sasa wa kutekeleza ule mpango wa matumizi bora ya ardhi. Tutenge sasa matumizi bora ya ardhi. Kilimo tuwatengee eneo lao, wafugaji maeneo yao, makazi maeneo yake, viwanda maeneo yake, madini maeneo yake. Hebu tupange hii. Tuipime nchi tuweke mipaka ambayo iko clear, ugomvi huu utapungua.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kitu kingine ambacho kitasaidia, kuna dormant Ranches. Ranch ambazo hazitumiki, tuangalie uwezekano wa kubadilisha matumizi. Kuna maeneo ya hifadhi pia ambayo hayana tija, tuyabadilishe matumizi pia. Tugawe kwa wakulima, tugawe kwa wafugaji, itatuongezea ardhi na pia migogoro hii itapungua.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine. Sisi wakulima na wafugaji, mimi ni mkulima pia na ni mfugaji. Namwomba hata Mzee Mtuka anisikilize kwenye jambo hili. Wafugaji tuwe tayari kupunguza idadi ya mifugo. Tupunguze idadi ya mifugo tumeongezeka na mifugo imeongezeka. Ardhi haiongezeki, sehemu za kuchungia haziongezeki, tuwe tayari kupunguza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Serikali ilisimamie hili, zile Wizara nne zile zisimamie, zikae na wakulima, zikae na wafugaji, waseme wao kiwango cha mwisho cha mfugaji kuwa na mifugo ni kiasi gani? Kama ni ng‟ombe mia moja tukubaliane iwekwe kwenye sheria, tukubaliane hilo. Haiwezekani mtu ana ng‟ombe 2,000 mwingine 5,000 haiwezekani ardhi haipo. Wafugaji wenzangu natoa wito, tukubaliane kiwango rasmi ambacho kila mfugaji ataishia kufuga. Huwezi kufuga tu yaani ng‟ombe unaotaka, haiwezekani, hili pia liwekwe kwenye sheria.
Mheshimiwa Mwenyekiti lakini kingine, baada ya kugawa yale maeneo, upande wa wafugaji nashauri sana wawekewe miundombinu. Hebu Serikali itusaidie, leteni hata yale magreda na vile vijiko vya Jeshi. Chimbeni mabwawa kule kwenye maeneo ya wafugaji ambayo yametengwa, chimba hata mabwawa maji yajae huko, weka majosho, weka majengo ambayo Wataalam wa Mifugo watakuwepo kule ili kuwa-control hawa wafugaji wasiweze kuhama hama. Ukiweka miundombinu hii, wafugaji hawatahama. Naliomba sana hilo, Serikali isaidie.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nihame hapo, nizungumzie kidogo vivutio vya utalii. Sisi Manyoni kule tuna kivutio kipya ambacho tunataka tukitilie nguvu na tunaomba Serikali ituunge mkono. Ukiiweka Tanzania kwenye ramani, ukai-set kwenye mitambo ile, ukatafuta kile kitovu cha nchi kinatua Manyoni, kuna sehemu inaitwa Kisingisa. Hebu naomba mtusaidie Serikali eneo lile.
MWENYEKITI: Ahsante.