Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Mbaraka Kitwana Dau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. MBARAKA K. DAU: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote nakushukuru kwa kunipa fursa hii ili nami niweze kuchangia hotuba hii ya Waziri wa Maliasili na Utalii. Mheshimiwa Waziri nianze kwa kuunga mkono hoja yako.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pili suala la utalii ni suala ambalo lipo interconnected, tunazungumzia utalii ambao uko under utilized. Utalii ili uwe utalii, utalii ili uweze kufanya kazi sawasawa ni lazima sekta nyingine saidizi ziweze kusukuma twenda sambamba, kwa mfano, suala la miundombinu kuanzia barabara na maeneo mengine ya usafiri, hata huduma za viwanja vya ndege. Matatizo yetu ya usafiri na utalii yanaanzia pale airport ya Dar es Salaam na Kilimanjaro. Mtalii anakuja anakutana na mazingira ambayo ni very unfriendly, hawezi kupata huduma nzuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mtalii anakaa anasubiri wale wanaochukua visa on arrival anakaa masaa matatu, mwingine anakaa kwenye foleni pale airport yenyewe, kuna joto, air condition hazifanyi kazi anaanza ku-experience matatizo akiwa pale kiwanja cha ndege. Sasa tunapozungumzia kukuza utalii tuangalie na aspect kama hizi tuhakikishe kwamba vituo vyetu vya airport na maeneo mengine ambayo watalii wanakuja wanaanza ku-experience mambo mazuri, pamoja na vitanda kule kwenye hoteli zetu ziwe za kutosha na miundombinu mingine.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hii dhana ya utalii tumejikita zaidi kuangalia mbuga pamoja na Mlima Kilimanjaro na vivutio kama hivyo. Lakini dhana ya utalii ni pana zaidi ya Mlima wa Kilimanjaro na mbuga. Kwa mfano, mimi natokea kisiwani Mafia, Kisiwa cha Mafia ni kisiwa tajiri sana kwa utalii, lakini mazingira ili uingie Mafia ni magumu kweli kuanzia usafiri kwa maana usafiri wa bahari na usafiri wa ndege. Lakini kubwa zaidi ni namna gani Serikali inatangaza utalii katika maeneo mbalimbali ya vivutio hivi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mafia tuna samaki anaitwa a whale shark au kwa jina lingine la Kiswahili anaitwa Potwe, samaki huyu ana tabia kama za dolphin, ni samaki friendly anaweza akaogelea na watalii, hana matatizo. Lakini dunia nzima samaki huyu anapatikana Australia na Mafia tu. Ni wangapi miongoni mwa Watanzania tunalijua hilo kwa utalii wa ndani peke yake ikilinganishwa na utalii wa nje? Kwa hiyo tunahitaji kwanza kutangaza na kuwekeza katika miundombinu ili vitu hivi vinapokuwa connected pamoja, basi utalii wetu utasonga mbele.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mafia kuna vivutio mbalimbali kama scuba diving, sport fishing na utalii wa kwenda kuangalia papa Potwe, lakini bado Serikali haijatia mkazo kuweza kutusaidia kutangaza utalii huu. Kikubwa zaidi Mheshimiwa Waziri pale kisiwani Mafia hatuna hata Afisa wa Utalii utawezaje kukuza utalii kwenye destination muhimu kama ya Mafia bila ya kuwa na Afisa wa Utalii wa Wilaya? Tumelizungumza hili sana, tumeandika barua lakini mpaka leo hatujapata Afisa wa Utalii.
MWENYEKITI: Ahsante muda wako ulikuwa ni dakika tano tu.