Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Doto Mashaka Biteko

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukombe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. DOTO M. BITEKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, pongezi nyingi sana kwa Wizara kwa hotuba nzuri sana. Pamoja na mambo mengine, naiomba Wizara iangalie na isaidie wananchi wa Bukombe kwa mambo kadhaa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo kubwa la Wilaya ya Bukombe ni la hifadhi ya Kigosi Muyowosi. Nashauri Wizara iwe na mpango wa kuwashirikisha wananchi katika uhifadhi na kuweka mahusiano mazuri kati ya wananchi na wahifadhi
Kwa kuwa eneo kubwa la Wilaya ya Bukombe ni hifadhi, naiomba Wizara na kuishauri iweke Ofisi ya Maliasili Wilayani Bukombe. Kwa sasa wananchi wanafuata huduma Wilayani Kahama ambako ni mbali kwa kilometa 96. Nawatakia kazi njema Waheshimiwa Waziri na Naibu Waziri