Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Prof. Norman Adamson Sigalla King

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makete

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. PROF. NORMAN A. S. KING: Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza kwa dhati ya moyo wangu Mheshimiwa Profesa Maghembe (Waziri) pamoja na wasaidizi wake wote. Masikitiko yangu makubwa ni juu ya mambo mawili:-
(i) Kutoweka mikakati ya kuendeleza Hifadhi ya Maua ya Kitulo. Hifadhi ya Maua Kitulo ni muhimu sana, lazima uboreshaji wa miundombinu ya utalii ikiwa ni pamoja na barabara za lami kutoka Chimala – Matamba – Kitulo; Mbeya – Kitulo – Makete; Njombe – Makete – Kitulo. Pia kuweka hoteli ya kitalii Matamba na Makete ili kuongeza utalii.
(ii) Ugomvi wa wachunga ng‟ombe na Hifadhi ya Taifa. Ni muhimu sana kutambua kuwa haiwezekani ukatenga eneo la kuchunga ng‟ombe, unaweza kutenga eneo la kufuga tu. Watu wetu sisi ni wachungaji ambao tabia yao kuu ni kufuata malisho. Nchi yetu ni ya kitropiki ina misimu ya hali ya hewa mikuu miwili yaani masika na kiangazi. Wakati wa masika migogoro ni michache kwa kuwa malisho ni mengi, wakati wa kiangazi migogoro ni mingi kwa kuwa wachungaji wataswaga ng‟ombe kufuata malisho. Muhimu ni Wizara kuamua kisayansi, haiwezekani kutenga eneo la kuchunga ng‟ombe, ni lazima wachungaji wafundishwe kufuga na hili ni muhimu kufanyika kupitia kufufua shamba la mifugo Kitulo.
(iii) Shamba la mifugo Kitulo. Shamba hili likifufuliwa litatumika kama eneo la kutoa mafunzo kwa vitendo juu ya ufugaji wa ng‟ombe wa maziwa na nyama. Shamba hili lilianzishwa mwaka 1965 na Mwalimu Nyerere pamoja na Mzee Karume, walijua huwezi kutenga eneo la kuchungia ng‟ombe, lazima twende kwenye uchumi wa kufuga ng‟ombe wa maziwa na nyama. Ng‟ombe wa maziwa wana faida kubwa kwa binadamu kiuchumi na kiafya.
(iv) Sheria ziwekwe na zisimamiwe kwa ukali. Waheshimiwa Wabunge bila shaka baadhi wana ng‟ombe wanaoswaga, hivyo hawawezi kuunga mkono hoja hii lakini sheria zisimamiwe kwa ukali. Mfano huruhusiwi kuswaga ng‟ombe kutoka Wilaya moja kwenda nyingine bila kibali, sheria hizi zizingatiwe.
(v) Trespass kwenye hifadhi. Ni vizuri Wizara ifahamu kuwa watu wanaochunga ng‟ombe kwenye buffer zone, baadhi yao ndiyo hubadilika na kuvuna pembe za ndovu. Kwenye hili, Wizara lazima isimamie hifadhi hizi kwa ukali. Nchi jirani ya Kenya, ukipeleka mfugo au binadamu kwenye hifadhi unapigwa risasi na wamefanya hivi kwa sababu ni vigumu kutofautisha jangili na mchunga ng‟ombe kwenye hifadhi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hifadhi ni muhimu sana kwa Taifa letu, si tu uchumi wa Taifa bali kiikolojia. Hifadhi ni msaada mkubwa wa kuhifadhi ikolojia ya mvua. Kama tukiruhusu uvamizi wa hifadhi, nchi yetu itakuwa jangwa. Serikali isimamie sheria kwa ukali, no compromise.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nawasilisha.