Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali katika Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Tunza Issa Malapo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali katika Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. TUNZA I. MALAPO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Awali ya yote, namshukuru Mwenyezi Mungu na Chama changu makini CHADEMA kwa kunipa nafasi hii. Pia napenda kuwapa pole wananchi wa Mtwara Mjini kwa kadhia ya mvua waliyoipata siku ya jana, lakini hii yote imesababishwa na miundombinu mibovu iliyowekwa na Serikali ya CCM. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kuchangia mpango huu nitajikita katika mambo mbalimbali. Mtwara imewekwa katika eneo la uwekezaji kwa maana ya viwanda, lakini tatizo kubwa la Mtwara ni maji ya kutosha kuhudumia viwanda. Mtwara Mjini kuna mradi unaotakiwa utoke Mto Ruvuma kuja Mtwara Mjini kuleta maji. Huu mradi umepitia process zote, kilichobaki ni kuwekeana saini kati ya Serikali ya China kupitia Exim Bank ya China na Wizara ya Fedha ya Tanzania, lakini huu mradi ulitakiwa uanze tangu mwezi wa Saba mwaka 2015 lakini mpaka leo haujaanza. Kwa hiyo, Mheshimiwa Waziri unayehusika, tunaomba mlifuatilie jambo hili ili tuweze kupata maji ya uhakika yatakayotosheleza kwa ajili ya kuhudumia hivyo viwanda vyetu.
Hatuwezi kuhudumia viwanda mfano, Dangote maji anayoyahitaji na maji yanayopatikana sasa hivi, akipewa yeye, maana yake sisi wananchi wa Mtwara Mjini hatuwezi kupata maji ya kutosha. Lakini suala la maji Mtwara Mjini, Serikali hailipi Idara ya Maji. Kinachotokea ni nini? Watu wa Idara ya Maji wameambiwa wajitegemee, wanajitegemea vipi wakati Serikali pale Manispaa ya Mtwara Mjini inadaiwa Shilingi milioni 581? Pesa zinakwenda, mpaka Mkuu wa Mkoa nyumbani wake anadaiwa Shilingi milioni moja na ushee. Kwa hiyo, tunachokisema, Serikali wapeni pesa Idara ya Maji waweze kujiendesha ili hata hivyo viwanda vinavyokuja viweze kufanya kazi. Maji ni muhimu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia nitaongelea elimu. Nasikitika sana, kila yanapotokea matokeo yawe ya Darasa la Saba, yawe ya Form Two, yawe ya Form Four na kwingine kote Mtwara lazima iingie kwenye kumi za mwisho. Hii ni aibu na ni fedheha kwetu, hatupendi. Nataka niwaambie, shule tatu katika mtihani wa Form Two zilizofanya vibaya, matokeo yaliyotoka juzi juzi zimetokea Mtwara. Mbili kati ya hizo, zimetoka Tandahimba ambako kuna shida kubwa ya maji; na watoto wanaohangaika wanafeli ni watoto wa kike. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunazungumzia Mtwara ya Viwanda wakati elimu yetu iko chini. Ndugu zangu tusifanye mambo yale yale kila siku, tusifanye kazi kwa mazoea. Mimi ni Mwalimu wa Walimu, naelewa vizuri. Nimekuwa nikifanya kazi na wanafunzi katika Shule. Mwanafunzi hawezi kusoma kwa kumtolea ada ya Sh. 20,000/= mwanafunzi ili aweze kusoma vizuri, anahitaji apate vitabu, anahitaji akae pazuri, anahitaji ashibe, anahitaji apate maji safi na salama. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, watoto wetu wa kike wa Mtwara, mnawalalamikia wanaolewa mapema, amefika Form Two maji yalikuwa yamhangaisha, amefeli, kinachofuata ni nini?
MHE. TUNZA I. MALAPO: Kwa hiyo, Serikali tunaomba muweke kipaumbele kwenye upatikanaji wa maji. Huu mradi wa Mto Ruvuma utahudumia vijiji 26; miongoni mwao vipo Mtwara Vijiijini na huko Mtwara Vijijini kuna shule ya mwisho imetokea huko kama sijakosea. (Makofi)
inatumiwa Bandari ya Dar es Salaam, wakati sisi tuna eneo kubwa. Kwa kuja kuwekeza kule na kui-upgrade hii bandari tunaamini vijana wenzangu kama mimi watapata ajira za kutosha na kuondokana na umaskini ambao unawatala. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho maana naona muda umeisha, nataka kusema, Chama cha Mapinduzi kilitengeneza majipu kwa miaka 55, sasa wameanza kuyatumbua hatujui watatumia miaka mingapi! Kwa hiyo, ninachosema, wala msiwaaminishe wananchi kwamba mnafanya kazi kubwa, hayo majipu mliyatengeneza wenyewe. (Kicheko/Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kuyasema hayo, naomba suala la maji lipewe kipaumbele.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia nauliza jambo moja, naomba ufafanuzi mtakapokuja kujumuisha. Suala la umeme; mimi najua mafuta yanakotoka bei inakuwa ndogo kuliko kwingine. Sisi Mtwara tunanunua mafuta bei kubwa. Kwanini umeme wote tunalipa sawa wakati unazalishwa kule kwetu? Tunalipa sawa na sehemu nyingine! Pia hilo naomba ufafanuzi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia katika suala la elimu, mimi natambua kila Wizara ina Kitengo cha Sheria; na Wizara ya Elimu bila shaka itakuwa na Kitengo cha Sheria. Sasa kama Sheria za Elimu zimepitwa na wakati, zinaruhusu matamko ya Mawaziri yanayorudisha elimu yetu nyuma, Kitengo cha Sheria Wizarani wakae wachambue wasiwape Mawaziri mamlaka yanayodidimiza elimu yetu.
Mama yangu Mheshimiwa Profesa Joyce Ndalichako, hapa katika kuzungumza, wanazungumzia Shule za Sekondari na Shule za Msingi. Nataka nikukumbushe kwamba kuna Vyuo vya Ualimu, ndiyo huko nilikotokea mimi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika sehemu yenye matatizo katika tasnia ya Ualimu ni pamoja na Vyuo vya Ualimu. Watu wa Vyuo vya Ualimu naomba ukawasikilize. Sasa hivi wameingiziwa, kuna NACTE, kuna Wizara, kuna TSD, hawaelewi, wanayumbayumba. Nenda ukawasikilize, ujue matatizo yao, wanashindwa kufanya kazi. Nimetoka huko, mpaka nachaguliwa kuwa Mbunge, nilikuwa nafundisha Chuo cha Ualimu Mtwara kawaida. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuongelea barabara. Sijui watu Mtwara tufanye nini ili mtusikie kuhusu barabara ya kutoka Mtwara Mjini, inapita Nanyamba, inapita Tandahimba, Newala Mjini mpaka Masasi. Tufanye nini ili mtusikie? Tunaomba mtujengee barabara. Korosho zinatokea huko kwa asilimia kubwa.
Mhesimiwa Mwenyekiti, vile vile Bandari yetu ya Mtwara kwanini hamtaki kui-upgrade? Kwa saabu ukisoma huu Mpango, asilimia kumi tu ndiyo inaonekana Bandari ya Mtwara na hizo nyingine, lakini asilimia kubwa