Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Mwanne Ismail Mchemba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. MWANNE I. MCHEMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, pongezi kwa Mheshimiwa Profesa Jumanne Maghembe, Waziri na Naibu Waziri Engineer Ramo Makani, Katibu Mkuu na watumishi wote kwa hotuba nzuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali iangalie uharibifu wa misitu kwa uvamizi wa wafugaji kwani kila wanapofika sehemu hukata miti yote. Kwa mfano, Kizengi, Bukene, Urambo, Bukumbi, Kitundo na kadhalika. Pia ukataji miti kwa kuchoma mkaa ni tatizo hivyo Serikali iangalie upya sheria zilizopo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu ufugaji nyuki, elimu itolewe kwa wajasiriamali ili wafuge kisasa kwa kutumia mizinga ya kisasa. Wajasiriamali hasa wanawake wakopeshwe mizinga ya kisasa kwa bei nafuu. Kuanzisha kiwanda cha kusindika asali kama ilivyokuwa zamani kwani Tabora ina historia ya kurina asali. Pia kiwanda hicho kinaweza kutumika kama Kanda ya Magharibi, Singida, Tabora, Kigoma na kadhalika kwa kusafirisha nje ya nchi pia kusindika nta.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu Chuo cha Nyuki tuombe chuo hicho kitambuliwe rasmi ili wanafunzi hao wanapohitimu mafunzo haya wapewe ajira kwani mpaka sasa ajira zao ni za kujitegemea, ni vyema sasa ajira hizo zilingane na vyuo vingine. Wanachuo hao wapewe vitendea kazi kama vile mizinga ya kisasa ili wakatoe elimu darasa maeneo mengine. Ukarabati wa chuo hicho niombe uendelee kwani maeneo mengi ni machakavu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sekta ya makumbusho; katika Mkoa wa Tabora katika Kata ya Kwihara kuna makumbusho ya kihistoria ya kumbukumbu za Dkt. Livingstone, Stanley, Said Ibin Batuta, waliokuwa watu maarufu kihistoria. Ni vyema eneo hilo pia likatangazwa kama utalii. Pia kuna majengo ya Ujerumani ambayo yana historia, ni ya maajabu. Naunga mkono hoja.