Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Zainabu Mussa Bakar

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. ZAINABU MUSSA BAKAR: Mheshimiwa Mwenyekiti, sekta hii ni sekta muhimu sana kwani inaleta pato kubwa kwa Taifa letu. Hivyo ni sekta ya kuthaminiwa sana na siyo ya kudharauliwa kama ilivyo sasa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaitaka Serikali ibadili utaratibu uliopo kwa utoaji wa leseni kwa wafanyabiashara wanaosafirisha watalii kwa kuondoa sharti la umiliki wa magari matano ndipo wapewe leseni ya kufanya biashara hiyo. Kiwango hiki kipunguzwe angalau yawe mawili au moja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na vivutio vingi tulivyonavyo vya watalii ni lazima pia kuwe na matangazo ambayo pia yatawavutia watalii, vinapotangazwa vivutio ndiyo watalii watakuja. Hivyo ni lazima tuwe na mpango madhubuti na bajeti ya kutosha ya kufanya matangazo ya vivutio vyetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia jambo lingine ni miundombinu imara husaidia na ni kivutio pia cha watalii kwani unapokuwa na miundombinu mizuri kunawafanya watalii wafike eneo hilo kwa urahisi bila ya machovu na kuweza kufurahia safari aliyokwenda.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia viwanja vya ndege viimarishwe ili watalii waweze kufikia vivutio hivyo kwa wepesi zaidi. Jambo lingine ni malazi mazuri yenye mvuto na sehemu nzuri za kujenga hoteli hizo ambazo watalii zitawavutia. Ni vema Serikali kuzingatia pia maoni ya wananchi. Vilevile kuwa na kanuni zinazowabana watalii ambazo zingeleta madhara kwa wanajamii na kizazi chetu. Kwa mfano, kuwe na maadili ya kuzingatia kama vile uvaaji wa mavazi yasiwe yanakihirisha, yawe ya heshima. Kushirikisha watu au wananchi vilivyo kufuata silka na mila au tamaduni husika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hii ni kwa sababu watoto wetu ni wenye kuiga sana mambo, watoto wengine wameharibika na kuwa hawana maadili hasa sehemu nyingi za fukwe na zenye hoteli kubwa, maadili yameporomoka kwa kuona wanayofanya. Watoto wengi huacha shule ili tu wapate ajira ya kutembeza watalii maeneo hayo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hivyo, Serikali iyaone haya na kuyafanyia kazi ipasavyo. Naomba kuwasilisha.