Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, vivutio Wilaya ya Rungwe; Wilaya ya Rungwe ina vivutio vingi sana ikiwepo Ziwa Ngozi, Mlima Rungwe, Daraja la Mungu, Kijungu na vivutio vingine vingi sana. Tatizo Wizara haijasaidia kutengeneza miundombinu ya kuwezesha watu kuja kutembelea.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Ziwa Ngozi limeachwa chafu na kutoa tozo ndogo ambayo haiwezi kuleta maendeleo yoyote. Halmashauri zetu hazina pesa ya kuwezesha kutangaza vivutio hivi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu misitu; Wilaya ya Rungwe tuna misitu ya kienyeji ambayo kiuchumi haina faida kwa wananchi wa kawaida. Vyura wa Kihansi tunaomba vyura hawa warudi Tanzania na nchi ya Marekani ilipe gharama kwa kukaa nao kwa muda mrefu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wachina na meno ya tembo; kumekuwa na wimbi la Wachina hapa nchini wakikutwa na nyara za Serikali hasa meno ya tembo, swali langu Serikali inachuakua hatua gani ya kisheria kwa wananchi hawa, je, toka wameanza wamekamatwa wangapi na wamefungwa miaka mingapi?
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu upandaji miti na nyuki ninaomba Wizara chini ya kitengo cha upandaji miti kunisaidia miche ya kupanda kwa makundi ya vijana, katika Wilaya ya Rungwe na Mkoa wote wa Mbeya. Pia mgogoro wa wafugaji Wilayani Mbarali, je, Serikali itaumaliza lini?