Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Rose Kamili Sukum

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. ROSE K. SUKUM: Mheshimiwa Mwenyekiti, migogoro ya mipaka na shughuli za kibinadamu ndani ya hifadhi za wanyamapori, sababu za mifugo kuingia kwenye hifadhi husababishwa na viongozi na watumishi wa maliasili kwa kuwanyang‟anya maeneo yao kuwa maeneo ya hifadhi bila kuwafidia maeneo mengine.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuanzisha mapori tengefu, mapori ya akiba na ushoroba maeneo hayo yote ni vijiji vilivyopimwa kwa ajili ya wananchi wanaopakana na hifadhi. Bila kuwa na utaratibu unaoeleweka kwa Wizara ya Ardhi, Maliasili, Kilimo na Mifugo, TAMISEMI na Wizara ya Maji kamwe hamtapata suluhisho la wafugaji na wakulima wanaozunguka hifadhi. Nashauri kuwa na kikao cha pamoja kutafuta suluhisho la kupatikana kwa ardhi ni kuwa na mpango wa kupatikana maeneo ya wafugaji na wakulima siyo kazi ya kuwakamata na kuwaua wao na mifugo yao. Tupeni mpango wa kumaliza tatizo hili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu Sheria Namba Tano ya mwaka 2009 (Sura 283), Sheria hii inazungumzia upande mmoja wa hifadhi. Je, maeneo mliyoongeza kwa kuwaghilibu viongozi wa vijiji kwa kutumia viongozi wa Wilaya na Mkoa, inawagusa wapi?
Sheria hii inawanyanyasa wafugaji kwa kuwanufaisha viongozi wa Wilaya na Kamati zao za usalama na mikoa kwa kulazimisha kutolewa rushwa au kukandamiza wafugaji kulipa faini. Hii mifano imefanyika Tarangire katika vijiji vya Ayamango, Galapo, Mkungunero, Sangasanga, Lulenge, Pori la Wamimbiki, Utengule huko Kilombero North Safari na kadhalika. Hii sheria ifanyiwe marekebisho.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lugha za kuudhi, kauli aliyoitoa Waziri wa Maliasili na Utalii Mheshimiwa Jumanne Maghembe katika mahojiano yaliyofanyika katika vipindi vya ITV dakika 45 ni lugha ya maudhi na dharau kwa wafugaji.
(a) Mapato yatolewayo na Maliasili na Utalii ni asilimia 22.5 huwezi kufananisha na mifugo ambayo hutoa mapato ya kiasi cha asilimia 4.5 akifananisha kuwa ukiwa na shilingi nne na ukiwa na shilingi 22 utachukua shilingi ngapi? Hiyo ni dharau, je, ng‟ombe wanaochinjwa Tanzania haijachangia kutokuagiza nyama kutoka nje? Hiyo siyo dola?
(b) Wafugaji hukaa nyuma ya mikia ya ng‟ombe zao tu, je Waziri alitakaje? Kuna style nyingine za kufuga ng‟ombe?
(c) Ng‟ombe wote walioko mipakani mwa hifadhi wana magonjwa kama kimeta, homa ya mapafu na kadhalika, hivyo nyama zao hazifai kwa kuliwa. Je, Waziri anaweza kutoa ushahidi wa magonjwa hayo kwa mifugo yote inayochinjwa?