Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Zaynab Matitu Vulu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. ZAYNABU M. VULU: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote namshukuru Mwenyezi Mungu kwa kuweza kuwepo leo na kuchangia hotuba ya Wizara yako.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nachukua nafasi hii kumpongeza Waziri Mheshimiwa Profesa Jumanne Maghembe, Naibu Waziri Mheshimiwa Ramo Makani na watendaji wote wa Wizara.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hoja yangu kubwa na ombi langu kwa Wizara hii ni kwamba naomba Wizara inipe majibu ni lini itaweka utaratibu wa kuzuia wananchi ambao hupata kipato chao kupitia uvuvi kwenye bwawa/mabwawa yaliyopo Selous, lakini Serikali imezuia na hata kufikia kuwaua. Hili ni tatizo naomba ufafanuzi.
Pia Mkoa wa Pwani kumezungukwa na misitu hivyo kwa wale ambao wanafanya biashara ya mbao (kutengeneza samani) hutozwa ushuru mkubwa wa shilingi 120,000 hata kama kitanda au samani ishatumika zaidi ya miaka 20. Naomba kauli ya Serikali lini itapunguza ushuru huo wa samani na mkaa? Naomba majibu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, misitu iliyopo Mkoa wa Pwani mingi imebaki vichaka kwa kuwa hakuna usimamizi mzuri na kupelekea ukataji hovyo wa miti.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Mkuranga eneo la Mwandege kuna msitu ambao kwa neno msitu kwa sasa si sahihi kwani ni kichaka na kuficha wahalifu wengi, naiomba Serikali itoe maelekezo au kubadili matumizi ya eneo hilo ili kupendezesha eneo hilo, laa kama hiyo haiwezekani basi uwepo upandaji upya wa miti na ulinzi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba maelezo ya Serikali na naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja.