Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Grace Sindato Kiwelu

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. GRACE S. KIWELU: Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo la wafugaji na wakulima na hifadhi zetu. Tatizo hili ni kubwa sana katika nchi yetu na kama hatua za dharura hazitachukuliwa tutapeleka nchi yetu kwenye umwagaji damu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimesema hayo baada ya kusikiliza michango ya Waheshimiwa Wabunge humu ukumbini. Jana michango hiyo inaligawa Taifa letu katika makundi makubwa ambao wote ni Watanzania. Mimi niiombe Serikali ichukue hatua za haraka kukaa na Wizara zake TAMISEMI, Ardhi na Maliasili kupanga maeneo kwa ajili ya wafugaji na wakulima, hii itaondoa tatizo hili kubwa, tumechoka kuona damu za Watanzania zikimwagika kila siku.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sote tunakumbuka Operesheni Tokomeza iliyofanyika katika nchi yetu na madhara yaliyopatikana katika zoezi hilo. Serikali iliunda Tume ili kuchunguza athari na Tume hii imemaliza kazi yake, je, ni lini taarifa hiyo itatoka ili Bunge lako lipate kujua Tume imebuni nini. Lakini pia liko suala la fidia kwa wananchi walioathirika katika operesheni hiyo, je, ni lini sasa fidia hiyo itatoka?
Mheshimiwa Mwenyekiti, ningependa kuishauri Wizara kutoa elimu kwa wananchi ili wajue umuhimu wa hifadhi zetu. Naamini elimu ikitolewa wananchi wetu wataelewa na watakuwa walinzi katika hifadhi zinazozunguka. Pia nitoe ushauri mwingine ili kuondoa tatizo la mipaka na vijiji vinavyozunguka hifadhi zetu ni muhimu sana wataalam wetu wanapokwenda huko kwenye maeneo washirikishe wananchi hii itaondoa migogoro iliyopo huko nimesema hayo kwa sababu wananchi wanalalamika hawashirikishwi wakati wao ni wenyeji wa maeneo hayo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Bunge lililopita tulijadili sana suala la Halmashauri zinazozunguka Mlima Kilimanjaro ambao wananchi wake pale ambapo likitokea tatizo hao ndiyo wanakuwa wa kwanza kushirikiana na hifadhi kutatua tatizo hilo. Sasa ningependa kujua ni lini Halmashauri hizo zitaanza kupokea mrabaha unaotokana na mapato ya mlima huo mzuri na wa kwanza Afrika?
Mheshimiwa Mwenyekiti, huo ndiyo mchango wangu kwa leo naomba kuwasilisha.