Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Mbaraka Kitwana Dau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. MBARAKA K. DAU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nichukue fursa hii kuanza kwa kuunga mkono hoja. Pili, kipekee nimshukuru Mheshimiwa Waziri Profesa Jumanne Maghembe na Naibu wake Engineer Ramo Makani kwa hotuba nzuri na yenye kuleta matumaini kwa Watanzania.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kwa kuishauri Serikali sikivu ya CCM kutanua wigo wa vivutio vya utalii kwa muda mrefu kumejengeka dhana kuwa utalii maana yake ni mbuga za wanyama na maeneo ya fukwe peke yake. Dhana hii si sahihi, kwani utalii una wigo mpana zaidi. Kwa mfano katika jimbo langu la Mafia (Kisiwa) kuna samaki aina ya papa mkubwa sana anaitwa Mhaleshark (Potwe) ni one of the species of shark, papa huyu ni adimu sana duniani, kwa sasa anapatikana Australia na Mafia tu dunia nzima.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa upande wa Australia ni ghrama kubwa kwa mtalii kwenda kumuona samaki huyo na moja ya sifa za whaleshark ni papa rafiki ana tabia zinazofanana na dolphin (pombuwe) mtalii anaweza kuogolea naye bila ya kupata madhara yoyote ile. Hivyo mtalii Australia anatumia gharama kubwa ikiwa ni pamoja na kukodi helikopta kwenda maeneo ya mbali sana kuogolea na papa. Lakini kwa upande wa Mafia papa huyu anaonekana umbali usiozidi mita 300 kutoka bandari kuu ya Kilindini Mafia. Ombi letu wana Mafia Serikali kupitia Bodi ya Utalii itusaidie kuutangazia ulimwengu upatikanaji na papa huyo ili kuongeza watalii wengi Mafia sambamba na maboresho ya hoteli zetu za kitalii na miundombinu ya kuingia na kutoka Mafia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ni uvunaji wa mikoko katika Kisiwa cha Mafia mwekezaji Tanspesca amewekeza kiwanda cha kamba katika kijiji cha Jimbo na kupewa kibali na Wizara ya Utalii kukata baadhi ya mikoko. Tunaiomba Wizara sehemu ya mapato yatokanayo na kukatwe kwa mikoko hiyo ibaki katika Halmashauri ili kuweza kusaidia shughuli za uhifadhi katika Kisiwa cha Mafia ikiwemo kupanda mikoko mingine kufidia ile iliyokatawa.
Suala lingine ni kukosekana kwa Afisa Utalii katika Wilaya ya Mafia. Pamoja na potential kubwa ya utalii katika Wilaya ya Mafia bado mpaka sasa hatuna Afisa wa Utalii wa kuratibu shughuli za utalii kisiwani Mafia, tunaomba Wizara kulifanyia kazi jambo hili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mara nyingine nawashukuru Waziri na timu yake yote na naunga mkono hoja. Ahsante sana.