Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Ally Mohamed Keissy

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. ALLY K. MOHAMED: Mheshimiwa Mwenyekiti, Nkasi na Mkoa wa Rukwa kwa ujumla tuna pori la akiba la ukubwa wa kilometa za mraba za 6,462.26; pori la akiba la Rukwa ukumbwa wake kilometa 4,194 na pori la Rwamfi kilometa 2,228.26 hilo pori linahujumiwa sana na majangili yaani wawindaji haramu ni kwa kuwa hilo pori la akiba limepakana na nchi jirani inakuwa vigumu sana kwa wafanyakazi wa idara kwa sababu hawana magari ya doria. Niliahidiwa kupewa gari jipya na Waziri wa Awamu ya Nne Mheshimiwa Nyalandu lakini mpaka leo sijapokea hilo gari kwa ajili ya kuokoa mali kwa ajili ya wanyama na miti. Tafadhali hilo gari ni muhimu kwa doria na pia kwa upande wa Ziwa Tanganyika, kwa hiyo, usafiri wa majini ni muhimu sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba ahadi ya aliyekuwa Waziri Mheshimiwa Nyalandu itekelezwe maana pori hilo la akiba linashambuliwa sana na wafugaji na majangili na wakata mbao. Naomba jibu kabla ya mwisho wa Bunge la bajeti kuhusu hilo gari maana ahadi ni deni na dawa ya deni ni kulipa, pori linaangamia sana sana.
Mheshimiwa Waziri gari jipya ni muhimu sana kwa ajili ya doria ya hilo pori.