Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. George Malima Lubeleje

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpwapwa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. GEORGE M. LUBELEJE: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa nakupongeza kwa hotuba yako nzuri sana yenye ufafanuzi wa masuala mbalimbali ya Wizara yako. Pili naunga mkono hoja hii kwa asilimia mia pamoja na kuunga mkono hoja hii naomba kuchangia maeneo yafuatayo:-
(i) Ufinyu wa bajeti katika Wizara hii na kusababisha kufanya Wizara kushindwa kutekeleza majukumu yake na hasa miradi mingi ya maendeleo kutokamilika kwa wakati. Fedha za miradi zitolewe za kutosha na kwa wakati.
(ii) Serikali isitegemee sana fedha za nje kwa ajili ya miradi ya maendeleo kwa kuwa hakuna uhakika kama fedha za nje zitaletwa zote au kidogo na kwa wakati gani. Fedha za ndani zitumike zaidi.
(iii) Uhaba wa watumishi wa sekta ya maliasili na utalii na hasa katika Wilaya zetu hakuna Maafisa Misitu, magari, pikipiki na baiskeli na maslahi duni.
(iv) Je, sababu gani zinazofanya idadi ya watalii kupungua?
(v) Je, ni sababu gani zinazofanya Wizara ya Maliasili na Utalii kushindwa kabisa kukabiliana na ujangili na kusababisha wanyama kama tembo, vifaru wanaoendelea kupungua katika mbuga zetu, je, hakuna mbinu za kisasa za kukabiliana na majangili kwa kuwa wanaongezeka siku hadi siku.
(vi) Serikali ijitahidi kuboresha huduma kwa watalii kama hoteli, afya, barabara na ulinzi wa watalii na viwanja vya ndege.