Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Savelina Slivanus Mwijage

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. SAVELINA S. MWIJAGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nichangie Wizara hii nikizingatia vitu muhimu sana ambavyo ni rasilimali zilizomo katika nchi hii ya Tanzania. Pamoja na kuingiza uchumi ili kuondokana na umaskini, jambo ambalo Wizara ya Maliasili na Utalii inafanya, nchi yetu ni tajiri sana kwa kuwa na vitega uchumi vya utalii. Tuna vivutio vingi sana na nchi yetu ni ya pili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tuna Serengeti, Ngorongoro, Tarangire, Momela, Mikumi, Katavi na Rubondo; tuna jiwe liko Ukerewe ambalo Serikali haijaona umuhimu wake kuipa kipaumbele ambalo Waheshimiwa Wabunge wengi wanajua maajabu makubwa sana ya hilo jiwe pamoja na Wabunge wa huko Ukerewe.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Biharamulo tuna msitu ambao kwa sasa umeingiliwa na wafugaji wengi wamevamiwa, wanashambuliwa pamoja na wachoma mkaa, hata hao wa ng‟ombe wanajifanya wafugaji, tunawaogopa sana. Wanaweza kuwa sio salama; huwezi kujua kama ni Watanzania au ni wakimbizi. Matokeo yake kuanza kuteka na kurudi kwenye pori hilo. Je, msitu mkubwa kama huo wanakula nini? Tunaomba msaada wa Serikali, hata wanyama wameanza kurudi sasa, watakaa wapi kwa style hii? Je, tuna faida gani? Kwa nini wafugaji wasitengewe wakawa na mipaka? Vijiji ambavyo viko karibu na pori hilo, shida wanavamiwa na wake zao wanabakwa, wakikuta vyakula wanakula, wanaume wanapigwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mipango ya Wizara iliyomo kwenye vitabu iwe ya kutekelezeka. Msitu huo uko kwenye Ziwa la Buligi ambalo lina maajabu makubwa sana. Limepakana Bukoba Vijijini, Biharamulo, Karagwe na Ngara.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaomba sana, tena sana, Serikali iweze kuweka mpango mkakati tuongeze kipato/ajira kwa vijana wetu. Vipo vitu vingi tu, ni mipango tu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, matangazo ya utalii wetu wa vivutio vyetu ni mdogo sana. Matangazo ya vipeperushi inafika mahali unakuta Kenya wanaongoza mbuga zetu kwa upande wao hata Mlima Kilimanjaro ni punde watasogea upande wa Kenya. Kweli tunakokwenda hili jambo mmekaa kimya, taratibu wanakuja. Hata Idd Amini alikuja hivyo hivyo kusogeza mipaka yetu ila angeingia kwenye nchi yetu, Mwalimu wetu Baba wa Taifa alipambana na Wajerumani, zimetolewa zinasogezwa matokeo yake nchi ikaingiakwenye vita. Sasa chonde chonde, Wizara iwahi mapema kusimamia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wizi wa pembe za tembo, hili suala limekuwa wimbo katika nchi hii. Ni maharamia wangapi wamefungwa? Ni kesi ngapi ambazo ziko mahakamani au zilizokwisha?
Mheshimiwa Mwenyekiti, mapato ya vivutio ni madogo sana ukilinganisha na vivutio tulivyonavyo vingi na kupata tofauti. Sisi tuna asili ya mali nyingi, hatupaswi kuwa hivyo, ni usimamizi siyo mzuri sana. Tuwe na usimamizi na mipango mikakati, tutaondokana na kutokuwa na plan za kudumaa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, miundombinu kama viwanja vya ndege vinatakiwa kuboreshwa hasa vya Musoma na Kilimanjaro (KIA). Kweli viwanja vya kuingiza wageni nchini viko hivyo na kama unavyojua wenzetu wanajali maisha yao na usalama. Miundombinu inashusha utalii. Viwanja vya mbugani vyote vya changarawe viboreshwe kwa kuwekewa lami. Sasa mvua ikinyesha wasije au?
Mheshimiwa Mwenyekiti, hoteli zetu tukiona wazungu tunapandisha bei, siyo vizuri. Naiomba hasa Serikali iingilie, ibadilike. Wizara inatengeneza sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ni ufugaji wa nyuki. Ufugaji nyuki ni ajira kubwa sana kwa vijana. Wapewe elimu wajiajiri wenyewe. Tuhamasishe vikundi vya kufuga nyuki wafuge kiutalaam zaidi. Misitu mingi ya nchi yetu inaruhusiwa kufuga nyuki, masoko ni mengi, lakini wanaofuga hawafugi kitaalam, wala hawapati elimu. Jambo hili liangaliwe au lipewe kipaumbele. Kadri tunavyochelewa kutenga bajeti ya kutosha, wakija wawekezaji watajipangia utaratibu wao.