Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Mussa Ramadhani Sima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. MUSSA R. SIMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza Waziri kwa uwasilishaji mzuri. Kwa kuwa Serikali kupitia Wizara hii ilitoa agizo la kuwauzia MPM miti kwa nusu ya bei, that is cubic meter 1 – 14,000 badala ya 28,000 tangu mwaka 2007 mpaka sasa hivi Serikali inaingia hasara isiyopungua shilingi bilioni 2.8 kila mwaka. Naomba Wizara ije na mkakati wa kuondokana na tatizo hilo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa karatasi inatengenezwa Kenya, lakini misitu iko Tanzania na bado importation ya karatasi ina punguzo la kodi la asilimia10 badala ya asilimia 25 ninaiomba Serikali ije na mpango wa kuhimiza viwanda vyetu kama MPM kutengeneza karatasi badala ya mifuko peke yake na tuongeze kodi ya importation iwe asilimia 25.