Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali katika Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Ally Abdulla Ally Saleh

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Malindi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali katika Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. ALLY SALEH ALLY: Hayupo, ndiyo maana nikaomba nafasi hiyo nichukue mimi. Hayupo Dodoma.
MWENYEKITI: Hayupo Dodoma. Umejipangia wewe mwenyewe, haya.
MHE. ALLY SALEH ALLY: Mheshimiwa Mwenyekiti, sikujipangia, nimekuletea ombi la ruksa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Ahsante. Tukitazama utekelezaji wa mpango wetu kwa muda wa miaka mitano iliyopita na hata mwaka mmoja uliopita, hatupati picha yenye kutia moyo. Ingawa umetekelezwa lakini kuna upungufu mwingi, ambapo kwa mfano kwenye umeme hatukuweza kufikia kiwango ambacho tulikuwa tumejiwekea cha zaidi ya megawati 4000. Kwenye barabara hatukuweza kufanikiwa ni chini ya asilimia 50, kwenye reli kilometa 174 au 75 zilizoweza kukarabatiwa. Pia kwenye irrigation ambapo jana kuna mtu mmoja alitoa taarifa, nilikuwa sijui kama tuna potentiality ya 20 million lakini kitu ambacho kimefanywa katika target ya milioni moja, tumefikia only 23%, pia Deni la Taifa limeongezeka katika miaka hii kutoka tisa mpaka 19.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hivyo, kama Wabunge na kama Serikali tunatakiwa tujiulize wanatupa moyo gani au wanatupa hope gani ya kuweza kutekelezwa kwa mpango huu unaokuja, wakati Mpango ambao umemalizika ulikuwa very much under-performed.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimefurahi kwamba Serikali wame-mention baadhi ya changamoto katika ukurasa wa 13 wa hotuba ya Mheshimiwa Waziri na wamekuja na solution katika ukurasa wa 14, katika baadhi ya changamoto zile imezungumziwa pia sekta binafsi kwamba ni solution mojawapo ambayo inaweza ikasaidia ikiwa suala zima la funding litafanywa kwa uhakika yaani ugharamiaji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda niiombe Serikali kwamba, wakati wakija na Mpango kamili hapo baadaye, waje na andiko ambalo litaelezea hii sekta binafsi itachangia vipi katika Mpango huo ili kuhakikisha kwamba funding inapatikana ya kutosha ndani lakini pia kutoka nje, baada ya kuwa na andiko ambalo litaonesha namna gani sekta binafsi itaweza kuchangia katika Mpango wetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia, ningependa pamoja na vile vipaumbele pale vilivyowekwa ambavyo ni vinne, ningependa suala la utawala bora lingewekwa kama mtambuka, kwa sababu tunalo tatizo kubwa la utawala bora ambalo huko mbele tutalizungumzia zaidi lakini katika hatua hii nataka niseme kwamba, sasa hivi Tanzania inadaiwa kuwa kuna suala kubwa la rushwa, inaidaiwa kwamba kuna tatizo la utekelezaji hata wa maagizo kutoka Mahakama ya Rufaa ya Tanzania, lakini pia kuna madai mbalimbali ya wananchi kunyanyaswa katika sehemu mbalimbali. Kwa hivyo, ili Mpango uwe endelevu na unaoweza kuwa wa uhakika, ningependa katika vipaumbele hivi pia suala la utawala bora lingewekwa katika umuhimu mzuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimevutiwa na Mpango wa Serikali wa kuweka katika yale mambo ya vipaumbele, kuweka miradi ya flagship, miradi ambayo hiyo itakuwa ni miradi kielelezi. Hili ni wazo zuri na ningefurahi kama katika wazo hilo katika mradi mmojawapo ambao unaweza kuwekwa au katika miradi ambayo itafikiriwa suala la Zanzibar liwe incoperative.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu mimi ni Mtanzania lakini nampigia kura Rais wa Tanzania, lakini pia kuna Wazanzibar ambao wanatumikia Serikali, sioni sababu gani Serikali ya Muungano haina specific project Zanzibar zaidi ya zile za kukagua kodi tu au za immigration ambapo kuna jengo kubwa. Hata hivyo, ningependa nione Serikali, inachangia kwa kuwa na mradi maalum (specific) ambao ni wa kutoka Zanzibar, ili Wazanzibar waone kwamba Serikali yao inawajali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hivyo katika miradi ambayo ni ya flagship, ningependa tuweke mradi, eneo letu ni dogo la ardhi, miradi ambayo inaweza ikaweka; nilisema juzi mama Waziri ulikuwepo, nilikwambia suala silicon veiling tunahimiza katika eneo lile la miradi wezeshi, habari ya TEHAMA. Ni vizuri, tukili-consider suala la silicon veiling, Tanzania ina urafiki mzuri na Bill Gates, tungeweza kutumia ushawishi wetu wa kuleta mradi kama huu wa silicon veiling ambao hauhitaji eneo kubwa sana lakini inaweza ikazalisha eneo kubwa. Mpaka sasa katika eneo letu lote la kanda hii hakuna mahali ambapo pana silicon veiling. Kwa hivyo, kwa wazo hilo ningependa tulitumie vizuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia, ningependa kuona kuwa tunatumia bahari yetu. Tuna masafa ya bahari ya kilomita 1,400 kutoka pembe mpaka pembe ya chini. Nchi kama Seychelles nchi ndogo kabisa ambayo ina watu laki moja. Ambayo ina eneo inaingia ndani ya Tanzania zaidi ya mara 2000 wao ndiyo wanaongoza duniani kwa uvuvi, wa pili kwa uvuvi wa samaki aina ya Tuna, sisi tuna bahari hapo hatujaweza kuitumia vya kutosha. Kwa hivyo hili, ningependa lifanyiwe mkazo kwa sababu tuna uwezo mkubwa sana wa kuvuna kutoka baharini. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kitu kingine ambacho ningependa tukitumie kama alama ya Tanzania ni excellence in education. Tunaweza tukajipanga vizuri, tukaweza ku-specialize katika maeneo maalum, zamani nakumbuka niliwahi kusikia, katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam masuala ya maji Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kilikuwa kina-save almost kanda yote hii hapa. Mtu yeyote akitaka kuja kusoma maji anakuja Tanzania. hata katika East Africa zamani ilikuwa kuna mgawanyiko, ukitaka kwenda kusoma kurusha ndege unakwenda Soruti, ukitaka kufanya kitu gani unakwenda sehemu gani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hivyo, ningependa hili tuli-concentrate, nchi kama ya Cyprus nimekwenda Northern Cyprus, uchumi wake mkubwa unategemea education wamejenga vyuo wame-specialize katika maeneo maalum wamejitangaza dunia nzima, wamejitangaza katika kanda mbalimbali, kwa hivyo wao wanavuna sana kutokana na suala zima la education.
Mheshimiwa Mwenyekiti, la mwisho, nataka kuzungumzia, nilisema pale nitarudia kwenye suala la utawala bora. Nataka nirudie hili la Zanzibar, kwanza nafadhaishwa sana kuona Mawaziri wetu hapa Waziri wa Mambo ya Ndani na Waziri wa Ulinzi wanakataa, wanakana kama hakuna suala la mazombi na masoksi Zanzibar, inaniumiza moyo sana. Labda kwa sababu ndugu yake, labda kwa sababu jamaa yake, au kwa nafasi yake yeye hajawahi kukutana na mazombi wakamdhuru au wakamfanyia vitu vingine. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati haya yakitokea tunakwenda katika Uchaguzi wa Zanzibar ,tunaambiwa kama unarudiwa, lakini ningependa Serikali itazame upya, itazame implication za kurudia uchaguzi huo, socially implication, 2001 siyo mbali, watu 4000 walikimbia nchi hii wakaenda Somalia. Tutazame economic implication, ikiharibika Zanzibar hakuna uchumi Bara.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jana alikuwa anazungumza mwenzangu mmoja anasema baada ya uchaguzi hapa hatuji hapa kujadili mpango, tutakuja hapa kujadili namna ya kujitoa kiuchumi. Kukiharibika Zanzibar, mtalii haji Ngorongoro, kwa sababu mtalii anaji-program kuja Ngorongoro kisha anakuja Zanzibar. Kuna security implication, ikiharibika hali ya Zanzibar hapatakuwa salama katika Tanzania, kuna stability implication, hali ya Zanzibar ikiharibika pia hapatakuwa stable hapa. Mnapotupeleka sasa hivi kama watu hawapati nafasi yao, uhuru wao, kupitia kwenye Katiba watatafuta kwa njia nyingine. Hizo njia nyingine ndiyo ambazo tunataka kuziepuka. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kingine, ni negative public relation, hivi Tanzania inajijengea sifa gani kwa dunia. Tanzania imekuwa mfano wa dunia, kwamba ni nchi ambayo inaheshimu demokrasia, ni nchi ambayo inaheshimu haki za binadamu, inaheshimu uchaguzi. Kwa nini tunalazimisha kwa Zanzibar, tulazimishe uchaguzi ambao hauna hata mantiki moja. Unarejea uchaguzi ili iwe nini, Tume ile ile, kwa maana ya marefa wale wale, ma-linesmen wale wale waliokufungisha mabao manne halafu unarudia uchaguzi ule ule, mnarudia uchaguzi ili iwe nini, tupate suluhu gani?
Mheshimiwa Mwenyekiti, nafikiri kuna haja ya Serikali kukaa kwa maana ya uchumi, kwa maana ya stability, kwa maana ya security implication, tukae chini tutazame suala la Zanzibar. Kama mnataka kumwokoa Dr. Shein awe Rais lazima utafute njia nyingine. Ahsante sana. (Makofi)