Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Venance Methusalah Mwamoto

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. VENANCE M. MWAMOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba nichangie hoja hii. Mimi ninatoka Wilaya ya Kilolo ambayo iko Mkoa wa Iringa, Hifadhi ya Udzungwa asilimia kubwa ipo katika Wilaya ya Kilolo japo Makao Makuu yapo Morogoro. Kuna vijiji ambavyo vinapakana na Udzungwa National Park. Vijiji vya Msosa, Ikula, Udekwa, Mahenge, Wotalisoli na kadhalika kuna tatizo kubwa la mamba, tembo hasa katika kijiji cha Msosa. Kwa sababu maji ya Mto Lukosi ndiyo yanayosababisha wananchi wengi kuliwa na mamba na pia kuuliwa na tembo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ombi:-
(1) Tunaomba Wizara iangalie utaratibu wa kujenga post (Kituo cha ulinzi wa vijiji vile pale Msosa), kujenga miundombinu ya maji yaani tanki la maji na kusambaza kijiji kile ili kupunguza ajali za mamba.
(2) Ujenzi wa barabara ya kutoka kijiji cha Mahenge kwenda Udekwa, kilometa 25 tu.
(3) Kuna mapango makubwa katika kijiji cha Udekwa ambayo ni kivutio kwa watalii wa ndani na nje, ningeomba wataalam wafike waone.
(4) Kutelekezwa kwa kivutio cha Kalenga, sehemu ambayo kichwa cha Mkwawa kimehifadhiwa, familia ya Mkwawa wanalalamika na kuna uwezekano mkubwa wa kuomba kukizika kichwa kile.