Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Khadija Hassan Aboud

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. KHADIJA HASSAN ABOUD: Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza Mheshimiwa Waziri kwa juhudi zake za kuhakikisha Wizara inatekeleza majukumu yake kama inavyotarajiwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu utalii naishauri Wizara iweke mkakati madhubuti katika kudhibiti mapato yatokanayo na utalii. Watalii wanaotembelea Tanzania walipie hapa nchini kuepusha upotevu wa mapato. Elimu na matangazo juu ya vivutio vya utalii vilivyopo nchini ipewe kipaumbele ili kuongeza idadi ya watalii kuitembelea Tanzania.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu misitu, upandaji wa miti uwe mara mbili zaidi ya miti inayokatwa. Nishati mbadala ya kupikia itasaidia kupunguza matumizi ya mkaa ambapo itasaidia kupunguza miti kuchomwa kwa kutengeneza mkaa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, usafirishaji wa mbao nje ya nchi udhibitiwe zaidi pamoja na kupunguza kiwango cha mbao zinazosafirishwa nje ya nchi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vibali vya ukataji na uvunaji miti katika mashamba ya miti, kwa mfano SAO Hill na kwingineko upatikanaji wake ni wa shida sana, hata muombaji aliyetimiza masharti yote. Kuna upendeleo na wanyonge ni shida sana kupata vibali hivyo. Nashauri upangwe utaratibu mzuri katika utoaji vibali vya uvunaji miti.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante na nawatakia kazi njema.