Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. ELIAS J. KWANDIKWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo la malisho katika Jimbo la Ushetu, napenda kushauri na kuomba Wizara iturejeshee msitu wa Usumbwa uliochukuliwa na Serikali mwaka 2002 ili wananchi wapate sehemu ya malisho na kushiriki kikamilifu kuhifadhi Mbuga ya Kigosi-Moyowosi. Ushetu tumeanza kutoa hamasa ya wananchi kushiriki katika hifadhi kwa kutozana faini za kimila ili kuzuia uharibifu, shida yetu ni eneo la malisho.
Pili niombe na kushauri tupewe eneo la msitu wa akiba wa Ushetu/Ubagwe ili tupate eneo la malisho.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ushirikiano; naomba sana Wizara itoe ushirikiano kwa wananchi na Wabunge wanaopakana na hifadhi, mashirika mbalimbali ikiwemo ya dini, vikundi na uongozi wa kimila ili tuzungumze namna bora ya kutatua migogoro katika maeneo yetu baina ya wahifadhi na wananchi ama wafugaji.