Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Oliver Daniel Semuguruka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa naunga mkono hoja asilimia mia moja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna matatizo mengi kwa wananchi hasa wakazi wa maeneo ya karibu na hifadhi. Wananchi wanataka kulima na kufuga, maeneo wanayoishi yamejaa, hayawatoshi. Wanaona kuna eneo jirani miaka yote lipo wazi na lina rutuba nzuri ya kilimo, wanaingia kulima na kufuga, wanakamatwa na kufunguliwa mashtaka ya uvamizi wa Hifadhi ya Taifa. Nini maana ya neno hifadhi ya Taifa maana isijekuwa inatumika sivyo. Hifadhi haina zuio lolote la mipaka inayojulikana kwa kijiji ikiwamo vibao vya kutambulisha hifadhi au fence.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hifadhi haina hata wanayamapori; kama ni hifadhi ya ardhi kwa wananchi kuitumia baadae basi ijulikane ni kwa matumizi yapi na hiyo baadae labda ndio imefika sasa kwa maana hifadhi nyingi za aina hiyo zimetengwa tokea ukoloni na zingine ni zaidi ya miaka 40. Je, Serikali ina mipango gani ya kutambulisha maeneo ya uhalisia wa leo na mwaka ulioanza kuwa hifadhi?
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu utalii; utalii unajulikana kwa matangazo. Tanzania ni nchi ya pili duniani kwa vivutio vya utalii ya kwanza ikiwa ni Brazil, lakini ni nchi inayopata watalii wachache sana kulinganisha na nchi zenye vivutio vichache. Watalii milioni moja tu wakati vivutio kibao, amani na utulivu inakuwaje nchi kama Misri yenye tatizo la usalama inapata watalii zaidi ya milioni ishirini kwa mwaka? Nchi kama Mauritania yenye vivutio vichache mno nayo inatushinda? Je, Wizara kweli inafanya matangazo? Makampuni ya utalii yanajihusishaje na kuuza utalii? Tunayo kweli makampuni ya utali maarufu ya kimataifa? Tunahitaji kuona utalii ukitangazwa kila kona.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Shirika la Ndege ni zao kubwa la utalii. ATCL haipo Kimataifa; ni nini mipango ya Serikali kufanya biashara ya utalii na ATCL kwa makampuni ya utalii kuwa na hisa ATCL? Ushauri wangu kwa Wizara ni kuhamasisha bidhaa za Tanzania hasa kazi za mikono kuuzwa kwenye maduka ya airports kubwa kama London - Heathrow, Schiphol - Amsterdam, Frankfurt - German na kadhalika. Jina Tanzania lionekane kila sehemu, linakuza hamu ya watu kuja kufanya utalii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia unaweza kufanya mikakati ya kuandaa vijana 100 kwenye miji mikubwa yenye watalii na kumvalisha nguo zenye maandishi ya Tanzania huku wakishikilia mabango na kuzunguka mitaani. Vijana hao wanalipwa ujira mdogo tu. Wizara ihakikishe jina Tanzania linasikika kila kona ya dunia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kodi zinazotozwa kwenye hotels za kitalii ni kubwa au ni hotels zenyewe maana hotels ni ghali sana ikiwemo chakula. Watalii wengi wanaokuja nchini ni wale ambao wamejibana kwa muda mrefu hivyo kutokuwa na pesa nyingi kutosheleza matumizi makubwa. Tuweke bei nafuu kuvutia watalii kuja nchini kwetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.