Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2015, Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Doto Mashaka Biteko

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukombe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2015, Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. DOTO M. BITEKO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa nafasi hii, na mimi nichangie Bajeti Kuu ya Serikali. Kabla ya kufanya hivyo, naomba tena nimshukuru Mungu kwa nafasi hii, ambaye amenipa uhai niweze kusimama tena mbele yako ili niweze kusema machache.
Mheshimiwa Naibu Spika, nikupongeze sana wewe binafsi kwa namna unavyoliendesha Bunge letu. Wewe umekuwa kamanda wa makamanda; tumeona hapa makamanda wanakukimbia kila ukitokea; na hiki ni kiashiria kwamba wewe hutishiki, uko imara. Na mimi nakuhakikishia tu kwamba sisi Wabunge wenye nia njema tuko pamoja na wewe. Endelea kutuongoza kwa kufuata kanuni zetu na taratibu tulizojiwekea, bila shaka na Mungu atakubariki. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nampongeza sana Mheshimiwa Waziri kwa bajeti aliyoiwasilisha. Bajeti hii bila shaka inatutatulia changamoto nyingi, lakini yako mambo ambayo nadhani yanahitaji kuboreshwa kidogo; na kwa maoni yangu ndiyo haya yaliyonifanya nisimame. Nianze na sekta ya elimu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, sekta ya elimu imetengewa jumla ya bajeti ya shilingi trilioni 4.8 na unafahamu kwamba kwenye Azimio la Dakar tulikubaliana kwamba kila nchi itenge 6% ya GDP yake ipelekwe kwenye elimu. Ukiangalia hapa, pesa ambazo tunapeleka kwenye elimu shilingi trilioni 4.8, fedha nyingi kati ya hizo tumesema, zinazokwenda kwenye maendeleo ni shilingi bilioni 897.7 na shilingi bilioni 427.6 zinakwenda kwenye matumizi mengineyo. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, fedha hizi za maendeleo zilizotengwa; 50% yake inakwenda kwenye mikopo ya wanafunzi. Kwa maoni yangu naona inaondoa dhana ya maendeleo, inaingia kwenye dhana ya matumizi mengineyo. Na mimi ninadhani, hizi fedha ambazo zimepekwa kwa ajili ya mikopo ya wanafunzi, zilipaswa zitoke kwenye kifungu cha maendeleo zije kwenye kifungu cha matumizi kwa sababu zenyewe zinakwenda kutumika kwa ajili ya kuwapatia mikopo wanafunzi. Namwomba sana Mheshimiwa Waziri aje atueleze kwa nini fedha hizi zinapelekwa kwenye maendeleo badala ya matumizi? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, tumezungumza miaka mingi, na mimi kabla sijawa Mbunge nilikuwa nafutailia Bunge hili. Kwa muda mrefu tumekuwa tukihangaika na kuifanya Idara ya Ukaguzi kuwa Wakala wa Ukaguzi wa Elimu Tanzania. Elimu ya Tanzania hii dawa yale iko kwenye ukaguzi; elimu ya Tanzania ili iwe bora lazima kuwe na mtu ambaye anaiangalia kila siku. Idara ya Ukaguzi ambayo iko chini ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, leo Sayansi na Teknolojia; fedha inayopewa ni kidogo sana. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nenda kila kona ukaangalie, Idara ya Ukaguzi wana hali mbaya ya kifedha. Magari yao hata matairi hayana; magari yao hata mafuta hayana; uwezo wa kukagua kwa maana ya capacity ya wafanyakazi ni kidogo. Leo kwenye bajeti hii ukaguzi wametengewa 20% peke yake; fedha hizi ni kidogo sana. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, tulikuwa tunadhani kwamba tunapiga hatua, tunakwenda mbele kwa kuifanya Idara hii kuwa Wakala Maalum wa Ukaguzi wa Elimu nchini ili quality assurance tunayoizungumza kila mara iweze kuwa na uhakika zaidi, lakini leo ninaona tunarudi nyuma badala ya kwenda mbele. Naomba sana Idara hii iangaliwe, wafanyakazi wake, miundombinu pamoja na vitendea kazi, wapatiwe ili tuweze kukagua elimu ya nchi hii. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo lingine ambalo nataka nilizungumzie ni kilimo. Kilimo kimetengewa shilingi trilioni 1.6 na kimebeba 4.9% ya Bajeti yote ya Serikali ukiondoa madeni. Mwaka wa 2014 walikopesha matrekta 118; mwaka 2015 wamekopesha matrekta 74 peke yake na mwaka huu tunarudi nyuma tena. Tulikuwa tunaamini kwamba kilimo ndiyo sekta ambayo inaajiri Watanzania wengi zaidi, tulipaswa kuweka nguvu zaidi pale kuliko kuiangalia kwa namna ambayo tunaiangalia hivi sasa. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nataka nikwambie mwaka huu wa kilimo na msimu huu wakulima wa pamba hawana habari njema wanayoielezea. Mbegu waliyopewa haijaota. Nenda Bukombe pale, wakulima wanalalamika mbegu waliyopewa 73% tu ndiyo iliyoota, haikuota. Wamepewa dawa za kuua wadudu, hazikuua wadudu, lakini wakulima hawa hawana namna ya kufidiwa. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba Bunge hili tuiombe Serikali, wakulima ambao walipelekewa dawa ambazo hazikuua wadudu, wakulima ambao walipelekewa mbegu ambazo hazikuota, Serikali ije na commitment ya kuwafidia watu hawa kwa sababu, wametumia nguvu kubwa kuwekeza pale; na kilimo hiki ni mara moja baada ya mwaka mmoja. Tusipowapa kifuta machozi watu hawa, nataka nikuhakikishie mwaka mzima watu hawa watakuwa maskini kwa sababu kile wanachokitarajia hawatakipata. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nataka nizungumzie vilevile kwenye eneo la wachimbaji wadogo wadogo. Wilaya yetu ya Bukombe na Mkoa wa Geita, kama unavyofahamu, ni Mkoa ambao una dhahabu nyingi. Uchumi wa Geita unategemea dhahabu na ndiyo maana hata Mheshimiwa Serukamba alivyosema katika mikoa maskini, indicators au vigezo walivyovitumia kuifanya Geita kuwa mkoa wa pili kwa umaskini Tanzania hata mimi ilikuwa inanisumbua.
Mheshimiwa Naibu Spika, nakuomba sana na Mheshimiwa Waziri wa Fedha, fedha za ruzuku kwa ajili ya wachimbaji wadogo wadogo tuzipeleke. Shilingi milioni 900 hizi tulizozitenga zisiishie kwenye makaratasi, ziende kwenye reality, tuwapalekee wachimbaji wetu wadogo wadogo waweze kuchimba kisasa ili waweze kujikwamua kiuchumi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, wananchi wa Geita vijana wengi uchumi wao na hasa wa Bukombe, wanategemea uchimbaji wa dhahabu. Ukienda huko kila mmoja anakuuliza ni lini mnatuletea maeneo? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nimemsikia Mheshimiwa Naibu Waziri anasema kuanzia mwezi wa saba. Ninaomba mwezi wa Saba iwe kweli, wachimbaji wadogo wadogo waanze kuchimba. Tusianze tena kuambiwa bado tuko kwenye michakato. Jamani wamesubiri michakato muda mrefu, sasa hivi wanahitaji kuona matokeo ya kuchimba na wanapatiwa eneo. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nizungumzie kidogo ufugaji wa nyuki. Ufugaji wa nyuki ni eneo ambalo kwa Wilaya ya Bukombe limeajiri Watanzania wengi sana. Wako watu zaidi ya 6,000 wameajiriwa kwenye sekta ya ufugaji wa nyuki, lakini watu hao hawana mtu wa kuwasaidia, wanafanya kwa mizinga ya kienyeji. Nimeangalia takwimu kwenye Hali ya Uchumi wa nchi, kuanzia mwaka 2010 sekta ya ufugaji wa nyuki inashuka. Mwaka 2010 tani 428 tu; mwaka 2011 tukashuka, tukavuna tani 343; mwaka 2012 tukashuka, tukavuna tani 103; mwaka 2013 tukashuka, tukavuna tani 83.
Mheshimiwa Naibu Spika, wafuga nyuki hawa wakipewa fedha kidogo tu kwa ajili ya kuwa na mizinga ya kisasa, kwa ajili ya kufuga nyuki kwa namna ya kisasa, nataka nikuhakikishie, inatoa ajira kubwa sana kwa Watanzania na hasa wananchi wa Bukombe.
Mheshimiwa Naibu Spika, ukienda Uyovu, ukienda Namonge, kule kote wananchi wa kule wanategemea ufugaji wa nyuki ili waweze kupata mapato yao. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nakuomba sana, mazingira haya wezeshi tuyafanye kote. Nchi yetu, amezungumza Mheshimiwa Waziri wa Fedha kwenye bajeti yake kwamba kazi tuliyonayo sasa hivi ni kutengeneza mazingira wezeshi ya wawekezaji. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nilikuwa nasoma kwenye taarifa moja ya urahisi wa kufanya biashara duniani; nchi yetu ni ya 139 kwa urasimu. Ukitaka kufungua biashara Tanzania, unahitaji siku siyo chini ya 19 ili uweze kufungua biashara. Mazingira haya ambayo siyo wezeshi hayawezi kuwavutia wawekezaji. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nimeangalia vilevile kwenye compliance, hivi tunawalindaje wawekezaji kama nchi? Nchi yetu ni nchi ya 64. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nafahamu tuna kazi kubwa ya kufanya, namwomba Mheshimiwa Waziri wa Fedha arekebishe haya, tuweze kuwasaidia Watanzania…

NAIBU SPIKA: Ahsante.