Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Livingstone Joseph Lusinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtera

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la kwanza kabisa nimshukuru Mungu kwa kunipa nafasi na kunijalia zawadi ya uhai ili niweze kusimama kwenye Bunge lako Tukufu niweze kutoa mchango wangu kwa Wizara hii ya Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Kikanda. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la kwanza hii ni kwa ajili kuweka rekodi vizuri tu, nataka nichukue nafasi hii kuwapongeza sana wananchi wa Iringa na hasa makanda wa Chama cha Mapinduzi wa pale Iringa Mjini. Kumbe walifanya kazi nzuri sana ya kumkaba mpinzani wao mpaka leo anaonesha kwenye Bunge hili kwamba ushindi wake ni ajabu sana hakuutegemea. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ukisoma taarifa hii ya Kambi Rasmi ya Upindani, unaona kuna vitu vimeandikwa kijinga kabisa. Moja ya kitu kulichoandikwa kijinga neno Mungu anaandikwa kwa herufi ndogo mimi sijawahi kuona mahali popote pale, ukitaka kutaja Mungu lazima uandike kwa herufi kubwa. Kwa hiyo, uchungaji wa Msigwa unanitia mashaka makubwa sana. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kwa kuzungumzia Chuo cha Diplomasia. Chuo cha Diplomasia ni chuo kinachofanya kazi kubwa sana ya kuwaelimisha, kuwafundisha, watu, wananchi wanaoteuliwa kuwa mabalozi, wake wa viongozi, Wakuu wa Nchi, ili kuweza kujua diplomasia inafanyaje kazi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, niiombe Serikali itenge fedha ya kutosha kwa chuo hiki ili kiweze kufanyakazi yake kwa ufanisi na nimuombe Waziri atakaposimama hapa kutoa majibu atueleze ni fedha kiasi gani zimetengwa kwa ajili ya chuo hiki ili kiweze kufanya kazi yake kwa ufanisi.
Tunasemwa maneno mabaya lakini tunavumilia mpaka wasemaji wamalize, lakini sisi tukitaka kujibu kidogo unasikia kelele za kuwashwa washwa upande wa pili. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka niseme moja ya diplomasia kubwa iliyojengwa katika nchi yetu ni kuwa na upinzani japo kwamba upinzani wenyewe ni dhaifu. Tunao upinzani lakini ni dhaifu hata kwenye kujenga hoja. Mtu anasimama hapa kuzungumzia habari ya Mabalozi hawafanyi kazi, anasimama hapa kuzungumzia habari ya Rais haendi nje. Tulikuwa na Rais Kikwete, anasafiri kila siku. Hawa walisimama Bungeni hapa kusema kwamba Rais anasafiri sana, Rais anatumia fedha nyingi, leo tumempata Dkt. Magufuli, Rais anabana matumizi, fedha zinaelekezwa kwenye maendeleo, hawa wanasimama kupinga, watu gani hawa. (Makofi/Vigelele)
Mheshimiwa Mwenyekiti, wanataka tufanye nini, leo nataka niwaambie ndugu zangu kweli kazi kubwa ya upinzani ni kupinga lakini sio huu, huu ni upinzani hewa kwa sababu hakuna wanachopinga, wao wenyewe wanaingia wanasaini wanaondoka bila kufanya kazi, leo hii wanataka kusema kwamba nchi hii haina demokrasia wangekuwepo hawa? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, leo upinzani wa Tanzania naufananisha kama mtoto mchanga tumboni. Mtoto mchanga tumboni haelewi ukubwa wa dunia. Kwa hiyo, anafikiria eneo la tumbo la mama yake ni eneo kubwa linalostahili hata kucheza. Hajui kwamba akitoka duniani kuna eneo kubwa mno, kuna eneo la kukimbia atachoka, kuna eneo la kucheza atachoka, kuna eneo la kulima atachoka, kuna eneo la kutembea atachoka. Hawa wanafikiria kama mtoto mchanga tumboni anayefikiria eneo la tumbo ni eneo kubwa sana. Leo unamkosoa Balozi eti kwamba tunao Mabalozi wenye hadhi ya nyumba kumi, haya ni matusi wa Mabalozi wetu. Mabalozi wetu ni Mabalozi waliochunjwa, wameiva, ukiwepo Balozi Mahiga, nani asiyejua kwamba Mahiga ni moja ya watu waliobobea katika masuala ya kidiplomasia ya kimataifa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, leo hii wanasimama hapa kutuambia as if kwamba sisi ni watoto wadogo. Hivi ingekuwa Watanzania wote au viongozi wote wa nchi hii wanatakiwa kusafiri nje ya nchi kwenda kuwasilisha masuala ya nchi hii wao wangekuwa Wabunge hapa. Si kila mwananchi wa Jimbo lao angekuja hapa Bungeni. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, haiwezekani wananchi wote kuja kwenye jengo hili ndio maana tumekuchagua Msigwa, ndio maana tumekuchagua Januari, ndio maana umechaguliwa Lusinde, kwa sababu wana nchi wa Jimbo zima hawawezi kuhudhuria katika kikao hiki. Sasa leo wanataka nchi nzima kila mtu akajiwakilishe kule, katika kimataifa aende akazungumzie matatizo ya nchi, haiwezekani ndio maana kuna Mabalozi wameteuliwa. Jifunzeni ninyi! Kwa hiyo, nataka niwaambie, anazungumza pale mwisho, anasema nchi ya kifisadi kama hii wakati fisadi mkuu mnaye nyie. (Makofi/Vigelele)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunao upinzani ambao unachosema haukielewi, wanachopinga hawakielewi, walichosema mwaka jana mwaka huu wanakuja wanajijibu. Walichokataa mwaka juzi, mwaka huu wanakuja wanakikubali. Nataka nimpongeze Rais Magufuli, amewafanya wapinzani wa nchi hii hawana hoja, ndio maana mnawaona wakisimama humu hakuna lolote la msingi wanalolisema. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Dkt. Magufuli, amewafanya wapinzani wa nchi hii hawana hoja ya msingi, sasa imekuwa moto ukiwaka wanatoka nje ya Bunge, daladala ikiungua wanatoka nje ya Bunge kwa sababu hoja ya msingi hawana maana Rais anafanya kazi vizuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nikuhakikishe Rais akienda kwa speed hii kufika mwaka 2020 hawa watakuwa hawapo ndani ya Bunge hili. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tutaitumia diplomasia ya nje kuhakikisha kwamba nchi hiii inapata uchumi mkubwa utakaowafanya wananchi wanufaike, na utakaowafanya wapinzani wa nchi hii waondolewe na wananchi kwenye Bunge.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nikuhakikishie, nina uzoefu wa kuongeza na hawa, nina uzoefu nao, unapowaona wanapiga kelele jua sindano zinaingia ndio maana unaona wanapiga kelele. Huwezi ukasimama kwenye Bunge hili ukiita Tanzania ni nchi ya kifisadi wakati fisadi mkuu mmemchukua, na itafika mahali nataka nikuambie, hata Mheshimiwa Mahiga hawa wakubeze vipi, siku ukijiunga kwao utakuwa mgombea Urais wa chama hicho, za kwao hawa ni kuokoteza tu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, namtia moyo Mheshimiwa Waziri na Naibu wako, Katibu Mkuu na Mabalozi wote wakilisheni nchi kama Rais alivyowaamini, watanzania tunawaamini, na ndio maana tuko nyuma yenu tunawaunga mkono.Chapeni kazi na hiyo kazi italeta manufaa hata kwenye Majimbo ya hawa wanaopiga kelele leo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nikuhakikishie, nina uzoefu wa kuongeza na hawa, nina uzoefu nao, unapowaona wanapiga kelele jua sindano zinaingia ndio maana unaona wanapiga kelele. Huwezi ukasimama kwenye Bunge hili ukiita Tanzania ni nchi ya kifisadi wakati fisadi mkuu mmemchukua, na itafika mahali nataka nikuambie, hata Mheshimiwa Mahiga hawa wakubeze vipi, siku ukijiunga kwao utakuwa mgombea Urais wa chama hicho, za kwao hawa ni kuokoteza tu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, namtia moyo Mheshimiwa Waziri na Naibu wako, Katibu Mkuu na Mabalozi wote wakilisheni nchi kama Rais alivyowaamini, watanzania tunawaamini, na ndio maana tuko nyuma yenu tunawaunga mkono.Chapeni kazi na hiyo kazi italeta manufaa hata kwenye Majimbo ya hawa wanaopiga kelele leo.