Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Joseph Kasheku Musukuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi niweze kuchangia hotuba ya mambo ya nje.
Kwanza nianze kwa kumpa taarifa tu kidogo mzungumzaji aliyemaliza kwa kutambua umuhimu wa Wabunge makini wa CCM wageni…
MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi niweze kuchangia hotuba ya mambo ya nje.
Kwanza nianze kwa kumpa taarifa tu kidogo mzungumzaji aliyemaliza kwa kutambua umuhimu wa Wabunge makini wa CCM wageni…
tunategemea kwenda kuomba Marekani, ameingia kigogo hataki kwenda Marekani mnamlazimisha kusafiri, hela zipo hapa hapa. Na nataka niwaambie ninyi ndio makuwadi wa wezi wa hela za Tanzania na mtabanwa mpaka mtaeleweka tu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pia umezungumza ukasema kwamba kuna watu wanapewa Ubalozi kama shukrani, huko kwenu huko watu wamepewa Ubunge kama shukrani hawajawahi kusimama hata kwenye jukwaa mbona husemi? Mbona husemi kwamba kwenu kuna watu wameokotwa hawajui hata CHADEMA ikoje wamepewa Ubunge; wewe umetoa mapovu miaka mitano umekuja kupambana Jimboni kuna watu wamepewa bure kule, hebu bisheni tuwataje. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, hawa tumewazoea hawana jipya, watu hawa wanatuchonganisha na Mabalozi; wanasema Mabalozi wetu ni sawa na Mabalozi wa Nyumba Kumi…
Ngojeni mje muugue mkienda India ndio mtajua…
Tuna Mabalozi waliosoma wala hawakupewa shukrani, achana na taarifa Mzee acha nimalize…
Mheshimiwa Mwenyekiti, huyu ni mwenzetu pengine anataka kuniongezea nondo…
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninachotaka kusema Mheshimiwa Msigwa ili utambue…
Kama ni muongo anasema Wabunge wa East Africa hawapewi mikopo ya magari sijui…
MWENYEKITI: Mheshimiwa Musukuma naomba ukae.
Taarifa...
MHE. JOSEPH K MUSUKUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nimeipokea, Mheshimiwa lakini message imeenda. Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Msigwa amesema Wabunge wetu wa East Africa hawapewi magari, pengine hana kumbukumbu sahihi na aliwataja nilitaka wangekuwepo pale wakamdhihirishia Wabunge hawa wa East Africa wanapewa mikopo ya magari kama tunavyopewa sisi na wana exemption ya magari mawili na ndio maana gari zao zinaandikwa namba za Ubalozi, wewe msomi gani huelewi?
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninarudia kusema kwamba kwa hali ilivyo Serikali ya Mheshimiwa Dkt. Magufuli ilivyojipanga hawa hawana cha kusema zaidi ya kutoka nje. Na mnasema kila anaposimama Mheshimiwa Dkt. Tulia, Mheshimiwa Naibu Spika mtatoka nje, tokeni; kama mlizoea Spika ambaye hafuati kanuni mlizitunga wenyewe wenyeji sisi wengine ni wageni. Tunakuomba Mheshimiwa Naibu Spika simamia Kanuni hawa watoke nje; tunawataka watoke nje kila siku tena ukae asubuhi tu kile kipindi cha live wafyatuke wakae wenyewe humu ndani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sina mengi naomba kuishia hapo.