Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Amb. Adadi Mohamed Rajabu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muheza

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kupata nafasi hii, kuchangia hoja hii ya Mambo ya Nchi za Nje. Nashukuru sana kwa sababu Wizara hii ni Wizara ambayo ni muhimu sana, Wizara ambayo inatuunganisha na mambo yetu huko nje.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ningependa tu kukuhakikishia kwamba Mabalozi ambao wako nje, Mabalozi ambao wameteuliwa na Mheshimiwa Rais huko nje wanafanyakazi nzuri sana. Wanafanya kazi nzuri na wanajenga, wanatoa sifa kubwa kwa nchi yetu ya Tanzania. Sisi ambao tumekuwa Mabalozi huko nje tunaelewa uthamini ambao tulikuwa tunapewa, heshima ambayo tulikuwa tunaipata huko nje na consultation nyingi nchi ya Tanzania, Mabalozi ambao wako nje walikuwa wanakuwa consulted kwa ushauri na kwa kila kitu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimemshangaa sana Mheshimiwa Waziri Kivuli, anapotupiga critic na kutulinganisha na Wajumbe wa Nyumba Kumi Kumi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kweli unaweza ukanilinganisha mimi na Mjumbe wa Nyuma Kumi Kumi? Unaweza kumlinganisha Balozi Mahiga na Mjumbe wa Nyumba Kumi Kumi, amekuwa Balozi wetu kwenye Umoja wa Mataifa kwa miaka kemkem mpaka Katibu Mkuu mwenyewe Ban Ki –Moon, akasema kwamba, hapana wewe umefanya kazi nzuri akampa kazi Somalia. (Kicheko/Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nimekuwa Balozi na kiongozi wa Mabalozi Zimbambwe kwa miaka chungu nzima, Mheshimiwa Msigwa unaweza kusema hivyo kweli? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, na mimi Mheshimiwa Msigwa nilikuonya nikakwambia kwamba, ushauri ambao tunakupa kwenye Kamati, usiuchukuwe ushauri huo ukaugeuza kwamba ndiyo critic na ndiyo ulichokifanya hicho. (Makofi/ Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri mwingi ambao umeuzungumza hapa ni ushauri ambao tumeupa Wizara kwamba vitu gani muhimu ambavyo wanatakiwa kuvifanya. Sasa yeye kazigeuza kwamba ndiyo critic, ndiyo madongo ya Wizara, hapana hivyo, hatuendi hivyo Mheshimiwa Msigwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninachotaka kusema ni kwamba, kazi ambayo wanafanyika huko ni kubwa na heshima ambayo tunaipata huko nje ni kubwa na Mabalozi hawa msiwakatishe tamaa, wanafanya kazi nzuri sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiangalia diplomasia ya uchumi, wameleta wawekezaji chungu nzima hapa. Mimi mwenyewe nimeshaleta wawekezaji chungu nzima hapa, wamekuza biashara chungu nzima na nchi yetu na nchi za nje. Jamani tusiwakatishe tamaa, tuzidi kuwaunga mkono, Mabalozi hawa kazi wanayofanya ni kubwa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunachokisema sasa hivi, Foreign Policy ya kwetu inabidi ibadilike kwamba zamani foreign policy ilikuwa politically, inakwenda politically, lakini sasa hivi ni lazima twende na hali halisi inavyokwenda duniani. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, na tumeishauri Wizara kwamba, ni lazima waangalie wanapoanzisha Balozi sasa hivi waanzishe balozi sio politically, waangalie kwamba tunaweza kufaidika vipi kiuchumi na ndiyo maana sasa hivi unakuta kwamba Balozi wana mipango, ambayo tumeshauri, sisi tumeishauri Kamati kwamba ni lazima wahakikishe kwamba wanaanzisha Balozi kwenye zile nchi, ambazo wanaona kwamba tunaweza kupata wawekezaji, kukuza biashara zetu na tunaweza pia kuleta watalii wengi hapa nchini. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, na ndiyo maana sasa hivi Wizara ina malengo makubwa sana ya kuanzisha ubalozi kule Uturuki, Qatar, South Korea na sehemu nyingine nyingi. Kwa hiyo, ni suala ambalo tunatakiwa tuwaunge mkono na tuhakikishe kwamba, wanapata fedha za kutosha kwa sababu diplomasia…. aaha!
Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja, ahsante sana.