Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Khatib Said Haji

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Konde

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. KHATIB SAID HAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Nikuelezee tu kwamba moyo wangu unasikia burudani sana unapokaa kwenye Kiti hicho. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza namshukuru Mwenyezi Mungu sana kunijalia na mimi leo kusema hapa. Pia nataka nimwombee dua zaidi kiongozi wetu wa Chama cha Wananchi CUF, Katibu Mkuu, Seif Sharif Hamad kwa majaribu anayokumbana nayo Wazanzibari na Watanzania wapenda haki wako sambamba na yeye. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kwa kusema kila aliaye anashika kichwa chake, hashiki kichwa cha mwenzie. Tarehe 25 Julai, kama sikosei, mwaka 2011, nilisimama kwenye Bunge hili wakati huo ikiwa Wizara ya Afrika Mashariki nikilalamikia kitendo cha Jamhuri ya Kenya wanachowafanyia wananchi wetu wa Zanzibar wanaokuwepo Kenya wakishiriki katika shughuli za kujitafutia rizki kupitia njia ya uvuvi. Nililalamika hilo na Waziri aliyekuwepo wakati ule alifuatilia kiasi chake mambo yale yalitulia kwa kiasi lakini katika miaka ya karibuni masuala ya askari wa Kenya kuwakamata wavuvi kutoka Kisiwani Pemba kule Kenya ni suala ambalo linaonekana ni jambo la kawaida. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, yamekuwa yakitokea, hivi karibuni tu, nadhani miezi mitatu iliyopita, wananchi karibu 100 kutoka Visiwa vya Pemba, wengi wao wakitoka katika majimbo yetu ya Kaskazini, Wilaya ya Micheweni, Wete walishikiliwa pale na sababu za msingi za kuwashikilia watu wale hawana, tumekuwa tukilalamika sana. Balozi wetu wa Kenya, Balozi mdogo aliyeko Mombasa amekuwa akifuatilia mambo haya na wakati mwingine amekuwa akiambiwa hakuna hasa shtaka la kuwashtaki watu wale badala yake wanapigwa faini ambazo kwa bahati mbaya sana tunalazimika Wabunge sisi kutoka Zanzibar hasa kutoka Pemba, tuchangishane mifukoni mwetu kwenda kuwagomboa watu wale kwa kuwalipia faini kubwa sana, haya mambo hayafai. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Zanzibar tuko kwenye Muungano, hatuna Wizara wala hatuna utetezi wa moja kwa moja, lazima tupitie kwenu. Mliyafanya, mnayaweza lazima muyaweze. Kule Zanzibar asilimia 90 ya watandika vitanda kwenye hoteli za kitalii ni Wakenya, wala hawanyanyaswi. Kwa nini Wapemba wanapata tabu katika Jamhuri ya Kenya? Naomba sana, Mheshimiwa Waziri akija atuambie tumekosea nini, wavuvi wetu wanapokuwa katika Jamhuri ya Kenya wanapata matatizo makubwa na yanajirudia kila mwaka. Hili haliwezekani na hatutakubali. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lazima tufike mahali tuseme kunyanyasiwa watu wetu imetosha, raia wa Tanzania ana thamani sana. Kwa hiyo, kuwaacha Wazanzibari ambao sasa ni Watanzania wakiendelea kuteseka na Balozi yupo, Mheshimiwa Waziri afuatilie jambo hili, linatukera sana. Kama wameshindwa wafikirie upya Zanzibar kuwa mwanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki waone tutakavyotetea haki zetu kule. Hilo la kwanza. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, nataka nizungumzie suala lingine la mahusiano. Tanzania imezuka aibu sana hasa kwa viongozi na watu wanaosimamia usalama wa nchi hii. Jambo dogo ugaidi, kuna ugaidi, kuna magaidi Amboni, kuna ugaidi Zanzibar, hii hatujengi! Neno ugaidi ukilitaja kwa watu wengine huko macho yao yanakaa hivi. Leo pale Zanzibar imetajwa ni kisiwa ambapo kuna magaidi yako mahakamani wakati hakuna tendo la ugaidi ambalo limewahi kufanyika Zanzibar, kama lipo litajeni!
MHE. KHATIB SAID HAJI: Sio sifa kutaja ugaidi wakati hakuna ugaidi.