Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Emmanuel Papian John

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiteto

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. EMMANUEL J. PAPIAN: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi. Kwanza nampongeza Waziri mwenye dhamana na Mambo ya Nchi za Nje, Mheshimiwa Mahiga kwa kazi nzuri anayoifanya. Pia nawapongeza Mabalozi wetu kwa kazi nzuri wanazofanya huko nje. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ya kwangu machache ni ushauri tu. Napenda kushauri Wizara ya Mambo ya Nje wakae na Mifuko ya Jamii. Vile viwanja vyetu vilivyoko nje ambavyo vinahitaji kujengwa wakae na Mifuko ya Jamii wapate pesa wajenge zile nyumba halafu zile pesa wanazolipa kwa maana ya zile nyumba wanazokodi waweze kulipa hiyo Mifuko na kurejesha ili tuweze kuwa na nyumba zetu kwenye Balozi zetu kote duniani ambapo tuna Balozi. Hilo ni jambo la kwanza. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini jambo la pili naomba Mheshimiwa Mahiga ajaribu kuhakikisha kwamba Mabalozi wetu tulionao nje ambao wanatusemea sisi wajitahidi kutafuta nafasi kwa ajili ya vijana wetu watoke nje waende kusoma, kutafuta washirika, misaada, matajiri walioko nje waweze kutu-support kusomesha watoto wetu katika vyuo vikuu vya nje ili waweze kutusaidia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tatu nataka kuzungumzia Chuo cha Diplomasia, napenda kushauri Wizara ijitahidi kuona ni namna gani inaweza kufanya training kwa ajili ya viongozi wetu hata wale wa kisiasa ambao tuko humu Bungeni. Watuletee wataalam tuelimishwe tujue namna gani ya kuishi kwenye mazingira haya ya kidiplomasia kwa maana tujue namna gani ku-behave kwenye community nje ya hapa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini jambo lingine nataka kushauri Wizara ya Mambo ya Nchi za Nje, soko letu la East Africa ni kubwa sana, lakini naomba niseme kuna challenge kubwa sana kwenye East Africa ambayo Tanzania haiendani na nchi nyingine. Ukiangalia kwa mfano Kiwanda cha Maziwa Musoma kilikuwa kinapeleka maziwa Kenya, kilipigwa mizengwe mpaka kikafa lakini leo Kenya ina-import maziwa Tanzania na tunakunywa. Unaweza ku-imagine ni namna gani nchi nyingine ndani ya East Africa zinajaribu kuhakikisha kwamba wawekezaji wao, biashara zao, sisi Tanzania ni market kwao lakini sisi kupeleka kwao inakuwa ni ngumu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano, leo ukipeleka mahindi Kenya lazima upitishe kwa mtu mmoja anunue hayo mahindi hakuna mtu mwingine mpaka yeye anunue. Mkenya akitoka Kenya kuja hapa lazima aingie Kiteto anunue kwa mkulima aende Hanang, Simanjiro, Iringa hakuna control, it means wao wako aware.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuishauri Wizara hii ijaribu ku-create watu ambao ni business attaché kwenye hizo embassies, wawe aware, waangalie ni namna gani ya ku-control wale watu wanaokuja lakini na wale watu ambao wako kule ili wananchi wetu waweze kupeleka biashara huko na sisi bidhaa zetu ziuzike huko kama ambavyo bidhaa zao zinavyoweza kuuzika hapa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kazi kubwa Wizara hii wanafanya lakini liko jambo moja nimejiuliza nikashindwa kupata majibu. Kama miaka miwili iliyopita magari yetu mengi yalikuwa yanapeleka mizigo Congo, Rwanda na Burundi. Leo naomba niwape swali moja jepesi, ukitoka Dar es Salaam kukanyaga Dodoma unakutana na magari ya Rwanda zaidi ya mia, nimejiuliza ni kwa nini? Sisi wakati tunapeleka ile mizigo madereva wetu walikuwa wana kazi, turnboy kazi, magari yetu yanakunywa mafuta hapa, creation ya employment ipo, sasa leo kwa sababu ya kushindwa kukabiliana na uwezo wa kupeleka mizigo, kuleta mizengwe mizengwe hapa katikati tumesababisha na kuwaamsha wale sasa wako kikazi zaidi. Hebu jiulizeni tumepoteza shilingi ngapi kwenye nchi yetu?
Mheshimiwa Mwenyekiti, niwaombe na kuwashauri mjaribu kuwa watu wa kukabiliana na hali ya soko, tuko kwenye East Africa, soko linatosha, opportunities zilizopo nyie ndiyo mnatakiwa mtuambie kuna hili, fanyeni hili ili Watanzania wetu waweze ku-benefit kwenye hizi nchi ambazo sisi ni Wanajumuiya. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kushauri jambo lingine. Huko nje Mabalozi wetu wanazo kazi lakini kazi kubwa ambayo wanatakiwa kuifanya sasa ni ya ku-market Tanzania kwa maana ya uwekezaji, kwa maana ya kututafutia mashirika makubwa na ku-monitor pesa zao zinakuja kufanya nini hapa. Hawa watu wanaokuja kwa kujipenyeza tutashtukia siku nyingine watu wanaingiza pesa hapa, wananyonya uchumi wetu na hatujui na wanajiita wawekezaji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, laundry money zitatembea hapa, uchumi na shilingi yetu itashuka, Watanzania tutabaki maskini wenzetu wakichakachua pesa. Niombe Waziri mwenye dhamana na Mabalozi wetu wajaribu kusimamia hili, waliangalie kwa ukaribu na wajitahidi kuhakikisha kwamba nchi yetu haipotezi na sisi tuna-benefit kutokana na hizo nchi ambazo wao wanaziwakilisha. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo, niwashukuru sana, niwaombe kwa jinsi wanavyoweza wajitahidi kufanya kazi hiyo. Watu wanabeza kwamba Tanzania haijafanya kitu, hatuwezi ushirikiano, hatuwezi umoja, hebu angalieni siku ya kukumbuka Uhuru wetu wageni wa kimataifa wanaokuja kushangilia nchi yetu. Hii ni indication kwamba Tanzania ina heshima ndani ya Afrika, ina heshima ndani ya dunia, kubali usikubali Tanzania kuna kitu imefanya katika investment ya umoja na diplomacy ndani ya dunia hii. Niwaombe mnaotubeza na nyie njooni na njia mbadala ya kutuambia tutoke hapa twende vipi badala ya kubeza yale ambayo tumekwishayafanya, hongereni sana kama Wizara.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kushukuru sana na naunga mkono hoja.