Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Dunstan Luka Kitandula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkinga

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. DUNSTAN L. KITANDULA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kwa kuunga mkono bajeti ya Wizara ya Mambo ya Nje.
Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, nipongeze jitihada zinazofanyika katika kuanzisha Vituo vya Pamoja vya Utoaji Huduma Mipakani (OSBP). Kituo cha Horohoro/Lungalunga ni miongoni mwa vituo vilivyokamilika. Hata hivyo, kituo hiki kinakabiliwa na tatizo kubwa la maji. Kituo hiki kimejengwa upande wa Tanzania eneo ambalo kuna tatizo kubwa la maji kiasi kwamba wananchi wanalazimika kufuata huduma ya maji umbali mrefu upande wa Kenya. Halmashauri ya Mkinga imejitahidi kuibua miradi itakayokuwa suluhisho la tatizo la maji katika eneo hili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tayari ripoti ya detailed design imepatikana ikionesha kuwa mradi huu unahitaji kiasi cha takribani shilingi bilioni sita na nusu. Halmashauri ya Mkinga haina uwezo wa kifedha wa kujenga mradi huu. Nashauri Wizara ya Mambo ya Nje ichukue mradi huu kwa kutafuta fedha toka vyanzo vya Jumuiya ya Afrika Mashariki au ufadhili mwingine wowote utakaowezesha kutekelezwa kwa mradi huu. Itakuwa jambo la aibu endapo kituo hiki kitafunguliwa bila ya kuwepo jawabu la utatuzi wa tatizo hili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo lingine ni European Union kushinikiza nchi za kiafrika kutia saini mkataba ujulikanao kama Economic Partnership Agreement. Mkataba huu ni mbovu na una madhara makubwa kiuchumi kwa nchi za kiafrika Tanzania ikiwemo. Taifa linapaswa kuwa na tahadhari kubwa na mkataba huu hususan sasa ambapo kama Taifa tumedhamiria nchi yetu kuwa nchi ya uchumi wa kati.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali iweke wazi ndani ya Bunge hili msimamo wetu kama nchi kuhusiana na jambo hili. Waziri atakapokuwa anafanya
majumuisho alieleze Bunge lako ni kwa vipi nchi yetu itaachana na mkataba huu wa kinyonyaji. Wizara ilishirikishe mapema Bunge katika kufahamu kwa undani suala hili la EPA ili Wabunge wawe na uelewa mpana utakaowawezesha kufanya maamuzi sahihi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa haya machache, naunga mkono hoja.