Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Willy Qulwi Qambalo

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Karatu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. QAMBALO W. QULWI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nchi yetu ilikuwa na mzozo wa mpaka na nchi ya Malawi ndani ya Ziwa Nyasa. Naomba Waziri aliambie Bunge hili mzozo huo umefikia hatua gani maana kwenye hotuba yake hajaugusia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nchi yetu ni kati ya nchi zenye vivutio vya utalii vinavyopendwa duniani. Sijui ni kwa kiasi gani Ofisi zetu za Ubalozi zinasaidia kutangaza vivutio hivyo. Nchi ya China hivi sasa inakuja juu sana kuleta watalii, nimshauri Mheshimiwa Waziri na Maafisa wake wajipange kutangaza nchi yetu ili tupate fedha za kigeni.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni jambo jema kuwa na utangamano wa Afrika ya Mashariki lakini isiwe ni kigezo cha kuwanyima watu wetu fursa za kiuchumi. Ni jambo lisilopendeza kabisa kuona hata kazi zile ambazo vijana wetu wanaweza kufanya zinafanywa na wageni toka nchi za nje. Mfano ukienda kwenye hoteli za kitalii na mashamba ya wawekezaji kazi za kuhudumia wageni hotelini au kusimamia vibarua mashambani zinafanywa na watu kutoka nje. Mbaya zaidi wageni hao wanawanyanyasa watu wetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mpaka wa Kenya pale Namanga kuna urasimu mkubwa upande wa Tanzania. Wakati wenzetu wa Kenya upande wao wa mpaka mambo yanaenda haraka, ukija upande wa Tanzania hata kule kugonga muhuri inachukua muda sana.