Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2015, Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Mohamed Omary Mchengerwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rufiji

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2015, Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA: Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote, naomba nianze kwanza kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu kunijalia afya njema kusimama mbele ya Bunge lako hili Tukufu. Pili, niwaombe Watanzania nchini kuendelea kupuuza kauli za wanasiasa waliochoka (wazee) ambao mimi nawaita wanasiasa wenye vioja wasiokuwa na hoja. Hivi karibuni kwenye Kigoda cha Mwalimu yupo mwanasiasa mmoja amediriki kumtukana Rais wa Awamu ya Nne, tunamshauri afuate Kanuni 21 ya Kanuni za Uongozi zinazowataka viongozi kufanya tafiti kabla ya kutoa kauli zao, nimeona niliseme hilo kwanza. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pili, nikupongeze kwa kuchaguliwa na Bunge hili kuwa Naibu Spika wa Bunge letu hili. Tunaongozwa na Ibara ya 86 ambapo sisi Wabunge ndiyo tumekuchagua. Pia Ibara ya 89 inatoa Kanuni za Kudumu za Bunge ambazo ni jukumu letu sisi Wabunge kuzifuata ili sasa tunapokuwa na malalamiko tuyaelekeze huko kwa mujibu wa Kanuni za Kudumu za Bunge. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, akinamama wapongezwa sana humu ndani ya Bunge lako hili Tukufu na mimi niseme tu kwamba, nawapongeza akinamama wote ndani ya Bunge hili na bila kumsahau mke wangu mpenzi Tumaini Mfikwa (Mrs. Mchengerwa na binti yangu Ghalia).
Mheshimiwa Naibu Spika, pia niseme hayo nikinukuu yale maneno ya Bibi Titi Mohamed aliyotoa miaka ile ya 55 ambapo bibi huyu kwa mujibu wa wazalendo, wapigania uhuru wa nchi hii wanasema alikuwa ni baada ya Mwalimu Nyerere maana alikuwa tayari kuvunja ndoa yake kwa ajili ya kupigania uhuru wa nchi hii. Nami nawapongeza akinamama wote nchini kwa juhudi kubwa za kupambana na mfumo dume katika nchi yetu hii unaotumiwa na Viongozi wa Chama cha Upinzani. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, niliona nianze na hilo na nirudi sasa kujikita kwa mujibu wa Kanuni ya 106 ya Kanuni za Kudumu za Bunge hili ambayo inanipasa nizungumze bila kuomba mabadiliko katika bajeti yetu hii iliyowasilishwa na Mheshimiwa Waziri. Nami niseme kwamba naunga mkono hotuba hii ya bajeti kwa asilimia mia moja, lakini nitakuwa na reservation zangu ambazo nitaomba Mheshimwa Waziri wa Fedha atakapofika hapa aweze kujibu baadhi ya hoja za msingi ambazo naamini kwamba zitasaidia katika kuinua uchumi wa nchi yetu hii.
Mheshimiwa Naibu Spika, nikianzia kwanza kwa Kanuni za Sera ya Fedha zilizotolewa mwaka 2016 lakini pia hotuba ya Mheshimiwa Waziri wa Fedha katika ukurasa wa 16 unaozungumzia takwimu za umaskini. Nimefanya tafiti sana na kugundua kwamba takwimu zilizotolewa na Mheshimiwa Waziri amezipata kutoka kwa Halmashauri ya kuonesha kwamba Mkoa wa Pwani ni mkoa tajiri kuliko Mkoa wa Mwanza.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niseme kwamba Mheshimiwa Waziri amedanganywa kabisa kwani Mkoa wa Pwani ni miongoni mwa mikoa maskini kabisa katika nchi hii pamoja na Mikoa yote ya Kusini. Labda kama kuna ajenda ya siri sisi watu wa Pwani tusiyoijua, basi tunaomba Mheshimiwa Waziri atueleze hizo ajenda ambazo sisi hatuzijui.
Mheshimiwa Naibu Spika, hapa nitazungumzia takwimu, ukurasa wa tano wa taarifa ya Mkurugenzi iliyokwenda kwa Mheshimiwa Waziri ambayo Mheshimiwa Waziri ameitumia katika Bunge lako hili Tukufu inaonesha kwamba Watanzania wa Rufiji wanaishi kwa kipato cha Sh. 25,000 kwa siku, huu ni udanganyifu wa hali ya juu. Niseme tu kwamba hakuna Mrufiji anayeishi kwa Sh. 25,000 na hii siyo kwa Rufiji tu hata kwa Mkoa mzima wa Pwani hilo suala ni la uongo wa hali ya juu.
Mheshimiwa Naibu Spika, takwimu hizi zinaonesha kwamba wananchi wa Mkoa wa Pwani wanapata pato la zaidi ya Sh. 700,000 kwa mwaka, huu ni uongo wa hali ya juu. Mimi kama Mwanasheria niko tayari kula kiapo kuthibitisha kwamba uongo huu haukubaliki ndani ya Bunge lako hili Tukufu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, takwimu zinaonesha kwamba Rufiji tuna zaidi ya square kilometers 500,000 ambazo hizi zilipaswa zitumike kwa ajili ya kilimo, eneo hili kubwa liko ndani ya bonde la Mto Rufiji. Takwimu pia zinaonesha kwamba ni asilimia 0.6 tu pekee ya wananchi wa Jimbo la Rufiji ambao wanajishughulisha na kilimo katika maeneo haya. Pia ikumbukwe kwamba zaidi ya asilimia 99 ya wananchi wa Jimbo la Rufiji wanategemea kilimo, lakini kilimo hiki hata pale wakati ambapo tuliona matrekta yanakwenda maeneo mbalimbali Rufiji hatujawahi kuona trekta hata siku moja. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, takwimu hizi nitaendelea kupingana nazo, kwa mujibu wa taarifa ya Mkurugenzi iliyokuja kwa Waziri wa Fedha, katika ukurasa wa 23 inaonesha kwamba hata vile Vyama vya Msingi vimeanguka na vinadaiwa na wananchi. Hata ukiangalia wananchi wangu ambao wanategemea korosho, korosho imekwama na imeanguka hata katika soko la dunia. Ukiangalia takwimu wananchi wanadai zaidi ya bilioni moja kwa Vyama hivi vya Msingi.
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa sielewi Mheshimiwa Waziri wa Fedha ana-rely kwenye information baada ya kutuma watu wake kwenda kutafiti na kupata takwimu za msingi kweli vinginevyo Mheshimiwa Waziri wa Fedha atuambie agenda iliyopo ili kama wanataka kupeleka maendeleo sehemu fulani ijulikane, lakini siyo kutumia takwimu za uongo, nami niko tayari kula kiapo kutokana na suala hilo. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, hata ukiangalia bajeti ya kilimo hakuna sehemu yoyote inayozungumzia Rufiji. Waziri wa Kilimo alikiri hilo na akaahidi kupeleka fedha, tunamshukuru kwamba ameahidi kuwasaidia vijana wa Jimbo langu la Rufiji.
Mheshimiwa Naibu Spika, ukisoma ukurasa wa 35 wa hotuba ya Mheshimiwa Waziri wa Fedha, inazungumzia kwamba zaidi ya 4.9 percent ya bajeti ya Serikali itakwenda kwenye kilimo lakini Rufiji haipo katika maeneo hayo. Kwa hiyo, hii inaonesha wazi kwamba takwimu zilizotolewa ni za uongo na tunamwomba Waziri wa Fedha sasa kujikita katika kusaidia wananchi wanyonge na maskini. Tunategemea sasa asilimia 40 ya pato hili la Taifa ikasaidie wananchi wanyonge.
Mheshimiwa Naibu Spika, turudi katika suala zima la elimu. Tarehe 5 Machi, 1998, Mwalimu Nyerere aliwahi kusema:-
“Nobody is asking us to love others more than we love ourselves; but those of us who have been lucky enough to receive a good education have a duty also to help to improve the well-being of the community to which we belong; is part of loving ourselves!” (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, Mwalimu alisisitiza akisema kwamba:-
“Education should be for service and not for selfishness”.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimeona niliseme hili kwa sababu Rufiji tuna shule moja tu ya sekondari kidato cha tano na cha sita japokuwa Rufiji ilianzishwa miaka ile ya 1890. Mgawanyo wa pato la Taifa ni kikwazo kikubwa na tunaona kwamba asilimia 40 iliyotengwa kwa ajili ya maendeleo haitawafikia wananchi wanyonge hususani wa Jimbo langu la Rufiji. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, hivi majuzi niliuliza swali kuhusu wananchi wangu wa Jimbo la Rufiji wa Tarafa ya Ikwiriri ambao wanapata maji kwa asilimia ndogo tu. Nilipokea majibu hapa kutoka kwa Waziri akituambia kwamba kiasi cha fedha tulichoomba kwa ajili ya ununuzi wa mota tusubiri bajeti ya 2017/2018, huu ni uonevu wa hali ya juu. Hawa ni wananchi wachache wasiopata maji safi na salama wanaambiwa wasubiri bajeti ya mwaka ujao ili kutoa shilingi milioni 36 tu. Ikumbukwe kwamba katika bajeti ya Mheshimiwa Waziri kuna maeneo ambapo wametengewa zaidi ya shilingi bilioni 100 ya maji sisi Rufiji hakuna hata senti moja. Huu ni uonevu wa mgawanyo wa pato la Taifa.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba ninukuu hapa maneno ya Mwandishi Mashuhuri wa mashairi na mwanaharakati, Maya Angelou ambaye aliwahi kusema:-
“People will forget what you did, but people will never forget how you made them feel”.
Mheshimiwa Naibu Spika, mimi nasema kwamba, maneno ya Mheshimiwa Waziri wa Maji yametufanya tusononeke na tuumie sana katika mioyo yetu kwa kuwa eneo hili la Rufiji ndiyo pekee lenye shida ya upatikanaji wa maji safi na salama.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba ninukuu Kanuni 21 za Uongozi, zinazozungumzia The Law of Solid Ground…

MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA: Mheshimiwa Naibu Spika, Dkt. Maxwell aliwahi kusisitiza neno moja la kuwataka...

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Mchengerwa, nilifikiri unamalizia kwa kuunga mkono hoja, muda umekwisha.

MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA: Hapana siwezi.