Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Rhoda Edward Kunchela

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Katavi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. RHODA E. KUNCHELA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Diplomasia ya Uchumi. Mheshimiwa Waziri pamoja na kusoma hotuba ya Wizara kuna mipango mingi mizuri hasa ya namna gani tunaweza kukuza uchumi wetu kupitia balozi zetu za nje ya nchi. Najielekeza katika balozi zetu hasa uendeshaji wa balozi zetu, Majengo (Pango), wafanyakazi katika Balozi, biashara zinazoweza kuingiza kipato.
Mheshimiwa Mwenyekiti, uendeshaji wa Balozi; kumekuwa na gharama kubwa za uendeshaji katika balozi zetu kutokana na Balozi nyingi kupanga majengo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pango la ofisi; kutokana na kukosa majengo ya ofisi, Balozi zimekuwa zikipanga, kitu ambacho ni gharama kubwa ukizingatia Balozi nyingi hawapati bajeti ya kutosha ya uendeshaji na hivyo pesa nyingi zinaishia kulipa kodi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nini kifanyike? Ni muda sasa wa Serikali kujikita katika kuhakikisha Balozi zinapewa bajeti ya kutosha ili wamiliki majengo kama ofisi na hivyo kuondoa aibu wanayoipata sasa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kushindwa kulipa kodi Zimbabwe. Licha ya Balozi kwa sasa kumiliki nyumba kama ofisi lakini pia inamiliki baadhi ya biashara kama Tanzania Club. Watanzania hupangishwa au mtu mwenye vigezo kuweza kuendesha lakini sasa Serikali ihakikishe inasimamia miradi hiyo kwa sababu kumekuwa na ubadhirifu mkubwa wa mali za Serikali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, fursa za ajira nje ya nchi; pamoja na Tanzania kuwa na fursa za kiuchumi tumeona tatizo la wageni kupewa fursa kirahisi rahisi tu, kitu ambacho ukienda nje ya Tanzania si rahisi kupata fursa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Work Permit; Serikali sasa ihakikishe inaweka sheria ambazo zitawabana wageni kutimiza vigezo vya uwekezaji na si kupata fursa za ajira kirahisi rahisi kama ilivyo sasa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Watanzania wamekuwa wakipoteza fursa za ajira huku wageni wakipewa kazi hizo. Zimbabwe si rahisi kupata work permit. Imefikia hatua Watanzania wamekaa kule zaidi ya miaka 10 lakini kupata work permit si kazi rahisi na hivyo Zimbabwe ni moja ya nchi ambayo inajipatia pesa kupitia wageni, hivyo Serikali ya Tanzania iwe mfano mzuri ili tukuze uchumi wetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini haya mahusiano ya Kimataifa sasa yawe na msaada kwa ajira mbalimbali za maana, si zao wageni wakija Tanzania wanapewa fursa nzuri na kazi za ngazi ya juu huku Watanzania wakiajiriwa nje ya nchi wanapata kazi zisizo na msingi kama viwandani, kusafisha viwanja vya mipira, kulea wazee na kuwasafisha wazee. Ifike sehemu sasa Watanzania waheshimiwe kwa sababu wageni wakija Tanzania wanaheshimika na kupewa fursa zenye maslahi mazuri kwao na si kunyanyasika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, balozi zitafute fursa mbalimbali za kiuchumi kwa kufungua miradi mbalimbali kama vile maduka ya vitu vya asili ya Tanzania vitakavyouzwa katika balozi zetu na zisibweteke na kukosa fedha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, usalama wa Watanzania wanaoishi nje ya nchi. Tanzania imekuwa kimya sana, Watanzania wanateswa na wananyanyaswa na kuuliwa lakini Serikali imekuwa ya upole bila kutoa matamko makali kama nchi. Mbona wageni wakija Tanzania wanaishi kwa usalama na Serikali inalinda diplomasia ya nje ya Tanzania?
Mheshimiwa Mwenyekiti, hadhi ya balozi zetu ni mbaya katika maeneo yafuatayo:-
Mishahara ya wafanyakazi katika balozi zetu, ukarabati wa ofisi zetu, majengo mengi hayana hadhi ya Balozi za Tanzania na ukizingatia majengo ya balozi baadhi unakuta yako nje ya miji mbali na mjini.