Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Makame Mashaka Foum

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. MAKAME MASHAKA FOUM: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza namshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunijalia kuchangia Wizara hii. Pia namshukuru Waziri pamoja na watendaji wake wote kwa kazi kubwa ya kuiongoza Wizara hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimeona ajabu kwa Wapinzani kwamba kazi yao kubwa ni kuelezea kasoro kwa Serikali. Je, hakuna mema yaliyofanywa na Mabalozi wetu? Yako mengi sana, kama kuanzisha Balozi katika nchi mbalimbali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mabalozi wetu waongeze jitihada kubwa ya kuitangaza Tanzania katika suala la utalii. Nchi yetu ina vivutio vingi vya utalii kama mbuga za wanyama sehemu za kihistoria, fukwe nzuri Zanzibar na Tanganyika. Pia bahari yetu ina vivutio vingi, kwa mfano aina ya papa huko Mafia ambao hawapatikani sehemu nyingine duniani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunawaomba Mabalozi kufanya kazi ya kutafuta wawekezaji wakubwa hasa kwa upande wa utalii. Tunayo fursa nzuri ya kuwapata watalii wa daraja la kwanza iwapo tutapata wawekezaji wakubwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la Mjusi wa Kihistoria (mabaki) Aliye Ujerumani; namshauri Waziri kuharakisha utaratibu mzuri wa kupata mafao au manufaa yatokanayo na mjusi huyo kwa nchi yetu ya Tanzania.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono kwa asilimia mia moja.