Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. James Kinyasi Millya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Simanjiro

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. JAMES K. MILLYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Tanzania ina nafasi gani katika ushirikiano wa kibiashara kwenye ukanda wa Kusini mwa Afrika?
Mheshimiwa Mwenyekiti, ndugu zetu wa kifugaji wanaokwenda Zambia na Afrika ya Kusini, wamekwenda kwa ajili ya kusuka nywele za akinamama kwa “style ya kimasai.” Ni sisi pekee nchi hii na Afrika ambao tunaweza kusuka nywele hizi na hazisukwi na mtu mwingine yeyote. Matatizo na adha wanayokumbana nayo wenzetu wa Kimasai katika nchi hizi mbili ni haya yafuatayo:-
(1) Wanakatwa, wanapigwa na kuhukumiwa bila kupewa usaidizi wa kisheria;
(2) Zambia kama nchi, imekuwa ikiwahukumu “Wamasai” bila kuwapa msaada wowote wa kisheria “fair hearing” trial hazifanyiki.
(3) Tunaiomba nchi ya Zambia ituambie wafugaji hawa wafanye nini ili wakidhi vigezo vya kufanya kazi nchini huko?
(4) Balozi wa Tanzania (Lusaka) amekuwa “reluctant” katika kuwasaidia vijana wetu wanaopata matatizo nchini Zambia. Naomba Balozi wa SADC atazame hili ili watusaidie kuwaondolea vijana wetu shida wanayokumbana nayo.
(5) Tunaomba vijana wetu waliofungwa kwenye Magereza ya Zambia wasaidiwe. Wapo wengi Magerezani na sijui kama Wizara ina takwimu zozote. Please hili lifuatiliwe pia.