Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Anastazia James Wambura

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. ANASTAZIA J. WAMBURA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nampongeza Mheshimiwa Waziri Mahiga, Naibu Waziri Kolimba na timu yote ya Watendaji kwa kuandaa vizuri hotuba ya bajeti ya Wizara hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nina ushauri katika maeneo mawili. Kwanza, nashauri Wizara iwekeze katika viwanja vilivyoko nje ili kupata fedha za kuendesha balozi zetu. Kwa mfano, kiwanja tulichopewa na Serikali ya Msumbiji tukakiacha, mwisho wake tunaweza kunyang‟anywa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, Maafisa wa Korea Kusini waliwahi kuja kuongea na Kamati yetu ya Mambo ya Nje na kuialika iende nchini humo ili kuona uwezekano wa kuanzisha Ofisi ya Ubalozi Korea Kusini. Ni ushauri wangu kwamba Wizara ilifanyie kazi hili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja. Ahsante.