Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Joyce John Mukya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. JOYCE J. MUKYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuchangia katika hotuba hii kama nilivyoainisha hapo juu, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuongelea tatizo la wafanyakazi kutopata ajira za kudumu katika Jumuiya ya Afrika Mashariki. Nilishafanya kazi na Jumuiya kabla sijawa Mbunge kuanzia mwaka 2006 mpaka 2009 kama IT Assistant. Wakati najiunga pale nilikuta wafanyakazi wa temporary ambao wanafanya kazi kama vibarua, naweza kusema hadi leo hii ni muda wa miaka 10 na zaidi sasa, baadhi yao hawajaajiriwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujua toka kwa Mheshimiwa Waziri ni lini ajira za hawa wafanyakazi zitatangazwa ili waweze kuajiriwa? Kwa sababu wangekuwa hawatakiwi, wasingekuwepo kazini hadi leo hii. Naweza kukupa majina yao kama utahitaji pia na wengi ni Watanzania.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo lingine, ni Serikali yetu kutopeleka fedha za kuendesha Jumuiya kwa wakati. Mfano, tokea makubaliano ya bajeti iliyopita kati ya Partner States hadi leo hii nchi yetu ya Tanzania haijapeleka au kukamilisha mchango wake wa kuendesha Jumuiya hiyo. Hii ni aibu sana kwa nchi yetu na ukizingatia Jumuiya hii Makao Makuu yake yapo Tanzania. Ilitakiwa tuoneshe mfano kwa nchi wanachama.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo lingine ni wafanyakazi wa ngazi ya profession kutokupatiwa Diplomatic Passports. Kama yalivyokuwa makubaliano ya nchi wanachama, yaani Headquarters Agreement, wafanyakazi wa level hii wanaotoka nchi nyingine wana diplomatic passports isipokuwa nchi yetu. Hili nilishalisemea tena Bungeni mara mbili na Mheshimiwa Waziri akaahidi watapewa kwani ni haki yao, lakini hadi leo imekuwa ni hadithi tu. Kwa hiyo, Mheshimiwa Waziri naomba kujua ni lini watapewa haki yao?
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia wafanyakazi wa Jumuiya wamekuwa na shida ya kupata Work Permit. Ni aibu kubwa sana kwa hili jambo. Mtumishi ana mkataba wa miaka mitano, lakini bado Serikali haimpi Work Permit ya miaka mitano na kusababisha kero kubwa kwa nchi wanachama wanaokuja kufanya kazi nchini ambako ndiyo sehemu Headquarter ilipo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, niende kwenye suala la Wabunge wa Jumuiya ya Afrika Mashariki. Naomba Mheshimiwa Waziri anijibu maswali yafuatayo:-
(1) Ni lini Wizara hii itaanza kukaa na Wabunge wa EAC ili kujadili mambo mbalimbali, kama mtakavyojipangia ratiba, kama Wizara ya EAC ya Awamu ya Nne ilivyokuwa inafanya?
(2) Ni lini mtawapatia ofisi Wabunge wa Tanzania ambao wanaunda Bunge la Afrika Mashariki na waache kufanyia kazi hotelini au nyumbani mwao?
(3) Ni lini Serikali ya Tanzania itaanza kuwapa mikopo ya magari Wabunge wa EAC kama zinavyofanya nchi wanachama, mfano Kenya na Uganda, ili waache kutumia mishahara yao na posho kununua magari?
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.