Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Daniel Nicodemus Nsanzugwako

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kasulu Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. DANIEL N. NSANZUGWANKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja hii. Hata hivyo, niseme machache. Kwanza, nianze na suala la usalama. Katika nchi za maziwa makubwa hali ya usalama ni tete sana, hali siyo shwari katika nchi nyingi za majirani. Kenya hali siyo nzuri; Uchaguzi Mkuu wa mwaka kesho nchini humo inatia shaka kama usalama utakuwepo. Ukabila nchini Kenya sasa ni kidonda ndugu. Hatari iliyopo ni kutengeneza wakimbizi na wengi watakimbilia Tanzania. Tanzania ichukue jukumu la usuluhishi na upatanishi ili tuwe salama.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tumepeleka vijana (Askari) kurejesha amani Kongo; ni jambo jema sana. Tuilinde Kongo kimkakati kama mbia wetu wa biashara na Foreign Service. Anzisheni Ofisi ndogo ya biashara pale Lubumbashi ili tulinde maslahi yetu ya kiuchumi na kibiashara.
Mheshimiwa Mwenyekiti, niongelee kuhusu Mgogoro wa Burundi na Usuluhishi. Juhudi zinazoendelea pale Arusha ni njema sana. Ni vizuri katika usuluhishi ule pia, washirikishwe Viongozi wa Dini hasa Wakristo na Waislamu. Haya ni makundi mahususi ambayo yanaweza kusaidia kuwezesha mawasiliano na maelewano. Zaidi usuluhishi huo pia, ushirikishe Baraza la Wazee (Council of Elders) ambalo linaweza kuundwa na Elders waliopo katika Mkoa wa Kigoma na Wilaya za Biharamulo na Ngara. Tamaduni za maeneo hayo zinafanana sana na hali/mazingira yaliyopo Burundi, hata lugha yetu ni moja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Kituo cha Kutangaza Lugha yetu ya Kiswahili kilichopo Addis Ababa, Ethiopia, kimeendelezwa kiasi gani? Kimeleta ajira ngapi kwa vijana wetu? Tunataka Kiswahili kiwe bidhaa tena bidhaa ambayo itatuongezea mapato kama Taifa. Kwa nini hadi sasa Kiswahili hakitumiki kama lugha rasmi ya EAC? Tatizo ni nini? We have to promote Kiswahili now.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Jumuiya ya Afrika Mashariki ni watumishi wangapi wa vyeo vya juu wameajiriwa pale Head Quarters iliyopo Arusha? Ni watumishi wangapi wa vyeo vya kati walioajiriwa na EAC Head Quarters pale Arusha? Watumishi wa vyeo vya chini/operating staff, wahudumu/drivers ni wangapi? Nataka kujua pia tunavyonufaika na EAC kuwapo katika ardhi ya Tanzania kiajira.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna protocol yoyote katika nchi wanachama za kuhakikisha demokrasia inakua na kustawi katika Jumuiya hii? Kitendo cha kung‟ang‟ania madaraka kwa Viongozi katika Jumuiya hii ni hatari sana, kitaua ustawi wa jamii na uhuru wa watu wetu. Tanzania must take lead; tuzungumze, tushauri na tuongoze juhudi hizi za kujenga demokrasia hii ambayo ni changa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.